Na Aisha Ndumbalo/Iribswahili.
Jeshi la Nigeria limetangaza kuwa magaidi wasiopungua 27 wa kundi la kigaidi na kitakfiri wa Boko wameangamizwa katika mashambulio kadhaa yaliyofanywa na jeshi hilo katika mkoa wa Borno kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
Taarifa iliyotolewa na jeshi la Nigeria imeeleza kuwa magaidi 19 wa kundi la Boko Haram waliuawa katika mapigano na jeshi hilo yaliyotokea kwenye kambi ya Dalore.
Katika mapigano hayo jeshi limefanikiwa pia kuwaokoa watu 67 waliokuwa wametekwa nyara na kundi hilo.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa magaidi wengine saba wa kundi la kigaidi na kitakfiri wa Boko Haram waliuawa katika shambulio la kuvizia lililofanywa na jeshi katika eneo la Dawashi mkoani Borno.
Watu zaidi ya 20,000 wameuawa na wengine zaidi ya milioni 2.5 wamelazimika kuwa wakimbizi ndani na nje ya nchi tangu kundi la Boko Haram lianzishe hujuma zake
nchini Nigeria mwaka 2009.
Mashambulio ya kigaidi ya kundi hilo yamevuka mipaka ya Nigeria na kuenea hadi nchi jirani za Cameroon, Chad na Niger.
No comments
Post a Comment