Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » CHAMA RASHTRIYA SWAYAMSEVAK SANGH (RSS) CHAONDOA KAPTURA KWENYE SARE INDIA
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post


Chama cha mrengo wa kulia cha Wahindi cha Rashtriya Swayamsevak Sangh (RSS) kimetangaza kwamba kitaondoa kaptura za rangi ya kaki kwenye sare yake, baada ya kutumiwa kwa miaka 91.

Sare ya chama hicho, ambayo imejumuisha suruali kipande, za rangi ya kaki sasa itakuwa na suruali ndefu za rangi ya hudhurungi.

Uamuzi huo ulifanywa kwenye mkutano mkuu wa kila mwaka wa viongozi wa chama hicho.
Chama cha RSS, ambacho maana ya jina lake ni Chama cha Taifa cha watu Waliojitolea, ndicho kilichoasisi sera zinazofuatwa na chama tawala cha BJP.

Waziri mkuu wa sasa Narendra Modi aliwahi kuwa mwanachama wa chama hicho.

Katibu mkuu wa chama hicho Suresh Bhaiyyaji Joshi amewaambia wanahabari kwamba mabadiliko hayo yanatokana na hali kwamba chama hicho kinataka kutembea na majira.

Kuhusu rangi, amenukuliwa na shirika la PTI akisema sababu pekee ya kuondoa rangi ya kaki ni kwamba rangi ya hudhurungi hupatikana kwa urahisi na “inapendeza”.

Mabadiliko hayo yatatekelezwa katika kipindi cha miezi sita ijayo.

Chama cha RSS (ambacho pia hujulikana kama Sangh) kilianzishwa 1925 na kimewahi kupigwa marufuku mara tatu tangu uhuru.

Wapinzani wa chama hicho husema ni chama cha kugawanya watu, cha kupenda vita na kinaamini katika “ubabe wa Wahindi” na hueneza chuki dhidi ya Waislamu na Wakristo walio wachache.

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / CHAMA RASHTRIYA SWAYAMSEVAK SANGH (RSS) CHAONDOA KAPTURA KWENYE SARE INDIA


Chama cha mrengo wa kulia cha Wahindi cha Rashtriya Swayamsevak Sangh (RSS) kimetangaza kwamba kitaondoa kaptura za rangi ya kaki kwenye sare yake, baada ya kutumiwa kwa miaka 91.

Sare ya chama hicho, ambayo imejumuisha suruali kipande, za rangi ya kaki sasa itakuwa na suruali ndefu za rangi ya hudhurungi.

Uamuzi huo ulifanywa kwenye mkutano mkuu wa kila mwaka wa viongozi wa chama hicho.
Chama cha RSS, ambacho maana ya jina lake ni Chama cha Taifa cha watu Waliojitolea, ndicho kilichoasisi sera zinazofuatwa na chama tawala cha BJP.

Waziri mkuu wa sasa Narendra Modi aliwahi kuwa mwanachama wa chama hicho.

Katibu mkuu wa chama hicho Suresh Bhaiyyaji Joshi amewaambia wanahabari kwamba mabadiliko hayo yanatokana na hali kwamba chama hicho kinataka kutembea na majira.

Kuhusu rangi, amenukuliwa na shirika la PTI akisema sababu pekee ya kuondoa rangi ya kaki ni kwamba rangi ya hudhurungi hupatikana kwa urahisi na “inapendeza”.

Mabadiliko hayo yatatekelezwa katika kipindi cha miezi sita ijayo.

Chama cha RSS (ambacho pia hujulikana kama Sangh) kilianzishwa 1925 na kimewahi kupigwa marufuku mara tatu tangu uhuru.

Wapinzani wa chama hicho husema ni chama cha kugawanya watu, cha kupenda vita na kinaamini katika “ubabe wa Wahindi” na hueneza chuki dhidi ya Waislamu na Wakristo walio wachache.

«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :