zaidi ya watu mia tatu wakaazi wa kijiji cha kikombo
mkoani dodoma wamebakia katika hali ya sinto fahamu baada ya mtu mmoja asiyejulikana
kujimilikisha maeneo ya wanakijiji hao bila ya uongozi wa kijiji hicho kuwa na
taarifa.
Wakizungumza na rasi fm wakaazi wa kijiji hicho
wamesema kuwa mtu aitwaye Ernest Kato amejimilikisha maeneo pasipo kuwashirikisha
wanakijiji hao nakutaka kuanza shughuli za uchimbaji wa mchanga jambo
lililowafanya wanachi kuiomba wizara ya madini kuweza kuifuta leseni hiyo ili kuweza
kuokoa vyanzo vya maji na mazingira.
&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&
Kiwanda cha Saruji Tanga (Simba Cement),
kimeingia makubaliano na Shirika la Reli Tanzania (TRL), kusafirisha shehena ya
saruji kwa njia ya reli kutoka mkoani Tanga kwenda mikoa ya Mwanza na Kigoma.
Chini ya Makubaliano hayo zaidi ya tani laki
nne na nusu zitasafirishwa kwa mwaka na hivyo kupunguza gharama ya bei ya
Saruji katika mikoa ya Kanda ya Ziwa na Magharibi kutokana na usafirishaji wa
reli kuwa wa bei nafuu.
&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&
Baada
ya kumpata Meya wa Jiji la Dar es Salaam, mchakato wa kumchagua naibu meya
umeanza.
Juzi, Diwani wa Kata ya Vijibweni (Chadema),
Isaya Mwita alichaguliwa kuwa umeya akimshinda mpinzani wake Yusuph Yenga (CCM)
kwa kura 84 dhidi ya 67.
Akizungumza jana, Meya Mwita alisema tarehe
rasmi ya uchaguzi wa kumpata naibu meya haijafahamika na kwamba leo
atashauriana na uongozi wa jiji na kwamba mara tu baada ya Sikukuu ya Pasaka
ataitisha kikao cha baraza.
Amesema kuwa makundi
ya wapiganaji wa Kiislam nchini Syria na Iraq moja ya tishio kwa nchi ya Ulaya
na kwamba yakiachwa yaendelee kustawi yatazitesa nchi za Ulaya
&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&
Baraza la Haki za
Binadamu la Umoja wa Mataifa jana liliitisha kikao kujadili hali ya mambo
nchini Burundi.
Kikao hicho
kilichofanyika mjini Geneva Uswisi kilijadili ripoti ya wataalamu watatu wa
Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kuhusiana na hali ya haki za
binadamu nchini Burundi.
Asasi zisizo za
kiserikali pamoja na nchi wanachama wa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa
Mataifa limeitaka serikali ya Burundi ianzishe mwenendo wa mazungumzo na
wapinzani kwa shabaha ya kuupatia ufumbuzi mgogoro wa kisiasa wa nchi hiyo.
NA
Al-Shabab
imewaarifu wafanyibiashara katika majimbo ya Kusini mwa Somalia na maeneo ya
Lower Shabelle kuwa bidhaa zinazotokea Uturuku ni haramu.
No comments
Post a Comment