Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » » MABALOZI WA NCHI ZA ULAYA NA MAREKANI WAKOSOA KUFANYIKA KWA UCHAGUZI ZANZIBAR
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Mabalozi wa nchi za Ulaya na Marekani wamekosoa uchaguzi wa marudio uliofanyika visiwani Zanzibar Jumapili.
Mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt Ali Mohammed Shein ametangazwa mshindi wa uchaguzi huo na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC).
Chama cha Wananchi (CUF) kilisusia uchaguzi huo.
Mabalozi wa Ubelgiji, Canada, Denmark, Umoja wa Ulaya, Finland, Ufaransa, Ujerumani, Ireland, Italia, Uholanzi, Norway, Uhispania, Sweden, Uswizi, Uingereza na Marekani wamesema uchaguzi huo haukufaa kufanyika bila ya kuwepo kwa maafikiano kuhusu suluhu ya mzozo wa kisiasa visiwani humo.
“Ili uchaguzi uwe wa kuaminika, ni lazima ushirikishe wote na uwe unaakisi nia ya watu,” mabalozi hao wamesema kupitia taarifa.
“Tunakariri wito wetu kwa Serikali ya Tanzania kutoa uongozi Zanzibar na kufanikisha suluhu kupitia mashauriano kati ya vyama, kwa lengo la kudumisha amani na umoja katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mabalozi hao walionekana kutoa wito kwa Rais John Magufuli kusaidia katika utatuzi wa mzozo huo.
Kiongozi huyo hata hivyo tayari amesema kwamba hataingilia mzozo katika visiwa hivyo.
Kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa na ZEC, Dkt Shein alipata kura 299,982 ambazo ni sawa na asilimia 91.4 ya kura zilizopigwa.
Mgombea urais wa chama cha ADC Hamad Rashid Mohammed aliibuka wa pili na kura 9,734 (3.0%).
Bw Seif Sharif Hamad wa CUF alipigiwa kura 6,076 (1.9%) licha ya kwamba chama chake kilisusia uchaguzi huo.

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / / MABALOZI WA NCHI ZA ULAYA NA MAREKANI WAKOSOA KUFANYIKA KWA UCHAGUZI ZANZIBAR

Mabalozi wa nchi za Ulaya na Marekani wamekosoa uchaguzi wa marudio uliofanyika visiwani Zanzibar Jumapili.
Mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt Ali Mohammed Shein ametangazwa mshindi wa uchaguzi huo na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC).
Chama cha Wananchi (CUF) kilisusia uchaguzi huo.
Mabalozi wa Ubelgiji, Canada, Denmark, Umoja wa Ulaya, Finland, Ufaransa, Ujerumani, Ireland, Italia, Uholanzi, Norway, Uhispania, Sweden, Uswizi, Uingereza na Marekani wamesema uchaguzi huo haukufaa kufanyika bila ya kuwepo kwa maafikiano kuhusu suluhu ya mzozo wa kisiasa visiwani humo.
“Ili uchaguzi uwe wa kuaminika, ni lazima ushirikishe wote na uwe unaakisi nia ya watu,” mabalozi hao wamesema kupitia taarifa.
“Tunakariri wito wetu kwa Serikali ya Tanzania kutoa uongozi Zanzibar na kufanikisha suluhu kupitia mashauriano kati ya vyama, kwa lengo la kudumisha amani na umoja katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mabalozi hao walionekana kutoa wito kwa Rais John Magufuli kusaidia katika utatuzi wa mzozo huo.
Kiongozi huyo hata hivyo tayari amesema kwamba hataingilia mzozo katika visiwa hivyo.
Kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa na ZEC, Dkt Shein alipata kura 299,982 ambazo ni sawa na asilimia 91.4 ya kura zilizopigwa.
Mgombea urais wa chama cha ADC Hamad Rashid Mohammed aliibuka wa pili na kura 9,734 (3.0%).
Bw Seif Sharif Hamad wa CUF alipigiwa kura 6,076 (1.9%) licha ya kwamba chama chake kilisusia uchaguzi huo.

«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :