Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » MATOKEO YA LIVERPOOL BAADA YA KOCHA MPYA HAYA HAPA NA MECHI NYINGINE EUROPA LEAGUE
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Meneja mpya wa Liverpool Jurgen Klopp alishindwa kuandikisha ushindi mechi yake ya kwanza Anfield baada ya vijana wake kulazimishiwa sare ya 1-1 na Rubin Kazan katika Europa League.

Wageni wao walichukua uongozi kupitia Marko Devic lakini nahodha wao Oleg Kuzmin alifukuzwa uwanjani baada ya kuonyeshwa kadi ya pili ya manjano muda mfupi baadaye.

Liverpool walijibu kupitia Emre Can baada ya kuchapwa kwa frikiki.

Nguvu mpya Christian Beneteke alikosea pembamba kuwafungia la pili baada ya kombora lake kugonga mlingoti wa goli na mwishowe Liverpool wakakubali kuondoka na sare ambayo ndiyo ya tatu mtawalia katika mechi zao Kundi B.

Licha ya kujikakamua sana dakika za mwisho, haukuwa usiku mwema kwa Klopp na Liverpool kwani walishindwa kupenya ngome ya wapinzani wao vipindi virefu vya mechi hiyo.

Matokeo hayo yamewaacha Liverpool nambari mbili katika kundi lao wakiwa na alama tatu, alama nne nyuma ya viongozi FC Sion.

Liverpool sasa wametoka sare mechi saba kati ya nane walizocheza karibuni zaidi.

Akizungumza baadaye, Klopp alisema: "Unapoingia kwenye nyumba mpya, huwa unapokea zawadi. Sijafurahishwa na zawadi niliyoipata leo".

Kwenye mechi nyingine zilizochezwa Alhamisi, matokeo yalikuwa kama ifuatavyo:

Molde 3 - 1 Celtic
Anderlecht 2 - 1 Tottenham Hotspur
Liverpool 1 - 1 Rubin Kazan
Fenerbahçe 1 - 0 Ajax
Monaco 1 - 0 FK Qarabag
Apoel Nic 2 - 1 Asteras Tripolis
Schalke 2 - 2 Sparta Prague
AZ Alkmaar 0 - 1 FC Augsburg
Partizan Belgrade 0 - 2 Athletic Bilbao
Bordeaux 0 - 1 FC Sion
FK Qabala 1 - 3 Borussia Dortmd

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / MATOKEO YA LIVERPOOL BAADA YA KOCHA MPYA HAYA HAPA NA MECHI NYINGINE EUROPA LEAGUE

Meneja mpya wa Liverpool Jurgen Klopp alishindwa kuandikisha ushindi mechi yake ya kwanza Anfield baada ya vijana wake kulazimishiwa sare ya 1-1 na Rubin Kazan katika Europa League.

Wageni wao walichukua uongozi kupitia Marko Devic lakini nahodha wao Oleg Kuzmin alifukuzwa uwanjani baada ya kuonyeshwa kadi ya pili ya manjano muda mfupi baadaye.

Liverpool walijibu kupitia Emre Can baada ya kuchapwa kwa frikiki.

Nguvu mpya Christian Beneteke alikosea pembamba kuwafungia la pili baada ya kombora lake kugonga mlingoti wa goli na mwishowe Liverpool wakakubali kuondoka na sare ambayo ndiyo ya tatu mtawalia katika mechi zao Kundi B.

Licha ya kujikakamua sana dakika za mwisho, haukuwa usiku mwema kwa Klopp na Liverpool kwani walishindwa kupenya ngome ya wapinzani wao vipindi virefu vya mechi hiyo.

Matokeo hayo yamewaacha Liverpool nambari mbili katika kundi lao wakiwa na alama tatu, alama nne nyuma ya viongozi FC Sion.

Liverpool sasa wametoka sare mechi saba kati ya nane walizocheza karibuni zaidi.

Akizungumza baadaye, Klopp alisema: "Unapoingia kwenye nyumba mpya, huwa unapokea zawadi. Sijafurahishwa na zawadi niliyoipata leo".

Kwenye mechi nyingine zilizochezwa Alhamisi, matokeo yalikuwa kama ifuatavyo:

Molde 3 - 1 Celtic
Anderlecht 2 - 1 Tottenham Hotspur
Liverpool 1 - 1 Rubin Kazan
Fenerbahçe 1 - 0 Ajax
Monaco 1 - 0 FK Qarabag
Apoel Nic 2 - 1 Asteras Tripolis
Schalke 2 - 2 Sparta Prague
AZ Alkmaar 0 - 1 FC Augsburg
Partizan Belgrade 0 - 2 Athletic Bilbao
Bordeaux 0 - 1 FC Sion
FK Qabala 1 - 3 Borussia Dortmd

«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :