Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » » MAAMUZI YA UKAWA YAWAFIKIA WATUMIAJI WA MITANDAO YA KIJAMII, FB WAMESEMA HAYA BAADA YA UKAWA KUTANGAZA KUTOHUDHURIA KUAPISHWA KWA DR. MAGUFULI
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), Freeman Mbowe amesema kuwa hawatashiriki shughuli ya kuapishwa kwa Dk. John Pombe Magufuli inayotarajiwa kufanyika Alhamis, Novemba 5, 2015.

Kauli hiyo ya Mwenyekiti Mbowe aliyoitoa leo, imekuja wakati kukiwa bado kuna sintofahamu kubwa miongoni mwa Watanzania kuhusu mchakato wa uchaguzi hususan upigaji kura, ukusanyaji na ujumlishaji wa matokeo ulivyofanyika hasa katika nafasi ya urais.

"Hatutahudhuria shughuli hiyo ya kumwapisha Magufuli. Tumekubaliana wote kwenye UKAWA, ndani ya CHADEMA, viongozi wetu, wabunge wetu wote hawatahudhuria uapishwaji wala sherehe.

"Tumetoa wito kwa wananchi wote, Watanzania wote, wapenda mabadiliko na wapenda haki wote kwa ujumla kutohudhuria shughuli hiyo," amesema Mwenyekiti Mbowe.

Mwenyekiti Mbowe amesisitiza kuwa UKAWA, wapenda mabadiliko wote na Watanzania wapenda haki hawakubaliani na wanapinga mchakato wa uchaguzi hususan matokeo ya urais ambayo, kwa mujibu wa Katiba ya Nchi aliyosema ni mbovu, yakishatangazwa hakuna haki ya kuyapinga katika mahakama yoyote ile.

"Tunataka nchi na dunia nzima ijue wazi kuwa hatukubaliani na mchakato wa uchaguzi hasa matokeo ya urais ambayo kwa mujibu wa Katiba yetu mbovu, Mwenyekiti wa Tume akishatangaza hakuna mahali pa kuyapinga."

"Matokeo ya ubunge au udiwani yanaweza kupingwa mahakamani, lakini kwa matokeo ya urais Katiba yetu mbovu inawafunga mikono na miguu Watanzania wote ambao wangependa waone haki imetendeka katika nafasi hiyo," amesema Mwenyekiti Mbowe.

"Watawala wamechezea haki ya Watanzania kupiga kura. Kura zimehesabiwa kama karatasi za kawaida tu. Hujuma dhidi ya matokeo ya wagombea wetu imehujumiwa waziwazi. Safari hii hujuma hazikuwa kificho tena.

Kila mtu amejionea matokeo yaliyokuwa na Jaji Lubuva si yale ambaye yalikuwa yamebandikwa vituoni. Hayakuwa na uhalisia na matokeo yaliyokusanywa na mawakala.

Uchaguzi umefanywa kama ni jambo lisilokuwa na maana yoyote. Hiyo ni hatari sana kwa taifa lolote linalotaka kukuza demokrasia kama mojawapo ya nguzo za maendeleo. Hatuwezi kukubali kufika huko," amesema Mbowe.

Aidha, Mwenyekiti Mbowe ameongeza kusema kuwa vyama vinavyounda UKAWA vimeitisha kikao cha Wabunge wateule wote wa vyama hivyo ambao watakutana Alhamis, saa 4 asubuhi, jijini Dar es Salaam.

Imetolewa leo Jumatano Novemba 4, 2015 na;
Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano

Coments za watumiaji wa Facebook

117 people like this.
Comments
George Kulwa Kama ni Kweli basi Lowasa atakuwa kawamaliza UKAWA na mimi rasmi kesho nachukua kadi ya CCM ili niutoe mchango wangu kuijenga nchi yangu kuputia CCM tanzania sio lowasa na Lowasa hawezi kuwa tanzania
Like · Reply · 2 · 8 hrs
Doyo Hasan Doyo
Doyo Hasan Doyo Itasaidia Nini
Respicius Joseph
Respicius Joseph mkapimwe kama hamuwezi kuamini kwamba mmeshindwa basi kuna shida ndani yenu Mgufuli ndiye raisi jaman amin
Like · Reply · 1 · 8 hrs
Enatha Lutha
Enatha Lutha lkn ninaimani watabaki nyumbani wakitazama tv zao na kushudia rais wetu mteule akiapishwa
Like · Reply · 1 · 8 hrs


Seiph Akili
Seiph Akili tumeshawazowea mbona hata 2010. hawakuwepo na hakuna kilicho halibika
Like · Reply · 2 · 7 hrs
Juma Ndaro
Juma Ndaro Mkisusa Wenzenu Tunakula - Aibu Yenu Aibu Yao!
Like · Reply · 1 · 6 hrs
Nzellah Nzellah
Nzellah Nzellah Kudondoka kwa nyasi (jani ) moja ktk nyumba hakuifanyi nyumba hiyo kuvuja.
Like · Reply · 2 · 6 hrs
Meshack Festo
Meshack Festo Huo n umbulula kutokuhudhiria hakuna maana yoyote
Shafiyu Hamad
Shafiyu Hamad mbowe acha ujinga kama unataka demokrasia kwanza ijenge kwenye chama chako kwani haipo kabisa kwani uteuzi wa mgombea uraisi uri ufanya mwenyewe arafu eti una dai demokrasia tz!!
Like · Reply · 1 · 3 hrs
Ally Ibn Walid
Ally Ibn Walid ccm chaguo letu wenyewe tuipenda wenyewe acha waisome namba kina mbowe
Alex Gideon
Alex Gideon Alafu kesho watakuja hapa watasema hooo katika hotuba yake leo ametusema sana, sasa umeona wapi kawasema wakati mmesema hamtaangalia kuapishwa kwake?
Like · Reply · 1 hr · Edited
Mwanja Ibadi
Mwanja Ibadi hapa kazi tu
Rajabu Kongoi
Rajabu Kongoi Nitaona kweli upinzani wakisusa kwenda Kuala bungeni
Jackline Anthony
Jackline Anthony Wajinga na viroba wanapelekeshwa na xhadema mbowe ana zake uarabunii
Denis Kazenzele
Write a comment...

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / / MAAMUZI YA UKAWA YAWAFIKIA WATUMIAJI WA MITANDAO YA KIJAMII, FB WAMESEMA HAYA BAADA YA UKAWA KUTANGAZA KUTOHUDHURIA KUAPISHWA KWA DR. MAGUFULI

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), Freeman Mbowe amesema kuwa hawatashiriki shughuli ya kuapishwa kwa Dk. John Pombe Magufuli inayotarajiwa kufanyika Alhamis, Novemba 5, 2015.

Kauli hiyo ya Mwenyekiti Mbowe aliyoitoa leo, imekuja wakati kukiwa bado kuna sintofahamu kubwa miongoni mwa Watanzania kuhusu mchakato wa uchaguzi hususan upigaji kura, ukusanyaji na ujumlishaji wa matokeo ulivyofanyika hasa katika nafasi ya urais.

"Hatutahudhuria shughuli hiyo ya kumwapisha Magufuli. Tumekubaliana wote kwenye UKAWA, ndani ya CHADEMA, viongozi wetu, wabunge wetu wote hawatahudhuria uapishwaji wala sherehe.

"Tumetoa wito kwa wananchi wote, Watanzania wote, wapenda mabadiliko na wapenda haki wote kwa ujumla kutohudhuria shughuli hiyo," amesema Mwenyekiti Mbowe.

Mwenyekiti Mbowe amesisitiza kuwa UKAWA, wapenda mabadiliko wote na Watanzania wapenda haki hawakubaliani na wanapinga mchakato wa uchaguzi hususan matokeo ya urais ambayo, kwa mujibu wa Katiba ya Nchi aliyosema ni mbovu, yakishatangazwa hakuna haki ya kuyapinga katika mahakama yoyote ile.

"Tunataka nchi na dunia nzima ijue wazi kuwa hatukubaliani na mchakato wa uchaguzi hasa matokeo ya urais ambayo kwa mujibu wa Katiba yetu mbovu, Mwenyekiti wa Tume akishatangaza hakuna mahali pa kuyapinga."

"Matokeo ya ubunge au udiwani yanaweza kupingwa mahakamani, lakini kwa matokeo ya urais Katiba yetu mbovu inawafunga mikono na miguu Watanzania wote ambao wangependa waone haki imetendeka katika nafasi hiyo," amesema Mwenyekiti Mbowe.

"Watawala wamechezea haki ya Watanzania kupiga kura. Kura zimehesabiwa kama karatasi za kawaida tu. Hujuma dhidi ya matokeo ya wagombea wetu imehujumiwa waziwazi. Safari hii hujuma hazikuwa kificho tena.

Kila mtu amejionea matokeo yaliyokuwa na Jaji Lubuva si yale ambaye yalikuwa yamebandikwa vituoni. Hayakuwa na uhalisia na matokeo yaliyokusanywa na mawakala.

Uchaguzi umefanywa kama ni jambo lisilokuwa na maana yoyote. Hiyo ni hatari sana kwa taifa lolote linalotaka kukuza demokrasia kama mojawapo ya nguzo za maendeleo. Hatuwezi kukubali kufika huko," amesema Mbowe.

Aidha, Mwenyekiti Mbowe ameongeza kusema kuwa vyama vinavyounda UKAWA vimeitisha kikao cha Wabunge wateule wote wa vyama hivyo ambao watakutana Alhamis, saa 4 asubuhi, jijini Dar es Salaam.

Imetolewa leo Jumatano Novemba 4, 2015 na;
Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano

Coments za watumiaji wa Facebook

117 people like this.
Comments
George Kulwa Kama ni Kweli basi Lowasa atakuwa kawamaliza UKAWA na mimi rasmi kesho nachukua kadi ya CCM ili niutoe mchango wangu kuijenga nchi yangu kuputia CCM tanzania sio lowasa na Lowasa hawezi kuwa tanzania
Like · Reply · 2 · 8 hrs
Doyo Hasan Doyo
Doyo Hasan Doyo Itasaidia Nini
Respicius Joseph
Respicius Joseph mkapimwe kama hamuwezi kuamini kwamba mmeshindwa basi kuna shida ndani yenu Mgufuli ndiye raisi jaman amin
Like · Reply · 1 · 8 hrs
Enatha Lutha
Enatha Lutha lkn ninaimani watabaki nyumbani wakitazama tv zao na kushudia rais wetu mteule akiapishwa
Like · Reply · 1 · 8 hrs


Seiph Akili
Seiph Akili tumeshawazowea mbona hata 2010. hawakuwepo na hakuna kilicho halibika
Like · Reply · 2 · 7 hrs
Juma Ndaro
Juma Ndaro Mkisusa Wenzenu Tunakula - Aibu Yenu Aibu Yao!
Like · Reply · 1 · 6 hrs
Nzellah Nzellah
Nzellah Nzellah Kudondoka kwa nyasi (jani ) moja ktk nyumba hakuifanyi nyumba hiyo kuvuja.
Like · Reply · 2 · 6 hrs
Meshack Festo
Meshack Festo Huo n umbulula kutokuhudhiria hakuna maana yoyote
Shafiyu Hamad
Shafiyu Hamad mbowe acha ujinga kama unataka demokrasia kwanza ijenge kwenye chama chako kwani haipo kabisa kwani uteuzi wa mgombea uraisi uri ufanya mwenyewe arafu eti una dai demokrasia tz!!
Like · Reply · 1 · 3 hrs
Ally Ibn Walid
Ally Ibn Walid ccm chaguo letu wenyewe tuipenda wenyewe acha waisome namba kina mbowe
Alex Gideon
Alex Gideon Alafu kesho watakuja hapa watasema hooo katika hotuba yake leo ametusema sana, sasa umeona wapi kawasema wakati mmesema hamtaangalia kuapishwa kwake?
Like · Reply · 1 hr · Edited
Mwanja Ibadi
Mwanja Ibadi hapa kazi tu
Rajabu Kongoi
Rajabu Kongoi Nitaona kweli upinzani wakisusa kwenda Kuala bungeni
Jackline Anthony
Jackline Anthony Wajinga na viroba wanapelekeshwa na xhadema mbowe ana zake uarabunii
Denis Kazenzele
Write a comment...


«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :