Aliyekuwa kiongozi wa muda mrefu wa
Cuba Fidel Castro amevunja kimya chake kuhusu ziara ya hivi majuzi ya
Rais wa Marekani Barack Obama nchini humo.
Fidel, aliyemkabidhi kakake Raul uongozi wa taifa hilo mwongo mmoja uliopita, amesema Cuba haihitaji zawadi zozote kutoka kwa Marekani.
Amesema maneno ya Obama ya kuhimiza maridhiano ni sawa na “rojo ya sukari” na kuonya kwamba raia wa Cuba wanaweza kupata “mshtuko wa moyo”.
Fidel Castro, 89, aliongoza Cuba kuanzia 1959 hadi 2008 alipomkabidhi nduguye madaraka.
No comments
Post a Comment