Na. Lydia Kishia na John Banda
JESHI la polisi Mkoani Dodoma limefanikiwa kukamata silaha 26 aina ya Gobole na mtambo ya kuyatengezea kinyume cha sheria ya umiliki wa siraha.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Dodoma Lazaro Mambosasa amewaambia waandishi wa habari kuwa Magobore 19 yamesalimishwa na wamiliki waliokuwa wakiyamiliki kinyume na sheria baada ya kusikia wito wa Jeshi hilo lililowataka kuzisalimisha.
Mambosasa amesema jeshi hilo pia linawashikilia watu 7 wakazi wa Manda Wilayani Chamwino baada ya kuwakamata na aina hiyo ya silaha 7 pamoja nyundo 1 risasi zilizotengenezwa kienyeji ambazo zinadaiwa zilikuwazikitumiwa kuwindia wanyama katika poli la Ruaha mkoani iringa
Aidha kamanda huyo amesema moja ya Gobole lilikuwa limevishwa shanga ambayo ni ishara ya nguvu za Giza ili polisi wasifanikiwe kuikamata ambapo pamoja na hilo wamefanikiwa kukamata pikipiki zenye makosa mbalimba 250 na kuwatoza wamiliki wake jumla ya million 7 na Laki 2 na 30 Elfu
No comments
Post a Comment