Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » » RUKA NA HIZI HAPA KITAIFA NA KIMATAIFA UFAHAMU MENGI KUTOKA NDANI NA NJE YA TANZANIA..
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

picha maktaba- sio halisi
DODOMA

Jeshi la polisi Mkoani Dodoma limefanikiwa kukamata silaha 26 aina ya Gobole na mitambo ya kuyatengezea silaha hizo kinyume cha sheria ya umiliki wa siraha.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Dodoma Lazaro Mambosasa amewaambia waandishi wa habari kuwa Magobore 19 yamesalimishwa na wamiliki waliokuwa wakiyamiliki kinyume na sheria baada ya kusikia wito wa Jeshi hilo lililowataka kuzisalimisha.

Mambosasa amesema jeshi hilo pia linawashikilia watu 7 wakazi wa Manda Wilayani Chamwino baada ya kuwakamata na aina hiyo ya silaha 7 pamoja nyundo 1na risasi zilizotengenezwa kienyeji ambazo zinadaiwa zilikuwa zikitumiwa kuwindia wanyama katika pori la Ruaha mkoani iringa.

Aidha kamanda huyo amesema moja ya Gobole lilikuwa limevishwa shanga ambayo ni ishara ya nguvu za Giza ili polisi wasifanikiwe kuikamata ambapo pamoja na hilo wamefanikiwa kukamata pikipiki zenye makosa mbalimba 250 na kuwatoza wamiliki wake jumla ya million 7 na Laki 2 na 30 Elfu.



CHANZO: LYDIA KISHIA/JOHN BANDA


 &&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&
  

MWANZA

Mbunge wa jimbo la Bunda,Ester Bulaya amekamatwa na Jeshi la Polisi  jijini Mwanza na kulazimika  kulala  rumande baada ya kunyimwa dhamana.
Polisi wamevamia Hoteli aliyofikia mbunge huyo na kumkamata majira ya saa 7 usiku na kisha  kumpeleka  kituo cha kati cha Jijini Mwanza akiwa ameambatana na Mhe. Halima Mdee, Joyce Sokombe pamoja na Wakili John Malya.

Wabunge hao pamoja na uongozi wa juu wa Chadema Wako jijini Mwanza 
kwa ajili ya kikao cha Baraza Kuu la chama hicho kinachofanyika leo katika Hotel ya Gold Crest.

Kikao hicho pia kinatarajiwa kumpata katibu mkuu mpya kushika nafasi iliyoachwa wazi na Dokta Wilbroad Slaa aliyejiuzuru mwaka uliopita baada ya kushindwa kuelewana katika baadhi ya maamuzi na uongozi wa chama hicho.



CHANZO: MPEKUZIHURU

&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&




DAR ES SALAAM

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amewataka wafanyakazi wa wizara yake kuacha kufanya kazi kwa mazoea kwani Serikali ya imejipanga kutumia sekta ya miundombinu kukuza na kufungua fursa za kiuchumi.

Akizungumza katika kikao kazi kilichohusisha Sekta za Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Mbarawa amemtaka kila mtu afanye kazi kwa umoja, uwazi na uadilifu ili kufikia lengo la kuanzishwa kwa wizara hiyo na kujihakikishia nafasi ya kuendelea kuwa mtumishi wa umma.

Amesema kila mfanyakazi atapewa malengo na atapimwa kulingana na malengo aliyopewa ili kuona iwapo utumishi wake unakidhi mahitaji ya Serikali kuwahudumia watanzania nchi inayojiandaa kuwa nchi ya kipato cha kati.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani amewataka wafanyakazi kuwa na maono katika majukumu yao na kujitathimini kila wakati ili kubaini mafanikio na changamoto na kuzipatia ufumbuzi kwa wakati.

Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano inaundwa na sekta tatu na inasimamia taasisi 29 zenye muelekeo wa ujenzi na usimamizi wa miundombinu na inatarajiwa kuiandaa Tanzania kuwa na miundombinu ya kisasa itakayowezesha kuhimili changamoto za kuwa nchi ya kipato cha kati ifikapo mwaka 2025.

CHANZO: FULLSHANGWE

 &&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&



ZANZIBAR

Maandalizi ya uchaguzi wa marudio zanziba yanaelekea yamekamilika baada ya tume ya Uchaguzi kudhibitisha kupokea shehena ya karatasi zitakazotumika kwa ajili ya kupigia kura katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Machi 20 mwaka huu.

Makaratasi hayo yaliyochapishwa nchini Afrika Kusini yamewasili jana na kupokewa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC huku tume hiyo ikitangaza kuwa maandalizi yote ya uchaguzi huo yamekamilika na kwamba, uchaguzi huo wa marudio utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 4.5.

Karatasi hizo zina picha za wagombea wote 14 wa kiti cha Urais wa Zanzibar licha ya baadhi ya wagombea akiwemo mgombea wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad kutangaza kwamba, hatogombea katika uchaguzi huo wa marudio.

Zanzibar ambayo ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliingia katika mgogoro wa kisiasa mwezi Oktoba mwaka jana baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi visiwani humo Jecha Salim Jecha kufuta matokeo ya uchaguzi kwa kile alichokiita ukiukwaji wa sheria na taratibu wakati wa zoezi la upigaji kura.

Uchaguzi wa marudio Zanzibar unatarajiwa kufanyika march 20 huku vyama tisa kati ya 14 vilivyoshiriki katika uchaguzi uliofutwa wa Oktoba 25, kikiwemo chama cha CUF ambacho kinadai mgombea wake wa urais Maalim Seif Sharif Hamad ndiye mshindi halali wa kiti hicho vikiwa vimeshatangaza rasmi kwamba, havitashiriki katika uchaguzi huo.

CHANZO: IRIBSWAHILI

 &&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&

KIMATAIFA


 DAMASCUS

Marekani imesema makubaliano ya kusitisha mapigano nchini Syria ambayo yamedumu kwa wiki mbili, yameheshimiwa kwa kiasi kikubwa licha ya kuendelea kwa mashambulizi dhidi ya raia kutoka kwa wanajeshi wa serikali ya Syria na upinzani.

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Marekani John Kirby amesema kusitishwa kwa mapigano kumepunguza ghasia na kuruhusu kupelekwa kwa misaada ya kibinadamu katika baadhi ya maeneo yanayozingirwa Syria.

Duru nyingine ya mazungumzo ya kutafuta amani inatarajiwa kuanza Jumatatu ijayo mjini Geneva na itadumu kwa takriban siku kumi.

Mjumbe wa Umoja wa Mataifa kuhusu Syria Stefan di Mistura hapo jana alitangaza chaguzi zitafanyika Syria mwezi Septemba mwaka ujao.

CHANZO: DWSWAHILI

&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepitisha azimio ambalo linataka vikosi vya wanajeshi wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa ambao wanakabiliwa na shutuma za kuhusika katika udhalilishaji kingono kurejeshwa katika nchi zao. 

Hii ndiyo mara ya kwanza kwa Baraza hilo la usalama kuchukua hatua za kuwaadhibu wanajeshi wa umoja huo wanaohusishwa na vitendo vya unyanyasaji wa kingono wakati wanapostahili kuwalinda raia katika maeneo yanayokumbwa na mizozo. 

Azimio hilo lililopitishwa jana litapelekea kikosi kizima cha wanajeshi wa kulinda amani kurejeshwa makwao iwapo baadhi ya wanajeshi wa nchi hiyo wanaohudumu katika ujumbe wa kulinda amani wanashutumiwa. 

Azimio hilo pia linamruhusu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon kuizuia nchi yoyote kutuma wanajeshi wa kulinda amani iwapo itashindwa kuchukua hatua dhidi wanajeshi wake wanaoshutumiwa.


CHANZO:DWSWAHILI

 &&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&


 LONDON

Uingereza imesema inatuma wanajeshi zaidi nchini Iraq kukisaidia kikosi chake kilichoko nchini humo ambacho kinatoa mafunzo kwa jeshi la Iraq ili liweze kupambana dhidi ya wanamgambo wenye itikadi kali wa Dola la Kiislamu.

Waziri wa ulinzi wa Uingereza Michael Fallon amesema wanajeshi thelathini zaidi watatumwa nchini humo kutoa mafunzo ya kiufundi pamoja na ya kimatibabu.

Hatua hiyo inamaanisha kuwa idadi jumla ya wanajeshi wa Uingereza nchini Iraq itakuwa ni 300.

Wanajeshi hao wa ziada watapelekwa katika kambi za kutoa mafunzo zilizoko Bismaya na Taji nje ya mji mkuu wa Iraq, Baghdad.

Fallon amesema hatua kubwa zimepigwa katika vita dhidi ya IS, na sasa ni muda wa kuimarisha mafunzo kwa wanajeshi wa Iraq wanaojitayarisha kuikomboa miji ya Fallujah na Mosul iliyo mikononi mwa wanamgambo hao.

CHANZO: DWSWAHILI                                                                       


NA


 CHICAGO



Mgombe urais kwa tiketi ya chama cha Republican nchini Marekani Donald Trump hapo jana amelazimika kufutilia mbali mkutano wake wa hadhara uliokuwa ufanyike Chicago usiku kutokana na sababu za kiusalama.

Hatua hiyo imechukuliwa baada ya kuzuka vurumai kubwa kati ya wafuasi wa Trump na wanaompinga.

Taarifa kutoka kwa Trump imesema kutokana na kuzingatia usalama wa maelfu ya watu ambao walikuwa wamekusanyika Chicago kwa ajili ya mkutano huo, imembidi aufutilie mbali mkutano huo hadi tarehe nyingine.

Kituo cha Televisheni cha Marekani CNN kimekadiria kulikuwa na watu kati ya 8,500 hadi 10,000 wakati fujo zilipozuka katika ukumbi wa mkutano.

Awali, waandamanaji walitatiza mkutano mwingine wa mgombea huyo wa Urais katika jimbo la Missouri.


CHANZO: DWSWAHILI

Mhariri habari zote-Denis Kazenzele                                                                        




About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / / RUKA NA HIZI HAPA KITAIFA NA KIMATAIFA UFAHAMU MENGI KUTOKA NDANI NA NJE YA TANZANIA..

picha maktaba- sio halisi
DODOMA

Jeshi la polisi Mkoani Dodoma limefanikiwa kukamata silaha 26 aina ya Gobole na mitambo ya kuyatengezea silaha hizo kinyume cha sheria ya umiliki wa siraha.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Dodoma Lazaro Mambosasa amewaambia waandishi wa habari kuwa Magobore 19 yamesalimishwa na wamiliki waliokuwa wakiyamiliki kinyume na sheria baada ya kusikia wito wa Jeshi hilo lililowataka kuzisalimisha.

Mambosasa amesema jeshi hilo pia linawashikilia watu 7 wakazi wa Manda Wilayani Chamwino baada ya kuwakamata na aina hiyo ya silaha 7 pamoja nyundo 1na risasi zilizotengenezwa kienyeji ambazo zinadaiwa zilikuwa zikitumiwa kuwindia wanyama katika pori la Ruaha mkoani iringa.

Aidha kamanda huyo amesema moja ya Gobole lilikuwa limevishwa shanga ambayo ni ishara ya nguvu za Giza ili polisi wasifanikiwe kuikamata ambapo pamoja na hilo wamefanikiwa kukamata pikipiki zenye makosa mbalimba 250 na kuwatoza wamiliki wake jumla ya million 7 na Laki 2 na 30 Elfu.



CHANZO: LYDIA KISHIA/JOHN BANDA


 &&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&
  

MWANZA

Mbunge wa jimbo la Bunda,Ester Bulaya amekamatwa na Jeshi la Polisi  jijini Mwanza na kulazimika  kulala  rumande baada ya kunyimwa dhamana.
Polisi wamevamia Hoteli aliyofikia mbunge huyo na kumkamata majira ya saa 7 usiku na kisha  kumpeleka  kituo cha kati cha Jijini Mwanza akiwa ameambatana na Mhe. Halima Mdee, Joyce Sokombe pamoja na Wakili John Malya.

Wabunge hao pamoja na uongozi wa juu wa Chadema Wako jijini Mwanza 
kwa ajili ya kikao cha Baraza Kuu la chama hicho kinachofanyika leo katika Hotel ya Gold Crest.

Kikao hicho pia kinatarajiwa kumpata katibu mkuu mpya kushika nafasi iliyoachwa wazi na Dokta Wilbroad Slaa aliyejiuzuru mwaka uliopita baada ya kushindwa kuelewana katika baadhi ya maamuzi na uongozi wa chama hicho.



CHANZO: MPEKUZIHURU

&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&




DAR ES SALAAM

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amewataka wafanyakazi wa wizara yake kuacha kufanya kazi kwa mazoea kwani Serikali ya imejipanga kutumia sekta ya miundombinu kukuza na kufungua fursa za kiuchumi.

Akizungumza katika kikao kazi kilichohusisha Sekta za Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Mbarawa amemtaka kila mtu afanye kazi kwa umoja, uwazi na uadilifu ili kufikia lengo la kuanzishwa kwa wizara hiyo na kujihakikishia nafasi ya kuendelea kuwa mtumishi wa umma.

Amesema kila mfanyakazi atapewa malengo na atapimwa kulingana na malengo aliyopewa ili kuona iwapo utumishi wake unakidhi mahitaji ya Serikali kuwahudumia watanzania nchi inayojiandaa kuwa nchi ya kipato cha kati.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani amewataka wafanyakazi kuwa na maono katika majukumu yao na kujitathimini kila wakati ili kubaini mafanikio na changamoto na kuzipatia ufumbuzi kwa wakati.

Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano inaundwa na sekta tatu na inasimamia taasisi 29 zenye muelekeo wa ujenzi na usimamizi wa miundombinu na inatarajiwa kuiandaa Tanzania kuwa na miundombinu ya kisasa itakayowezesha kuhimili changamoto za kuwa nchi ya kipato cha kati ifikapo mwaka 2025.

CHANZO: FULLSHANGWE

 &&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&



ZANZIBAR

Maandalizi ya uchaguzi wa marudio zanziba yanaelekea yamekamilika baada ya tume ya Uchaguzi kudhibitisha kupokea shehena ya karatasi zitakazotumika kwa ajili ya kupigia kura katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Machi 20 mwaka huu.

Makaratasi hayo yaliyochapishwa nchini Afrika Kusini yamewasili jana na kupokewa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC huku tume hiyo ikitangaza kuwa maandalizi yote ya uchaguzi huo yamekamilika na kwamba, uchaguzi huo wa marudio utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 4.5.

Karatasi hizo zina picha za wagombea wote 14 wa kiti cha Urais wa Zanzibar licha ya baadhi ya wagombea akiwemo mgombea wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad kutangaza kwamba, hatogombea katika uchaguzi huo wa marudio.

Zanzibar ambayo ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliingia katika mgogoro wa kisiasa mwezi Oktoba mwaka jana baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi visiwani humo Jecha Salim Jecha kufuta matokeo ya uchaguzi kwa kile alichokiita ukiukwaji wa sheria na taratibu wakati wa zoezi la upigaji kura.

Uchaguzi wa marudio Zanzibar unatarajiwa kufanyika march 20 huku vyama tisa kati ya 14 vilivyoshiriki katika uchaguzi uliofutwa wa Oktoba 25, kikiwemo chama cha CUF ambacho kinadai mgombea wake wa urais Maalim Seif Sharif Hamad ndiye mshindi halali wa kiti hicho vikiwa vimeshatangaza rasmi kwamba, havitashiriki katika uchaguzi huo.

CHANZO: IRIBSWAHILI

 &&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&

KIMATAIFA


 DAMASCUS

Marekani imesema makubaliano ya kusitisha mapigano nchini Syria ambayo yamedumu kwa wiki mbili, yameheshimiwa kwa kiasi kikubwa licha ya kuendelea kwa mashambulizi dhidi ya raia kutoka kwa wanajeshi wa serikali ya Syria na upinzani.

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Marekani John Kirby amesema kusitishwa kwa mapigano kumepunguza ghasia na kuruhusu kupelekwa kwa misaada ya kibinadamu katika baadhi ya maeneo yanayozingirwa Syria.

Duru nyingine ya mazungumzo ya kutafuta amani inatarajiwa kuanza Jumatatu ijayo mjini Geneva na itadumu kwa takriban siku kumi.

Mjumbe wa Umoja wa Mataifa kuhusu Syria Stefan di Mistura hapo jana alitangaza chaguzi zitafanyika Syria mwezi Septemba mwaka ujao.

CHANZO: DWSWAHILI

&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepitisha azimio ambalo linataka vikosi vya wanajeshi wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa ambao wanakabiliwa na shutuma za kuhusika katika udhalilishaji kingono kurejeshwa katika nchi zao. 

Hii ndiyo mara ya kwanza kwa Baraza hilo la usalama kuchukua hatua za kuwaadhibu wanajeshi wa umoja huo wanaohusishwa na vitendo vya unyanyasaji wa kingono wakati wanapostahili kuwalinda raia katika maeneo yanayokumbwa na mizozo. 

Azimio hilo lililopitishwa jana litapelekea kikosi kizima cha wanajeshi wa kulinda amani kurejeshwa makwao iwapo baadhi ya wanajeshi wa nchi hiyo wanaohudumu katika ujumbe wa kulinda amani wanashutumiwa. 

Azimio hilo pia linamruhusu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon kuizuia nchi yoyote kutuma wanajeshi wa kulinda amani iwapo itashindwa kuchukua hatua dhidi wanajeshi wake wanaoshutumiwa.


CHANZO:DWSWAHILI

 &&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&


 LONDON

Uingereza imesema inatuma wanajeshi zaidi nchini Iraq kukisaidia kikosi chake kilichoko nchini humo ambacho kinatoa mafunzo kwa jeshi la Iraq ili liweze kupambana dhidi ya wanamgambo wenye itikadi kali wa Dola la Kiislamu.

Waziri wa ulinzi wa Uingereza Michael Fallon amesema wanajeshi thelathini zaidi watatumwa nchini humo kutoa mafunzo ya kiufundi pamoja na ya kimatibabu.

Hatua hiyo inamaanisha kuwa idadi jumla ya wanajeshi wa Uingereza nchini Iraq itakuwa ni 300.

Wanajeshi hao wa ziada watapelekwa katika kambi za kutoa mafunzo zilizoko Bismaya na Taji nje ya mji mkuu wa Iraq, Baghdad.

Fallon amesema hatua kubwa zimepigwa katika vita dhidi ya IS, na sasa ni muda wa kuimarisha mafunzo kwa wanajeshi wa Iraq wanaojitayarisha kuikomboa miji ya Fallujah na Mosul iliyo mikononi mwa wanamgambo hao.

CHANZO: DWSWAHILI                                                                       


NA


 CHICAGO



Mgombe urais kwa tiketi ya chama cha Republican nchini Marekani Donald Trump hapo jana amelazimika kufutilia mbali mkutano wake wa hadhara uliokuwa ufanyike Chicago usiku kutokana na sababu za kiusalama.

Hatua hiyo imechukuliwa baada ya kuzuka vurumai kubwa kati ya wafuasi wa Trump na wanaompinga.

Taarifa kutoka kwa Trump imesema kutokana na kuzingatia usalama wa maelfu ya watu ambao walikuwa wamekusanyika Chicago kwa ajili ya mkutano huo, imembidi aufutilie mbali mkutano huo hadi tarehe nyingine.

Kituo cha Televisheni cha Marekani CNN kimekadiria kulikuwa na watu kati ya 8,500 hadi 10,000 wakati fujo zilipozuka katika ukumbi wa mkutano.

Awali, waandamanaji walitatiza mkutano mwingine wa mgombea huyo wa Urais katika jimbo la Missouri.


CHANZO: DWSWAHILI

Mhariri habari zote-Denis Kazenzele                                                                        





«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :