Ukiwa
unaingia nchini misri hasa ni kocha au mchezaji na bahatimbaya ukawa unakutana na zamalek na ukafika sehemu moja
ikijulikana kama Petro Sport Stadium –uwanja wao wa kujidai au Cairo
Stadium kwa Al Ahly unauhakika wa
kukutana na
vitimbi vya kutosha ikiwa ni vikwazo vya hapa na pale ili tu kukufanya ushindwe kucheza vema ili tu wakutoe mchezoni maksudi, hii ndio huitwa fitna mchezoni.
vitimbi vya kutosha ikiwa ni vikwazo vya hapa na pale ili tu kukufanya ushindwe kucheza vema ili tu wakutoe mchezoni maksudi, hii ndio huitwa fitna mchezoni.
Nenda pia pale Ismailia Stadium au pale Harras El-Hedoud Stadium
mjini Alexandria, Misri hali ni hiyo hiyo, kwanini kwa sababu
wanahitaji ushindi.
Utasema ni tabia ya wamisri pengine wana tabia mbaya sasa
twende Morocco kutana na Raja Casablanca
katika dimba lao la Stade Mohamed V, ni yale yale neon uzalendo
unalipata huko sio hapa.
&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&
Laikini hapa naomba
nianze kwa kusema ikiwa tunahitaji soka letu kukua na kufikia kuitwa wa kimataifa
ni lazima kujitoa kwa nguvu na roho kwa kuzipa msaada wa hali na mali timu
zetu, hasa zinaposhiriki michuano ya kiataifa lich aya kwamba hata michuano ya
ndani uzalendo ni muhimu.
Uzalendo wa ndani
ni kila mtanzania kujitoa kuisaidia timu yake anayoishabikia kama mwanachama
ili iweze kufanya vema katika michuano ya ndani, lakini linapokuja suala la
michuano ya kimataifa ni lazima sasa kujiweza kizalendo kama taifa na si kama
klabu.
Lakini katika suala
hili wanaopaswa kuonesha uzalendo wakiwa mstari wa mbele ni wenye mamlaka y
aSoka nikimaanisha TFF kwa kuzipa support timu zetu hasa zinazoshiriki michuano
ya kimataifa ili kufanya vema kwani kwa kufanya hivyo kutatoa mianya mingi ya
ajir anje ya nchi kwa wanamichezo wetu.
Lakini sasa
kinachoonekana ni tofauti kabisa kutokana na mienendo ya TFF linapokuja suala
la uzalendo na maamuzi yenye tija kwa taifa wao badala ya kuwa msaada kwa wote
kwa kutenda haki, wao ndio uzalendo unawatoka na kuonekana wakibeba kujitafutia
umaarufu kwa wachache wanaojua kuongea pasipo kujali utaifa una maana gani
kwetu.
Ukiachana na
mashabiki wa Timu za Azam na Yanga kulalamikia ratiba ilivyovurugwa ili
kuifurahisha klabu ya samba iliyokwenda kulalamika kwa shirikisho hilo, lakini
pia hata wataalamu wa soka wameliona tatizo hilo na kuonesha kuingiwa wasiwasi
na maamuzi ya watendaji wa Tff likiwemo shirikisho hilo kwa ujumla wake lakini
pia bodi ya ligi kutokana na ratiba yao ilivyo.
Ndio, naiita ratiba
yao kwa kuwa wanaweza kuibadili muda wowote wanaotaka lakini ukweli ni kwamba
wameshindwa kupanga vema ratiba hiyo kulingana na kalend aya kimataifa, hivi
wanadhani ligi kubwa kama ya England {VPL} kwanini mwezi wa 12 huwa na michezo
mingi mfululizo kwa timu zao au kwanini timu nyingine za ulaya na baadhi za
afrika hakuna mkanganyiko wa ratiba na kuweka viporo? Ni kwa sababu wanaifahamu
ratiba ya mechi za kimatafa.
April 9 Yanga
inacheza na Al Ahly ya Misri hapa Tanzania
katika dimba la taifa la Dar es salaam, lakini ukiangalia jinsi inavyocheza
mechi mfululizo ni aibu, sasa sijui TFF imeamua kuikomoa kwa sababu ya maneno
na ushawishi wa wachache au imekaa ikafikiria kuwa hakuna tatizo katika hilo! Sina
uhakika katika hilo.
Ukichukua michezo
yanga itakayocheza kuanzia kesho March 31 hadi april 9 unakutana na michezo
mitano katika mashingano matatu tofauti ikiwemo Ligi kuu bara, FA pamoja na
Ligi ya mabingwa Afrika, lakini kwa wapinzani wao kwa muda wote huo watakuwa na
mechi moja pekee na hutumia kiwanja kizuri sio kama vya hapa nchini , hili ni
tatizo na kama hatuna uwezo wa kufanya kitu ni vema tukaomba msaada wa
kufanyiwa au kurekebishiwa vitu na si kutumia akili za wachache kupanga mambo
ya wengi tutaumia baadae.
Kocha mkuu wa timu
ya Yanga sc akiongea na gazeti la Champion Jumatano, amesema hivi namnukuu :”umeona
yamefanyika mabadiliko ya mechi za ligi kuu,ndani ya takribani siku 14
tutacheza hadi mechi tano,hasa ukijumlish ana ile ya FA na ile dhidi ya Al Ahly”.”Hata
timu nyingine yoyote ya ulay aisingekuwa na uwezo huo.hapo unatengeneza uchovu
na majeraha”. Tayari lakini hata TFF walipaswa kujua yanga inakwenda kupambana na Al Ahly kwa
ajili ya Taifa, sasa haiwakilishi wanayanga pekee wangetoa nafasi ya ya
maandalizi ya uhakika. Yang asi timu kubwa kama Al Ahly inabanwa kwenye
maandalizi wakati Al Ahly ambao ni wakubwa wamepewa nafasi kubwa wajiandae kwa
nafasi”. Mwisho wa kunukuu.
Mi nadhani Tff
inapaswa kutumia busara kurekebisha ratiba zao ni heri ligi ikasimama kwa muda
kupisha michuano ya kimataifa kama vile inapokuwa ikicheza timu ya taifa mbona
ligi husimama?
Au uzalendo tunapaswa kuonesha huko tu?, mbona katika timu ya
taifa huwa na wachezaji kutoka baadhi ya timu na si timu zote? Basi zile zisizo na
wachezaji katika timu za taifa ziendelee na mechi nyinginezo, lakini
haiwezekani kutokana na kwamba watanzania wote wanapaswa kuifuatilia timu ya
taifa kuishangilia kuiongezea nguvu vivyo hivyo hata vilabu vyetu vinaposhiiki
michuano mikubwa kama hii basi vipewe heshima yao.
Yanga na Azam fc ni
timu zinazowakilisha nchi, hivyo basi ni wajibu wa watanzania kutoa utofauti
wao na ushabiki wa Simba na Yanga na kuziunga mkono Yanga na Azam fc ili
kufanya vema na kuitangaza Tanzania nje ya nchi kwani kwa kufanya hivyo hata
vilabu vingine vitapata nafasi ya kutangazwa kimataifa.
Nategemea siku ya
April 9 Bwana Haji Manara mkuu wa idara y ahabari ya Simba SC na Mkuu wa idara
ya habari ya Young Africa Jeri Muro kukaa hata jukwaa moja wakibadilishana
mawazo ili kupeana mikakati, lakini pia nategemea kumuona Rais wa Shirikisho la
mpira wa miguu Tanzania TFF akiwa pamoja na benchi la ufundi la yanga na sio
kukaa jukwaani kama shabiki au mgeni rasmi hii itasaidia pia kuongeza nguvu,
lakini pia kwa upande wa Azam hivyo hivyo sitegemei kumsikia Rais wa TFF akitoa
majibu ya maswali atakayoulizwa na waandishi wa habari kwa njia ya simu zaidi
nategemea kusikia akiwa na waandishi hao uwanjani na kuelezea mapungufu na
uimara wa Azam Fc kwa utaalamu kutokana
na alichokiona tofauti na hapo nitaamini zaidi kuwa pasipo na kitu cha
kujinufaisha hakuna dalili za uzalendo katika soka letu na kuendelea tuwaachie
wenye kuelewa nini faida ya uzalendo wa kimichezo katiak taifa linalokua kisoka
kama ilivyo kwa Tanzania ya leo.
TFF endekezeni
uzalendo, msisikie masuala ya lawama za umimi na kuharibu ukuta wa nyumba kwa
ajili ya kutengeneza Banda la mifugo.ni hayo kwa leo Asanteni…
No comments
Post a Comment