Ziara hii ya
siku tatu ndiyo kilele cha mazungumzo ya miaka miwili yaliyonuia kurekebisha
uhusiano kati ya Marekani dola kubwa zaidi duniani na jirani yake yenye mfumo
wa kiujamaa.
Punde baada ya
kuwasili Obama ametembea kwenye barabara za mji wa kale wa Havana na pia
kuwahutubia wafanyakazi wa ubalozi mpya wa Marekani.
Kiongozi huyo amesisitiza ziara yake
inatoa nafasi kushauriana na raia wa kisiwa hicho,pia ameahidi kuangazia
masuala ya haki za binadamu, kuwepo mageuzi ya kisiasa japo maafisa wa Cuba
wamesema hakuna ajenda ya kujadili vile nchi hiyo inaweza kukubali vyama vingi
vya kisiasa.
Rais Obama baadae atakutana na Rais wan
chi hiyo Raul Castro.
MWISHO
No comments
Post a Comment