Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » WAZIRI WA HAKI GABON AJIUZULU KUPINGA MATOKEO
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Waziri wa haki nchini Gabon Seraphim Moundounga amejizulu kulalamikia utata ambao umegubika matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika nchini humo wiki moja iliyopita.
Anadaiwa kumuonya Rais Ali Bongo, ambaye alitangazwa mshindi na tume ya uchaguzi, kwamba angefutilia mbali matokeo ya uchaguzi huo iwapo "hayakulingana na uhalisia."
Bw Mondunga ndiye afisa wa juu serikalini kujiuzulu kufuatia mzozo huo kuhusu matokeo ya uchaguzi.
Mamlaka za Gabon zimesema watu watatu wameuawa na zaidi ya 100 kujeruhiwa kwenye ghasia ambapo pia maelfu wamekamatwa.
Baadhi ya taarifa zinasema huenda idadi ya raia waliokufa ikawa juu. Ufaransa imelalamikia hali nchini Gabon na kusema baadhi ya raia wake nchini humo hawajulikani waliko.
Ali Bongo alitangazwa mshindi wa uchaguzi, lakini upinzani ukiongozwa na Jean Ping ulipinga matokeo.
Bw Bongo alipata 49.8% ya kura naye Bw Ping akiwa na 48.2%, tofauti kati yao ikiwa kura 5,594.
Bw Ping alishinda majimbo sita kati ya tisa na ameomba kurudiwa tena kwa shughuli ya hesabu ya kura.
Katika jimbo la Haut-Ogooue, anamotoka Bw Bongo, waliojitokeza kupiga kura walikuwa 99.93% kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa na 95% ya kura zilipigiwa rais huyo

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / WAZIRI WA HAKI GABON AJIUZULU KUPINGA MATOKEO

Waziri wa haki nchini Gabon Seraphim Moundounga amejizulu kulalamikia utata ambao umegubika matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika nchini humo wiki moja iliyopita.
Anadaiwa kumuonya Rais Ali Bongo, ambaye alitangazwa mshindi na tume ya uchaguzi, kwamba angefutilia mbali matokeo ya uchaguzi huo iwapo "hayakulingana na uhalisia."
Bw Mondunga ndiye afisa wa juu serikalini kujiuzulu kufuatia mzozo huo kuhusu matokeo ya uchaguzi.
Mamlaka za Gabon zimesema watu watatu wameuawa na zaidi ya 100 kujeruhiwa kwenye ghasia ambapo pia maelfu wamekamatwa.
Baadhi ya taarifa zinasema huenda idadi ya raia waliokufa ikawa juu. Ufaransa imelalamikia hali nchini Gabon na kusema baadhi ya raia wake nchini humo hawajulikani waliko.
Ali Bongo alitangazwa mshindi wa uchaguzi, lakini upinzani ukiongozwa na Jean Ping ulipinga matokeo.
Bw Bongo alipata 49.8% ya kura naye Bw Ping akiwa na 48.2%, tofauti kati yao ikiwa kura 5,594.
Bw Ping alishinda majimbo sita kati ya tisa na ameomba kurudiwa tena kwa shughuli ya hesabu ya kura.
Katika jimbo la Haut-Ogooue, anamotoka Bw Bongo, waliojitokeza kupiga kura walikuwa 99.93% kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa na 95% ya kura zilipigiwa rais huyo

«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :