Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

Nyani alivuruga mitambo ya umeme katika mji wa Livingstone nchini Zambia na kukata umeme kwa karibu watu 50,000
Nyani huyo alifanikiwa kuingia katika kituo cha umeme siku ya Jumapili, na kuvuruga mitambo yenye umeme inayosambaza umeme kuenda maeneo ya Kusini na magharibi mwa Zambia kwa mujibu wa kampuni ya umeme nchini humo Zesco.
Alisema kuwa wakaazi 28,000 wa Livingstone na watu wengine 22,000 wa eneo hilo walibaki kabisa bila umeme kwa zaidi ya saa sita wakati ukarabati ulikuw ukiendelea.
"Nyani huyo alipigwa na umeme lakini kutokana na maumbile yake ya kimazingira alipata tu majeraha mabaya ya moto. Kama angekuwa binadamu angekufa." alisema Kapata.
Kapata alisema kuwa kampuni hiyo imeomba msamaha wateja wake kwa hasara waliyoipata.
Mji wa Livingstone ni maarugu kwa wanyama pori kama nyani na ndovu wanaotoka mbuga iliyo karibu.
MAZUNGUMZO ya kumaliza mzozo wa mchanga wenye madini (makinikia), baina ya Serikali na Kampuni ya Barrick Gold Corporation kupitia mshirika wake, Acacia, yanaweza kuwa si tu magumu, bali yakachukua muda mrefu kupata suluhisho.

Mazingira hayo yanatokana na uzoefu wa kampuni hiyo katika historia ya kimataifa kuonyesha kwamba inatumia umakini wa hali ya juu kulinda maslahi yake pale panapotokea nafasi ya mazungumzo ya kutafuta suluhisho la jambo lolote linalohusiana na uwekezaji wake katika nchi mbalimbali duniani.

Kwa kutambua changamoto mbalimbali za kiuwekezaji, kampuni hiyo ina bodi maalumu inayohusika na ushauri wa kimataifa ambayo inaundwa na watu wenye ubobezi katika maeneo mbalimbali, hasa ya kisiasa na jiografia.
MTANZANIA Jumamosi limechunguza mwenendo wa kampuni hiyo kuhusu aina ya makubaliano yake ya kiuwekezaji na mataifa mbalimbali na kubaini kuwa imekumbana na misukosuko mikubwa ya uwekezaji wa madini.
Ukiachilia mbali masuala ya makinikia, ambayo kwa sasa yanaipeleka kampuni hiyo kwenye meza moja ya mazungumzo na Serikali, masuala ya mivutano ya ardhi, uchafuzi wa mazingira na migogoro ya mikataba nayo imekuwa ni sehemu ya misukosuko inayoikumba kampuni hiyo katika baadhi ya mataifa ambako imewekeza.
Gazeti hili limebaini kuwa, miongoni mwa mataifa ambayo yanaweza kuchukuliwa kama mfano au Tanzania kujifunza na hata kutafuta mbinu mpya ni Dominica na Saudi Arabia, ambako zilipitia changamoto kama hizi za mikataba mibovu iliyosababisha nchi hizo kunyonywa hadi pale pande zote mbili zilipolazimika kuketi meza moja ya mazungumzo.
Itakumbukwa mapema wiki hii, Rais Dk. John Magufuli baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation, ambaye ni mmiliki mkubwa wa Kampuni ya Acacia Mining Limited, Profesa John Thornton, nchi hizo zilitajwa kwamba zilipita njia kama hii hii inayopitia Tanzania kwa sasa.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili kupitia vyombo vya habari vya kimataifa na  kwenye mtandao wa intaneti umebaini kuwa, hata ule mgogoro wake wa mkataba wa uchimbaji wa madini  na Taifa la Dominica lenye takribani watu milioni 10, mazungumzo ya kutafuta mapatano yalidumu kwa miezi minane.
Inaelezwa kuwa, Serikali ya Dominica iliipa mkataba Kampuni ya Barrick Gold Cooperation wa kuchimba madini kwa miaka 30 katika mgodi wa Pueblo Viejo, ambao ni moja ya migodi mikubwa ya dhahabu duniani.
Katika uwekezaji huo, Kampuni zote mbili ambazo zinatoka nchini Canada, Barrick Gold Cooperation ilimiliki asilimia 60 na Goldcorp asilimia 40.
Msingi wa mgogoro baina ya serikali ya nchi hiyo na Kampuni ya Barrick ni mkataba ambao ulielekeza kuwa nchi hiyo ingenufaika kwa asilimia tatu tu ya faida ya dhahabu inayochimbwa.
Vyombo vya habari nchini Dominica vinaeleza kuwa, vuguvugu la maandamano ya wananchi yasiyokuwa na ukomo ambayo yaliongozwa na asasi mbalimbali za kiraia yaliisukuma serikali ya nchi hiyo kwa kiasi kikubwa kuupitia upya mkataba wake na Kampuni ya Barrick.
Kwa mujibu wa taarifa za vyombo hivyo, baada ya serikali ya nchi hiyo kupitia mkataba upya wa Barrick, iliingia kwenye mazungumzo na kufikia mwafaka wa kulipwa asilimia 28 ya fedha zitokanazo na faida ya dhahabu iliyochimbwa.
Taarifa hizo na zile za Kampuni ya Barrick zinaeleza kuwa; Ongezeko hilo ni sawa na asilimia 25 kutoka malipo yaliyokuwapo kwenye mkataba wa awali uliokuwa unapigiwa kelele na wananchi.
Tangazo la makubaliano hayo baina ya kampuni hiyo na Serikali ya Dominica ambalo lilitolewa na Barrick Mei 8 mwaka 2013, lilitanabahisha kuwa kusudio la makubaliano hayo ni kuwa na uchumi wenye kunufaisha pande zote mbili.
Katika kutafuta makubaliano hayo, Barrick walipendekeza masharti manne ambayo yalijenga msingi wa kupatikana kwa suluhisho.
Masharti hayo, kwanza ni kuondolewa kwa asilimia 10 ya kodi iliyowekwa kwenye mtaji wa awali wa uwekezaji kwa ajili ya kupata faida (NPI).
Pili, kuongezwa kwa muda ambao utaiwezesha serikali ya nchi hiyo kupitia kampuni yake ya Pueblo Viejo Dominicana Corporation (PVDC) kurejesha mtaji wake uliowekezwa.
Tatu, kusogezwa kwa muda wa kuanza makato mapya yatokanayo na faida (NPI).
Nne, kuwekwa punguzo la kiwango cha makato ya thamani.
Taarifa zinaeleza kuwa, baada ya serikali kukubaliana na mapendekezo hayo, Barrick nayo iliridhia mapendezo ya serikali kwa muktadha wa kuanza kulipa  kiwango cha juu cha kodi kilichopendekezwa.
Hata hivyo, ulipaji huo ulianza kufanyika kwa masharti ya kwamba kodi itapandishwa na kushushwa kwa kutegemea bei ya dhahabu kwenye soko.
Pia kiwango cha juu cha makato ya kodi ya dhahabu kitakuwa kinapitiwa na kupangwa upya kila baada ya miaka mitatu kuendana na asilimia 90 ya kodi iliyokuwa inalipwa awali kwenye Kampuni ya Serikali ya PVDC.
Makubaliano hayo yalikadiriwa kuweka usawa wa 50/50 wa mzunguko wa fedha ya madini kati ya Kampuni ya Serikali PVDC na Serikali yenyewe, kati ya mwaka 2013 hadi 2016.
Matokeo yake, Serikali ilitarajia kuvuna zaidi ya dola za Kimarekani bilioni 2.2 katika kipindi ambacho bei ya dhahabu itakuwa inauzwa kwa dola za Kimarekani 1,600 kwa wakia moja (ounce) ambayo ni sawa na gramu 28.3.
Zaidi faida ya kiuchumi ya mabadiliko hayo yalitarajiwa kufika dola za Kimarekani bilioni 1.5.
Kwa ujumla msingi wa makubaliano mambo matatu yaliafikiwa. Kwanza ni kuongezwa kwa kodi ya mapato kwa asilimia 25, pili mrahaba safi wa makinikia kutozwa kwa asilimia 3.2 na tatu, jumla ya faida yote ya madini kutozwa kodi ya asilimia 28.75.
Mgodi wa Pueblo Vienjo una uhai wa miaka 25 na  una madini ya kiwango cha juu na cha chini ambapo kwa mwaka unachangia wastani wa wakia (ounces) 625,000 hadi 675,000 za dhahabu kwa Kampuni ya Barrick.

MKATABA NA SAUDI ARABIA
Taarifa ambazo gazeti hili limezikusanya kutoka katika vyombo vya habari vya Saud Arabia na Kampuni ya Barrick, zinaonyesha kuwa kampuni hiyo mwaka 2014 ililazimika kuingia mkataba wa makubaliano ya uwekezaji wa asilimia 50 kwa 50 na Serikali ya Saudi Arabia kupitia kampuni yake ya madini Ma’aden, kwa ajili ya kuchimba madini ya shaba kwenye mgodi wa Shaba wa Jabal Sayid.
Katika usimamizi au kujua vyote vinavyotoka kwenye uchimbaji huo, mkataba unaipa nafasi Saudi Arabia kusafirisha makinikia ya shaba kwa gharama ya chini.
Kupitia uwekezaji huo, jumla ya pauni milioni 100(kilogramu milioni 45.3) za makinikia ya shaba hupatikana kwa mwaka.
Si hilo tu, mwekezaji huyo mpya atalazimika kufuata misingi yote ya viwango vya maendeleo ya kijamii na kuendeleza kile kinachoitwa ‘Saudization’, yaani kuwaendeleza wazawa katika teknolojia ya uchimbaji madini.

Chini ya makubaliano hayo, pia ni lazima kampuni hiyo iweke asilimia fulani ya nafasi za kazi kwa wananchi wanaozunguka mradi huo na pia kutoa mafunzo maalumu ya utaalamu kwa makampuni ya ndani ya nchi.

Tanzania pia inaweza kuchota uzoefu huu ama kwenda mbali zaidi, hasa wakati ambapo nchi inataka kurekebisha mikataba yake ya madini ambapo inadaiwa nchi inaibiwa sana.

Pamoja na hayo, licha ya kuwa na uzoefu wa changamoto kama hizi katika maeneo inakowekeza,  hata hivyo uamuzi huu wa serikali ya Rais Magufuli umeonekana kuiumiza kichwa Kampuni ya Barrick na Acacia kwa ujumla.
Juzi katika kikao cha wanahisa ambacho kilifanyika kwa njia ya simu, kikiongozwa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Acacia, Brad Gordon, kimetoa mwelekeo wa kutaka kujipanga sawasawa kuanzia kwenye kuunda timu ambayo itakuja kufanya mazungumzo hapa nchini.
Miongoni mwa mikakati yao, Acacia imetaka kupata ripoti ya pili iliyowasilishwa kwa Rais Magufuli mapema wiki hii.
Gordon aliwaambia wanahisa hao kuwa ripoti ya kwanza tayari wamekwishaipata na watahakikisha wanaipata ya pili kabla ya kuanza kwa mazungumzo.
Pamoja na hilo, Acacia wametaka kufahamu mapema timu ambayo itaongozwa na Rais Magufuli katika mazungumzo hayo pamoja na namna mazungumzo yatakavyofanyika.
Katika kikao hicho, Ofisa huyo alikuwa makini kueleza moja kwa moja kama wamekubaliana kutekeleza na kile ambacho kimedaiwa katika ripoti hiyo, ikiwamo suala la ujenzi wa kinu cha uchenjuaji wa dhahabu, akisema kuwa suala hilo wameliacha kwenye mazungumzo pindi majadiliano yatakapoanza.

UCHUNGUZI WA TANZANIA KUHUSU MAKINIKIA
Machi mwaka huu serikali ilizuia makontena zaidi ya 200 kwenye Bandari ya Dar es Salaam kwa ajili ya kuchunguza mchanga wa madini (makinikia) ambao ulikuwa unasafirishwa nje ya nchi kwa ajili ya kuchenjuliwa.
Mchanga huo ulikuwa ni mali ya Kampuni ya Acacia, ambayo ni kampuni mshirika wa Barrick Gold Corporation.
Baada ya zuio la mchanga huo, Rais Dk. John Magufuli aliteua kamati mbili kwa ajili ya kuchunguza makinikia hayo, ambapo kamati ya kwanza iliyokuwa inaundwa na wanasayansi ilibaini kiasi kikubwa cha madini ambayo yangeibiwa kupitia mchanga huo.
Kamati ya pili ya uchunguzi iliundwa na wachumi na wanasheria ambapo ilibaini zaidi ya Sh trilioni 100 zimeibiwa kupitia usafirishaji wa makinikia, huku sheria nyingi za madini zikikutwa na kasoro inayotoa upenyo wa wawekezaji kutorosha madini.
Baada ya ripoti ya pili ya wachumi na wanasheria kuwasilishwa, Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation ambaye ni mmiliki mkubwa wa Kampuni ya Acacia Mining Limited, wakiwa na hisa asilimia 64, Profesa John Thornton, alikuja nchini na kukutana na Rais, Dk. John Magufuli, ambapo walifanya mazungumzo na kukubaliana kuunda timu mbili za majadiliano.
Timu hizo zitahusisha Serikali ya Tanzania na wawakilishi wa Kampuni ya Barrick kutoka Canada na Marekani na watafanya majadiliano ambayo yatahusu namna ya kufikia mwafaka katika suala la kusafirisha mchanga wa dhahabu (makinikia) nje ya nchi kwa faida ya pande zote mbili.
Na EVANS MAGEGE- MTANZANIA


Tukio  la kushangaza lililohusishwa na kifo cha Denis Komba (24) baada ya nyoka aliyekuwa naye kuuawa, limechukua sura mpya baada ya mambo kadhaa kuibuka.

Hayo ni pamoja na familia kudai mzoga wa nyoka na kwenda nao kuuzika nyumbani, jambo lililoendelea kuhusisha suala hilo na imani za kishirikina.

Imeelezwa kuwa familia ilielezwa na mganga wa kienyeji kuwa mwili uliohifadhiwa hospitali, si wa mtoto wao, jambo lililowafanya kuuchukua mzoga wa nyoka na kwenda kuuweka katika mfuko wa sarandusi (kiroba) na kuuzika.

Hata hivyo, mashuhuda walieleza kuwa, familia hiyo ilikikata kichwa cha nyoka na kukizika kivyake na kiwiliwili sehemu nyingine huku mwili wa Komba ambaye naye alizikwa jana, ukizikwa katika kaburi eneo lingine tofauti. Tukio hilo ni la juzi na lilimhusu Komba, mkazi wa Mateka, manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.

Nyumbani kwao ni kilometa tano kutoka katikati ya mji wa Songea. Kabla ya maziko, baadhi ya vijana waliokuwa wamebeba jeneza, walikuwa wakikimbia nalo mwendo wa mchakamchaka huku wakiimba “mkimbize mkimbize nyoka awahi asije kudhuru watu wengine”.

Katika maziko hayo, hakuna ndugu aliyeonekana kulia wala hakukuwa na ibada yoyote wakati jina la marehemu linadhihirisha kuwa ni wa imani ya Kikristo. 

Wakati hayo yakiendelea msibani, baadhi ya watu wake wa karibu walidai alikuwa na tabia ya kucheza na nyoka mara kwa mara.

Hata hivyo, baba mzazi alikana kumuona mwanawe na nyoka. Naye daktari aliyechunguza mwili, alisema kifo cha Komba kinatokana na kugongwa na nyoka mwenye sumu kali, lakini hakuna jeraha wala alama yoyote iliyoonekana katika mwili huo.

Habari zinaeleza kuwa juzi familia ilikwenda kuzungumza na watu wa Idara ya Maliasili, waliochukua mzoga wa nyoka kwa uchunguzi kama nyara ya serikali. Walikubaliana kuwa familia itakwenda kuufukia na ndipo Maliasili walimrudisha nyoka hadi eneo la tukio na familia kumchukua.

Ilielezwa kuwa hatua hiyo, inatokana na madai kuwa kuna mganga amehusisha mzoga wa nyoka huyo na mwili wa Komba.

Watu wa karibu wa familia hiyo, ambao hawakutaka kutaja majina yao wakiwemo mafundi seremala na majirani, walieleza kuwa familia wakiongozwa na baba mzazi Sevelin Komba, walirudi eneo la tukio baada ya kutoka kwa mganga wa kienyeji na kumchukua nyoka na kumpeleka nyumbani.

Habari zinaeleza kuwa familia baada ya tukio hilo, walikwenda kwa mtaalamu wa mambo ya asili (mganga wa kienyeji) ambaye hakufahamika mara moja na kuelezwa kwa nini wamekubali kumuacha mtoto wao akiteseka juani kwani mwili walioupeleka nyumbani kutoka hospitali si wa Denis (Komba).

Aidha familia baada ya kumchukua nyoka huyo eneo la tukio alikouawa, baada ya kufikishwa nyumbani alikatwa kichwa kwa makubaliano ya familia ya marehemu na kiwiliwili kuzikwa tofauti na kichwa katika mfuko wa sarandusi. Baba mzazi alikanusha suala hilo la kwenda kwa mganga.

Katika maziko hayo, hakukuwa na chakula wala matanga na watu wengi walijitokeza ili kushuhudia kitakachoendelea. 

picha na maktaba

DUNIANI kuna mambo, ndivyo unaweza kusema kutokana na mkazi wa Mtaa wa Mateka, Manispaa ya Songea, Denis Komba (26) kufa baada ya nyoka wake aliyekuwa amembeba kwenye mfuko wa jaketi kuuawa na wananchi.

Komba alifariki dunia katika hospitali ya Rufaa Songea mkoa wa Ruvuma (Homso) ambako alilazwa baada ya watu wenye hasira kumuua kwa mawe na fimbo nyoka wake huyo.

Mashuhuda wanaeleza kuwa kabla ya wananchi kumuua nyoka huyo, Komba aliwasihi wasifanye hivyo kwa kuwa wakimuua na yeye angekufa, lakini ombi lake hilo halikusikilizwa.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, siku ya tukio Komba alikodi pikipiki ya Kassian Haule (24) ambaye ni mkazi wa Mpitimbi, yenye namba za usajili MC 724 AKB ili apelekwe nyumbani kwake mtaa wa Mateka.

Akisimulia tukio hilo, alisema alipofika katika eneo la Benki ya Posta ya zamani barabara kuu ya Sokoine, dereva wa pikipiki alihisi kuna kitu kinamtekenya na kumgonga gonga kwa nyuma, ndipo alipogeuka nyuma na kumwona abiria wake amebeba nyoka mkubwa huku amesimamisha kichwa.

Haule alisema, baada ya kumuona nyoka huyo aliruka kutoka kwenye pikipiki na kuanguka pembeni mwa barabara na abiria wake alimwachia yule nyoka ambaye alikimbilia kwenye kalavati la maji.

Aliongeza kuwa ndipo alipopiga kelele za kuomba msaada na kundi la vijana waendesha pikipiki wenzake walifika eneo hilo la tukio kwa lengo la kumsaidia mwenzao juu ya maswahiba yaliyompata hadi kumfanya apige kelele.

Alisema kabla ya vijana hao hawajafanya jambo lolote, Komba aliwaomba vijana hao na watu wengine waliofika katika eneo hilo wasimpige nyoka wake kwani iwapo watampiga na kufa yeye pia atapoteza maisha. Kutokana na maneno hayo, Haule alimtoa nyoka huyo ndani ya kalavati na kwa kushirikiana na vijana wenzake walianza kumpiga nyoka huyo hadi kufa.

Alisema wakati wanampiga nyoka huyo, Komba ambaye ndiye mmiliki wa nyoka huyo naye alianza kulegea kisha akaanguka chini huku akitokwa na mapovu mdomoni na puani.

Habari zinasema kuwa,baada ya Komba kuanguka alikimbizwa hospitali kwa ajili ya kupatiwa matibabu; hata hivyo juhudi za madaktari na wauguzi wa hospitali za kuokoa maisha yake zilishindikana kwani Komba alifariki.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Zuberi Mwombeji, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa mwili wa marehemu haukuwa na jeraha lolote na umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya rufaa Songea.

Alisema nyoka aliyeuawa na wananchi amechukuliwa na idara ya maliasili na uchunguzi zaidi ya tukio hilo unaendelea ili kubaini kiini cha tukio hilo la kuuawa kwa nyoka na kisha mmiliki wake naye kufa. Kamanda Mwombeji alisema, kwa upande wa dereva wa pikipiki yeye anaendelea vizuri na anapatiwa matibabu katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Ruvuma.

Aidha Kamanda Mwombeji, ametoa rai kwa wananchi kuacha mara moja kumiliki nyara za serikali zinazoweza kuwaletea madhara kama vile majeraha au vifo.

Aidha katika tukio lingine, mkazi wa kijiji cha Mdunduwalo Joseph Charles (27) amefariki dunia kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali tumboni na Oddo Komba (34) mkazi wa Mhepai Peramiho baada ya kuhitilafiana wakati wakitoka kunywa pombe.


Kamanda huyo wa polisi alisema, tukio hilo limetokea tarehe 26 mwezi huu saa 1 usiku katika kijiji cha Mtyangimbole kata ya Gumbiro katika halmashauri ya wilaya ya Madaba wilayani Songea ambapo chanzo cha mauaji hayo ni ugomvi uliotokea njiani kati yao wakati wakirudi nyumbani kutoka kwenye klabu za pombe ya kienyeji.

Mwanajeshi aliyenusurika kifo, Roman Valutov.

Roman Valutov akiwa katika pozi.
Bado Urusi ipo kwenye hali ya sintofahamu kufuatia ajali mbaya ya ndege, iliyotokea juzi na kusababisha vifo vya watu 91, wakiwemo wanakwaya wa jeshi wa kikosi cha Red Army Alexandrov, waliokuwa wakielekea Latakia nchini Syria, tayari Rais Vladmir Putin wa Urusi, amevitaka vyombo vinavyohusika kufanya kazi yake na kumpelekea ripoti ya kilichosababisha ajali hiyo.
Wakati abiria wote waliokuwa ndani ya ndege hiyo wakipoteza maisha, ipo simulizi ya kusisimua juu ya mwanajeshi ambaye alipaswa kuwa ndani ya ndege hiyo lakini akazuiwa uwanja wa ndege kusafiri baada ya kubainika kwamba hati yake ya kusafiria ilikuwa ime-expire tangu mwezi wa saba.
Ilikuwaje? Akisimulia mkasa huo huku akitokwa na machozi, mwanajeshi huyo, Roman Valutov, 29, alisema:
“Nilikuwa kwenye orodha ya watu waliopaswa kusafiri na bendi yetu kuelekea nchini Syria. Nilishajiandaa kwa kila kitu lakini tukiwa uwanjani hapo, ilipofika zamu yangu kwenda kukaguliwa, dada aliyekuwa kwenye ofisi ya uhamiaji, alinitazama kwa macho ya mshangao.
“Nikamuuliza kulikoni? Akaniambia ananishangaa kupanga mstari pale wakati najua kwamba hati yangu ya kusafiria ilishaisha muda wake tangu Julai, nikamwambia sikuwa najua. Ilibidi niwekwe pembeni na maafisa wa uwanja huo, wakaanza kujadiliana nini cha kufanya.
“Wakati huo wenzangu waliendelea kukaguliwa na hatimaye wakaelekea kwenye ndege. Nilipouliza kuhusu hatma yangu, niliambiwa ‘huendi popote, paspoti yako imeisha muda wake.’ Nilisikitika sana kwa sababu nilipenda kusafiri na wenzangu lakini sikuwa na ujanja.
“Ilibidi nirudi nyumbani kupumzika. Baadaye nikashangaa simu imeanza kuita mfululizo, watu wengi wakawa wananipigia na kuniuliza kama nipo hai, nikawauliza kumetokea nini? Wakaniambiandege imepata ajali na jina langu lilikuwa miongoni mwa watu waliotangazwa kwamba wamekufa kwenye ajali hiyo, nilipata na mshtuko mkubwa sana. Ndugu zangu nao walikuwa kwenye taharuki, ni tukio la ajabu sana, ahsante Mungu kwamba bado naishi.”

Chanzo:Global Publisher
Jamii inahitaji majukwaa kama ili isikie wananchi!
Nilikemea 2008 kumakatwa yamejirudia. Si sawa
********************************************************************
In case you missed it...
  1. From now on I'll also be making assists via the controller. 👍🏼😉🎮 Happy to be an ambassador!
  2. Mesut Ozil
    • ***********************************************************************************
    1. T 2473 - Variety spice of life ! 6 am testing muscle strength, 1 pm being tested by colleagues, 6 pm the ultimate test with Granddaughter

    Amithab Bachchan

    ******************************************************************************************************************

    So thrilled to be playing at one of the biggest indoor arenas I've ever played at today, in San Juan!
    Maria Sharapova
    ************************************************************************************************************

    Thanks for keeping me on time all these years ☺️👏🏼
    I look forward to another 4 trips around the Sun with you guys!

    Novac Djokovic
     *******************************************************************************************************************
    Nape Nnauye

    *******************************************************************************************************************

    Dhamira ya kufikia uchumi wa viwanda haitofikiwa kama hatutoimarisha miundo mbinu
    ya Barabara na Upatikanaji wa mazao

    Picha Mwalimu Nyerere
    ******************************************************************************************


    There's good news concerning this guy… 🗣 “Danny Welbeck is one week away from being back in full training with the squad.”

    Danny Welbeck





MAKALA

Nyani alivuruga mitambo ya umeme katika mji wa Livingstone nchini Zambia na kukata umeme kwa karibu watu 50,000
Nyani huyo alifanikiwa kuingia katika kituo cha umeme siku ya Jumapili, na kuvuruga mitambo yenye umeme inayosambaza umeme kuenda maeneo ya Kusini na magharibi mwa Zambia kwa mujibu wa kampuni ya umeme nchini humo Zesco.
Alisema kuwa wakaazi 28,000 wa Livingstone na watu wengine 22,000 wa eneo hilo walibaki kabisa bila umeme kwa zaidi ya saa sita wakati ukarabati ulikuw ukiendelea.
"Nyani huyo alipigwa na umeme lakini kutokana na maumbile yake ya kimazingira alipata tu majeraha mabaya ya moto. Kama angekuwa binadamu angekufa." alisema Kapata.
Kapata alisema kuwa kampuni hiyo imeomba msamaha wateja wake kwa hasara waliyoipata.
Mji wa Livingstone ni maarugu kwa wanyama pori kama nyani na ndovu wanaotoka mbuga iliyo karibu.
MAZUNGUMZO ya kumaliza mzozo wa mchanga wenye madini (makinikia), baina ya Serikali na Kampuni ya Barrick Gold Corporation kupitia mshirika wake, Acacia, yanaweza kuwa si tu magumu, bali yakachukua muda mrefu kupata suluhisho.

Mazingira hayo yanatokana na uzoefu wa kampuni hiyo katika historia ya kimataifa kuonyesha kwamba inatumia umakini wa hali ya juu kulinda maslahi yake pale panapotokea nafasi ya mazungumzo ya kutafuta suluhisho la jambo lolote linalohusiana na uwekezaji wake katika nchi mbalimbali duniani.

Kwa kutambua changamoto mbalimbali za kiuwekezaji, kampuni hiyo ina bodi maalumu inayohusika na ushauri wa kimataifa ambayo inaundwa na watu wenye ubobezi katika maeneo mbalimbali, hasa ya kisiasa na jiografia.
MTANZANIA Jumamosi limechunguza mwenendo wa kampuni hiyo kuhusu aina ya makubaliano yake ya kiuwekezaji na mataifa mbalimbali na kubaini kuwa imekumbana na misukosuko mikubwa ya uwekezaji wa madini.
Ukiachilia mbali masuala ya makinikia, ambayo kwa sasa yanaipeleka kampuni hiyo kwenye meza moja ya mazungumzo na Serikali, masuala ya mivutano ya ardhi, uchafuzi wa mazingira na migogoro ya mikataba nayo imekuwa ni sehemu ya misukosuko inayoikumba kampuni hiyo katika baadhi ya mataifa ambako imewekeza.
Gazeti hili limebaini kuwa, miongoni mwa mataifa ambayo yanaweza kuchukuliwa kama mfano au Tanzania kujifunza na hata kutafuta mbinu mpya ni Dominica na Saudi Arabia, ambako zilipitia changamoto kama hizi za mikataba mibovu iliyosababisha nchi hizo kunyonywa hadi pale pande zote mbili zilipolazimika kuketi meza moja ya mazungumzo.
Itakumbukwa mapema wiki hii, Rais Dk. John Magufuli baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation, ambaye ni mmiliki mkubwa wa Kampuni ya Acacia Mining Limited, Profesa John Thornton, nchi hizo zilitajwa kwamba zilipita njia kama hii hii inayopitia Tanzania kwa sasa.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili kupitia vyombo vya habari vya kimataifa na  kwenye mtandao wa intaneti umebaini kuwa, hata ule mgogoro wake wa mkataba wa uchimbaji wa madini  na Taifa la Dominica lenye takribani watu milioni 10, mazungumzo ya kutafuta mapatano yalidumu kwa miezi minane.
Inaelezwa kuwa, Serikali ya Dominica iliipa mkataba Kampuni ya Barrick Gold Cooperation wa kuchimba madini kwa miaka 30 katika mgodi wa Pueblo Viejo, ambao ni moja ya migodi mikubwa ya dhahabu duniani.
Katika uwekezaji huo, Kampuni zote mbili ambazo zinatoka nchini Canada, Barrick Gold Cooperation ilimiliki asilimia 60 na Goldcorp asilimia 40.
Msingi wa mgogoro baina ya serikali ya nchi hiyo na Kampuni ya Barrick ni mkataba ambao ulielekeza kuwa nchi hiyo ingenufaika kwa asilimia tatu tu ya faida ya dhahabu inayochimbwa.
Vyombo vya habari nchini Dominica vinaeleza kuwa, vuguvugu la maandamano ya wananchi yasiyokuwa na ukomo ambayo yaliongozwa na asasi mbalimbali za kiraia yaliisukuma serikali ya nchi hiyo kwa kiasi kikubwa kuupitia upya mkataba wake na Kampuni ya Barrick.
Kwa mujibu wa taarifa za vyombo hivyo, baada ya serikali ya nchi hiyo kupitia mkataba upya wa Barrick, iliingia kwenye mazungumzo na kufikia mwafaka wa kulipwa asilimia 28 ya fedha zitokanazo na faida ya dhahabu iliyochimbwa.
Taarifa hizo na zile za Kampuni ya Barrick zinaeleza kuwa; Ongezeko hilo ni sawa na asilimia 25 kutoka malipo yaliyokuwapo kwenye mkataba wa awali uliokuwa unapigiwa kelele na wananchi.
Tangazo la makubaliano hayo baina ya kampuni hiyo na Serikali ya Dominica ambalo lilitolewa na Barrick Mei 8 mwaka 2013, lilitanabahisha kuwa kusudio la makubaliano hayo ni kuwa na uchumi wenye kunufaisha pande zote mbili.
Katika kutafuta makubaliano hayo, Barrick walipendekeza masharti manne ambayo yalijenga msingi wa kupatikana kwa suluhisho.
Masharti hayo, kwanza ni kuondolewa kwa asilimia 10 ya kodi iliyowekwa kwenye mtaji wa awali wa uwekezaji kwa ajili ya kupata faida (NPI).
Pili, kuongezwa kwa muda ambao utaiwezesha serikali ya nchi hiyo kupitia kampuni yake ya Pueblo Viejo Dominicana Corporation (PVDC) kurejesha mtaji wake uliowekezwa.
Tatu, kusogezwa kwa muda wa kuanza makato mapya yatokanayo na faida (NPI).
Nne, kuwekwa punguzo la kiwango cha makato ya thamani.
Taarifa zinaeleza kuwa, baada ya serikali kukubaliana na mapendekezo hayo, Barrick nayo iliridhia mapendezo ya serikali kwa muktadha wa kuanza kulipa  kiwango cha juu cha kodi kilichopendekezwa.
Hata hivyo, ulipaji huo ulianza kufanyika kwa masharti ya kwamba kodi itapandishwa na kushushwa kwa kutegemea bei ya dhahabu kwenye soko.
Pia kiwango cha juu cha makato ya kodi ya dhahabu kitakuwa kinapitiwa na kupangwa upya kila baada ya miaka mitatu kuendana na asilimia 90 ya kodi iliyokuwa inalipwa awali kwenye Kampuni ya Serikali ya PVDC.
Makubaliano hayo yalikadiriwa kuweka usawa wa 50/50 wa mzunguko wa fedha ya madini kati ya Kampuni ya Serikali PVDC na Serikali yenyewe, kati ya mwaka 2013 hadi 2016.
Matokeo yake, Serikali ilitarajia kuvuna zaidi ya dola za Kimarekani bilioni 2.2 katika kipindi ambacho bei ya dhahabu itakuwa inauzwa kwa dola za Kimarekani 1,600 kwa wakia moja (ounce) ambayo ni sawa na gramu 28.3.
Zaidi faida ya kiuchumi ya mabadiliko hayo yalitarajiwa kufika dola za Kimarekani bilioni 1.5.
Kwa ujumla msingi wa makubaliano mambo matatu yaliafikiwa. Kwanza ni kuongezwa kwa kodi ya mapato kwa asilimia 25, pili mrahaba safi wa makinikia kutozwa kwa asilimia 3.2 na tatu, jumla ya faida yote ya madini kutozwa kodi ya asilimia 28.75.
Mgodi wa Pueblo Vienjo una uhai wa miaka 25 na  una madini ya kiwango cha juu na cha chini ambapo kwa mwaka unachangia wastani wa wakia (ounces) 625,000 hadi 675,000 za dhahabu kwa Kampuni ya Barrick.

MKATABA NA SAUDI ARABIA
Taarifa ambazo gazeti hili limezikusanya kutoka katika vyombo vya habari vya Saud Arabia na Kampuni ya Barrick, zinaonyesha kuwa kampuni hiyo mwaka 2014 ililazimika kuingia mkataba wa makubaliano ya uwekezaji wa asilimia 50 kwa 50 na Serikali ya Saudi Arabia kupitia kampuni yake ya madini Ma’aden, kwa ajili ya kuchimba madini ya shaba kwenye mgodi wa Shaba wa Jabal Sayid.
Katika usimamizi au kujua vyote vinavyotoka kwenye uchimbaji huo, mkataba unaipa nafasi Saudi Arabia kusafirisha makinikia ya shaba kwa gharama ya chini.
Kupitia uwekezaji huo, jumla ya pauni milioni 100(kilogramu milioni 45.3) za makinikia ya shaba hupatikana kwa mwaka.
Si hilo tu, mwekezaji huyo mpya atalazimika kufuata misingi yote ya viwango vya maendeleo ya kijamii na kuendeleza kile kinachoitwa ‘Saudization’, yaani kuwaendeleza wazawa katika teknolojia ya uchimbaji madini.

Chini ya makubaliano hayo, pia ni lazima kampuni hiyo iweke asilimia fulani ya nafasi za kazi kwa wananchi wanaozunguka mradi huo na pia kutoa mafunzo maalumu ya utaalamu kwa makampuni ya ndani ya nchi.

Tanzania pia inaweza kuchota uzoefu huu ama kwenda mbali zaidi, hasa wakati ambapo nchi inataka kurekebisha mikataba yake ya madini ambapo inadaiwa nchi inaibiwa sana.

Pamoja na hayo, licha ya kuwa na uzoefu wa changamoto kama hizi katika maeneo inakowekeza,  hata hivyo uamuzi huu wa serikali ya Rais Magufuli umeonekana kuiumiza kichwa Kampuni ya Barrick na Acacia kwa ujumla.
Juzi katika kikao cha wanahisa ambacho kilifanyika kwa njia ya simu, kikiongozwa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Acacia, Brad Gordon, kimetoa mwelekeo wa kutaka kujipanga sawasawa kuanzia kwenye kuunda timu ambayo itakuja kufanya mazungumzo hapa nchini.
Miongoni mwa mikakati yao, Acacia imetaka kupata ripoti ya pili iliyowasilishwa kwa Rais Magufuli mapema wiki hii.
Gordon aliwaambia wanahisa hao kuwa ripoti ya kwanza tayari wamekwishaipata na watahakikisha wanaipata ya pili kabla ya kuanza kwa mazungumzo.
Pamoja na hilo, Acacia wametaka kufahamu mapema timu ambayo itaongozwa na Rais Magufuli katika mazungumzo hayo pamoja na namna mazungumzo yatakavyofanyika.
Katika kikao hicho, Ofisa huyo alikuwa makini kueleza moja kwa moja kama wamekubaliana kutekeleza na kile ambacho kimedaiwa katika ripoti hiyo, ikiwamo suala la ujenzi wa kinu cha uchenjuaji wa dhahabu, akisema kuwa suala hilo wameliacha kwenye mazungumzo pindi majadiliano yatakapoanza.

UCHUNGUZI WA TANZANIA KUHUSU MAKINIKIA
Machi mwaka huu serikali ilizuia makontena zaidi ya 200 kwenye Bandari ya Dar es Salaam kwa ajili ya kuchunguza mchanga wa madini (makinikia) ambao ulikuwa unasafirishwa nje ya nchi kwa ajili ya kuchenjuliwa.
Mchanga huo ulikuwa ni mali ya Kampuni ya Acacia, ambayo ni kampuni mshirika wa Barrick Gold Corporation.
Baada ya zuio la mchanga huo, Rais Dk. John Magufuli aliteua kamati mbili kwa ajili ya kuchunguza makinikia hayo, ambapo kamati ya kwanza iliyokuwa inaundwa na wanasayansi ilibaini kiasi kikubwa cha madini ambayo yangeibiwa kupitia mchanga huo.
Kamati ya pili ya uchunguzi iliundwa na wachumi na wanasheria ambapo ilibaini zaidi ya Sh trilioni 100 zimeibiwa kupitia usafirishaji wa makinikia, huku sheria nyingi za madini zikikutwa na kasoro inayotoa upenyo wa wawekezaji kutorosha madini.
Baada ya ripoti ya pili ya wachumi na wanasheria kuwasilishwa, Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation ambaye ni mmiliki mkubwa wa Kampuni ya Acacia Mining Limited, wakiwa na hisa asilimia 64, Profesa John Thornton, alikuja nchini na kukutana na Rais, Dk. John Magufuli, ambapo walifanya mazungumzo na kukubaliana kuunda timu mbili za majadiliano.
Timu hizo zitahusisha Serikali ya Tanzania na wawakilishi wa Kampuni ya Barrick kutoka Canada na Marekani na watafanya majadiliano ambayo yatahusu namna ya kufikia mwafaka katika suala la kusafirisha mchanga wa dhahabu (makinikia) nje ya nchi kwa faida ya pande zote mbili.
Na EVANS MAGEGE- MTANZANIA


Tukio  la kushangaza lililohusishwa na kifo cha Denis Komba (24) baada ya nyoka aliyekuwa naye kuuawa, limechukua sura mpya baada ya mambo kadhaa kuibuka.

Hayo ni pamoja na familia kudai mzoga wa nyoka na kwenda nao kuuzika nyumbani, jambo lililoendelea kuhusisha suala hilo na imani za kishirikina.

Imeelezwa kuwa familia ilielezwa na mganga wa kienyeji kuwa mwili uliohifadhiwa hospitali, si wa mtoto wao, jambo lililowafanya kuuchukua mzoga wa nyoka na kwenda kuuweka katika mfuko wa sarandusi (kiroba) na kuuzika.

Hata hivyo, mashuhuda walieleza kuwa, familia hiyo ilikikata kichwa cha nyoka na kukizika kivyake na kiwiliwili sehemu nyingine huku mwili wa Komba ambaye naye alizikwa jana, ukizikwa katika kaburi eneo lingine tofauti. Tukio hilo ni la juzi na lilimhusu Komba, mkazi wa Mateka, manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.

Nyumbani kwao ni kilometa tano kutoka katikati ya mji wa Songea. Kabla ya maziko, baadhi ya vijana waliokuwa wamebeba jeneza, walikuwa wakikimbia nalo mwendo wa mchakamchaka huku wakiimba “mkimbize mkimbize nyoka awahi asije kudhuru watu wengine”.

Katika maziko hayo, hakuna ndugu aliyeonekana kulia wala hakukuwa na ibada yoyote wakati jina la marehemu linadhihirisha kuwa ni wa imani ya Kikristo. 

Wakati hayo yakiendelea msibani, baadhi ya watu wake wa karibu walidai alikuwa na tabia ya kucheza na nyoka mara kwa mara.

Hata hivyo, baba mzazi alikana kumuona mwanawe na nyoka. Naye daktari aliyechunguza mwili, alisema kifo cha Komba kinatokana na kugongwa na nyoka mwenye sumu kali, lakini hakuna jeraha wala alama yoyote iliyoonekana katika mwili huo.

Habari zinaeleza kuwa juzi familia ilikwenda kuzungumza na watu wa Idara ya Maliasili, waliochukua mzoga wa nyoka kwa uchunguzi kama nyara ya serikali. Walikubaliana kuwa familia itakwenda kuufukia na ndipo Maliasili walimrudisha nyoka hadi eneo la tukio na familia kumchukua.

Ilielezwa kuwa hatua hiyo, inatokana na madai kuwa kuna mganga amehusisha mzoga wa nyoka huyo na mwili wa Komba.

Watu wa karibu wa familia hiyo, ambao hawakutaka kutaja majina yao wakiwemo mafundi seremala na majirani, walieleza kuwa familia wakiongozwa na baba mzazi Sevelin Komba, walirudi eneo la tukio baada ya kutoka kwa mganga wa kienyeji na kumchukua nyoka na kumpeleka nyumbani.

Habari zinaeleza kuwa familia baada ya tukio hilo, walikwenda kwa mtaalamu wa mambo ya asili (mganga wa kienyeji) ambaye hakufahamika mara moja na kuelezwa kwa nini wamekubali kumuacha mtoto wao akiteseka juani kwani mwili walioupeleka nyumbani kutoka hospitali si wa Denis (Komba).

Aidha familia baada ya kumchukua nyoka huyo eneo la tukio alikouawa, baada ya kufikishwa nyumbani alikatwa kichwa kwa makubaliano ya familia ya marehemu na kiwiliwili kuzikwa tofauti na kichwa katika mfuko wa sarandusi. Baba mzazi alikanusha suala hilo la kwenda kwa mganga.

Katika maziko hayo, hakukuwa na chakula wala matanga na watu wengi walijitokeza ili kushuhudia kitakachoendelea. 

picha na maktaba

DUNIANI kuna mambo, ndivyo unaweza kusema kutokana na mkazi wa Mtaa wa Mateka, Manispaa ya Songea, Denis Komba (26) kufa baada ya nyoka wake aliyekuwa amembeba kwenye mfuko wa jaketi kuuawa na wananchi.

Komba alifariki dunia katika hospitali ya Rufaa Songea mkoa wa Ruvuma (Homso) ambako alilazwa baada ya watu wenye hasira kumuua kwa mawe na fimbo nyoka wake huyo.

Mashuhuda wanaeleza kuwa kabla ya wananchi kumuua nyoka huyo, Komba aliwasihi wasifanye hivyo kwa kuwa wakimuua na yeye angekufa, lakini ombi lake hilo halikusikilizwa.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, siku ya tukio Komba alikodi pikipiki ya Kassian Haule (24) ambaye ni mkazi wa Mpitimbi, yenye namba za usajili MC 724 AKB ili apelekwe nyumbani kwake mtaa wa Mateka.

Akisimulia tukio hilo, alisema alipofika katika eneo la Benki ya Posta ya zamani barabara kuu ya Sokoine, dereva wa pikipiki alihisi kuna kitu kinamtekenya na kumgonga gonga kwa nyuma, ndipo alipogeuka nyuma na kumwona abiria wake amebeba nyoka mkubwa huku amesimamisha kichwa.

Haule alisema, baada ya kumuona nyoka huyo aliruka kutoka kwenye pikipiki na kuanguka pembeni mwa barabara na abiria wake alimwachia yule nyoka ambaye alikimbilia kwenye kalavati la maji.

Aliongeza kuwa ndipo alipopiga kelele za kuomba msaada na kundi la vijana waendesha pikipiki wenzake walifika eneo hilo la tukio kwa lengo la kumsaidia mwenzao juu ya maswahiba yaliyompata hadi kumfanya apige kelele.

Alisema kabla ya vijana hao hawajafanya jambo lolote, Komba aliwaomba vijana hao na watu wengine waliofika katika eneo hilo wasimpige nyoka wake kwani iwapo watampiga na kufa yeye pia atapoteza maisha. Kutokana na maneno hayo, Haule alimtoa nyoka huyo ndani ya kalavati na kwa kushirikiana na vijana wenzake walianza kumpiga nyoka huyo hadi kufa.

Alisema wakati wanampiga nyoka huyo, Komba ambaye ndiye mmiliki wa nyoka huyo naye alianza kulegea kisha akaanguka chini huku akitokwa na mapovu mdomoni na puani.

Habari zinasema kuwa,baada ya Komba kuanguka alikimbizwa hospitali kwa ajili ya kupatiwa matibabu; hata hivyo juhudi za madaktari na wauguzi wa hospitali za kuokoa maisha yake zilishindikana kwani Komba alifariki.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Zuberi Mwombeji, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa mwili wa marehemu haukuwa na jeraha lolote na umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya rufaa Songea.

Alisema nyoka aliyeuawa na wananchi amechukuliwa na idara ya maliasili na uchunguzi zaidi ya tukio hilo unaendelea ili kubaini kiini cha tukio hilo la kuuawa kwa nyoka na kisha mmiliki wake naye kufa. Kamanda Mwombeji alisema, kwa upande wa dereva wa pikipiki yeye anaendelea vizuri na anapatiwa matibabu katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Ruvuma.

Aidha Kamanda Mwombeji, ametoa rai kwa wananchi kuacha mara moja kumiliki nyara za serikali zinazoweza kuwaletea madhara kama vile majeraha au vifo.

Aidha katika tukio lingine, mkazi wa kijiji cha Mdunduwalo Joseph Charles (27) amefariki dunia kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali tumboni na Oddo Komba (34) mkazi wa Mhepai Peramiho baada ya kuhitilafiana wakati wakitoka kunywa pombe.


Kamanda huyo wa polisi alisema, tukio hilo limetokea tarehe 26 mwezi huu saa 1 usiku katika kijiji cha Mtyangimbole kata ya Gumbiro katika halmashauri ya wilaya ya Madaba wilayani Songea ambapo chanzo cha mauaji hayo ni ugomvi uliotokea njiani kati yao wakati wakirudi nyumbani kutoka kwenye klabu za pombe ya kienyeji.

Mwanajeshi aliyenusurika kifo, Roman Valutov.

Roman Valutov akiwa katika pozi.
Bado Urusi ipo kwenye hali ya sintofahamu kufuatia ajali mbaya ya ndege, iliyotokea juzi na kusababisha vifo vya watu 91, wakiwemo wanakwaya wa jeshi wa kikosi cha Red Army Alexandrov, waliokuwa wakielekea Latakia nchini Syria, tayari Rais Vladmir Putin wa Urusi, amevitaka vyombo vinavyohusika kufanya kazi yake na kumpelekea ripoti ya kilichosababisha ajali hiyo.
Wakati abiria wote waliokuwa ndani ya ndege hiyo wakipoteza maisha, ipo simulizi ya kusisimua juu ya mwanajeshi ambaye alipaswa kuwa ndani ya ndege hiyo lakini akazuiwa uwanja wa ndege kusafiri baada ya kubainika kwamba hati yake ya kusafiria ilikuwa ime-expire tangu mwezi wa saba.
Ilikuwaje? Akisimulia mkasa huo huku akitokwa na machozi, mwanajeshi huyo, Roman Valutov, 29, alisema:
“Nilikuwa kwenye orodha ya watu waliopaswa kusafiri na bendi yetu kuelekea nchini Syria. Nilishajiandaa kwa kila kitu lakini tukiwa uwanjani hapo, ilipofika zamu yangu kwenda kukaguliwa, dada aliyekuwa kwenye ofisi ya uhamiaji, alinitazama kwa macho ya mshangao.
“Nikamuuliza kulikoni? Akaniambia ananishangaa kupanga mstari pale wakati najua kwamba hati yangu ya kusafiria ilishaisha muda wake tangu Julai, nikamwambia sikuwa najua. Ilibidi niwekwe pembeni na maafisa wa uwanja huo, wakaanza kujadiliana nini cha kufanya.
“Wakati huo wenzangu waliendelea kukaguliwa na hatimaye wakaelekea kwenye ndege. Nilipouliza kuhusu hatma yangu, niliambiwa ‘huendi popote, paspoti yako imeisha muda wake.’ Nilisikitika sana kwa sababu nilipenda kusafiri na wenzangu lakini sikuwa na ujanja.
“Ilibidi nirudi nyumbani kupumzika. Baadaye nikashangaa simu imeanza kuita mfululizo, watu wengi wakawa wananipigia na kuniuliza kama nipo hai, nikawauliza kumetokea nini? Wakaniambiandege imepata ajali na jina langu lilikuwa miongoni mwa watu waliotangazwa kwamba wamekufa kwenye ajali hiyo, nilipata na mshtuko mkubwa sana. Ndugu zangu nao walikuwa kwenye taharuki, ni tukio la ajabu sana, ahsante Mungu kwamba bado naishi.”

Chanzo:Global Publisher
Jamii inahitaji majukwaa kama ili isikie wananchi!
Nilikemea 2008 kumakatwa yamejirudia. Si sawa
********************************************************************
In case you missed it...
  1. From now on I'll also be making assists via the controller. 👍🏼😉🎮 Happy to be an ambassador!
  2. Mesut Ozil
    • ***********************************************************************************
    1. T 2473 - Variety spice of life ! 6 am testing muscle strength, 1 pm being tested by colleagues, 6 pm the ultimate test with Granddaughter

    Amithab Bachchan

    ******************************************************************************************************************

    So thrilled to be playing at one of the biggest indoor arenas I've ever played at today, in San Juan!
    Maria Sharapova
    ************************************************************************************************************

    Thanks for keeping me on time all these years ☺️👏🏼
    I look forward to another 4 trips around the Sun with you guys!

    Novac Djokovic
     *******************************************************************************************************************
    Nape Nnauye

    *******************************************************************************************************************

    Dhamira ya kufikia uchumi wa viwanda haitofikiwa kama hatutoimarisha miundo mbinu
    ya Barabara na Upatikanaji wa mazao

    Picha Mwalimu Nyerere
    ******************************************************************************************


    There's good news concerning this guy… 🗣 “Danny Welbeck is one week away from being back in full training with the squad.”

    Danny Welbeck