Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » IKIWA UNAKULA NA KUSAZA KISHA KUMWAGA CHAKULA, UNAFAHAMU KUWA DODOMA KUNA SEHEMU WANACHEMSHA MAWE NA KULA KISAMVU NA MATUNDA? HII HAPA STORI NZIMA
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post




Na Peter Mkwavila,Dodoma.

WAKAZI wa vijiji vya Chunyu na Nghambi wilayani Mpwapwa wamekuwa wakilazimika kuwandangaya watoto wao kwa kuwasha moto asubuhi na kuchemsha mawe kwa kuwaridisha kuwa wanapika chakula kuepuka vilio vya njaa.

Hali ambayo pia imewalazimisha kula matunda ya porini na kisamvu ili kukabiliana na njaa kali iliyopo kwenye  eneo hilo hivyo kumtaka Mbunge wa Jimbo hilo George Lubeleje kuwasaidia kutatua tatizo hilo.

wakazi wa vijiji hivyo walisema wamekuwa wakitumia mbinu hiyo ikiwemo na kutumia matunda ya porini yanayofahamika (Manyakfwega) ili kupunguza njaa waliyonayo.

Mmoja wa wakazi wa kijiji cha Nghambi Peter Mkanwa, alisema kuwa imembidi kwenda porini kusaka matunda hayo ambayo hata hivyo yameanza kuadimika kwa ajili ya kupunguza njaa iliyoikumba familia zilizo nyingi.

Alisema kutokana na tatizo hilo kuwa ni kubwa kwenye eneo hilo la vijiji,akina mama walio wengi wanatumia mbinu za kuchemsha mawe asubuhi kwa kuyafunika kwenye sufuria hivyo wakiona vile wanajua watapata mlo kwa siku hiyo.

“Ndugu mwana habari hapa tuna njaa ya ajabu unavyoniona naelekea porini kutafuta matunda  kwani nyumbani hakuna chakula,ila kama hata una shilingi 500 naomba ninunue unga tukakoroge uji ili tunywe na familia yangu’’Mkanhwa alisema.

Naye Juma Mwanamboka alimtaka Mbunge wa Jimbo hilo kuishirikisha serikali ili iweze kulishughulikia suala hilo kwa umakini kwa kutafuta ufumbuzi wa haraka kwani familia nyingi zimekuwa zikiadhirika.

Mwanamboka alisema kutokana na njaa hiyo hivi sasa pia vijana wengi wa kiume katika vijiji hivyo wamekuwa wakiitumia fursa hiyo pia kuwarubuni watoto wetu wa kike.

Alisema kwa hali hiyo kuna hatari ya kuibuka kwa mimba wasizotarajia ikiwemo na magonjwa ya kuambukizana kama vile maambukizi ya virusi vya ukimwi hivyo serikali iliangalie hili pia.

Naye Salome Chishome mkazi wa kijiji cha Chunyu alisema wamekuwa wakichuma kisamfu kwenye maeneo ya makaburi ambapo hata hivyo pia kimeanza kuadimika ili kukabiliana na tatizo la njaa.

“Hata hivyo tunamshukuru mungu hapa kwenye makaburi yaliyo mengi kuna miti ya mihogo mingi hivyo ndio tunakitumia kama mboga na kama chakula”alisema.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la hilo George Lubeleje,alisema amewaagiza madiwani  kulijadili suala hilo kama hoja ya dharula katika kikao cha baraza la madiwani kitakachokaa hivi karibuni.

Pia alimtaka Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo,Donoti Nhenzi kulishughulikia suala hilo akishirikiana na kamati ya maafa kwa kuhakikisha wanalitatua tatizo hilo kwa kuwapelekea chakula.

Naye Mkuu wa wilaya hiyo,Mohammed Utaly ambaye ndiye Mwenyekiti wa kamati ya maafa ya wilaya alisema suala la ukosefu wa chakula limekuwa ni tatizo kutokana na ukosefu wa mvua msimu uliopita.

Alisema kutokana na mvua za kutosha na pamoja na wananchi hao kupenda kulima zao la mahindi badala ya mtama na muhogo imechangia kwa kiasi kikubwa kuwepo kwa njaa hiyo.

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / IKIWA UNAKULA NA KUSAZA KISHA KUMWAGA CHAKULA, UNAFAHAMU KUWA DODOMA KUNA SEHEMU WANACHEMSHA MAWE NA KULA KISAMVU NA MATUNDA? HII HAPA STORI NZIMA




Na Peter Mkwavila,Dodoma.

WAKAZI wa vijiji vya Chunyu na Nghambi wilayani Mpwapwa wamekuwa wakilazimika kuwandangaya watoto wao kwa kuwasha moto asubuhi na kuchemsha mawe kwa kuwaridisha kuwa wanapika chakula kuepuka vilio vya njaa.

Hali ambayo pia imewalazimisha kula matunda ya porini na kisamvu ili kukabiliana na njaa kali iliyopo kwenye  eneo hilo hivyo kumtaka Mbunge wa Jimbo hilo George Lubeleje kuwasaidia kutatua tatizo hilo.

wakazi wa vijiji hivyo walisema wamekuwa wakitumia mbinu hiyo ikiwemo na kutumia matunda ya porini yanayofahamika (Manyakfwega) ili kupunguza njaa waliyonayo.

Mmoja wa wakazi wa kijiji cha Nghambi Peter Mkanwa, alisema kuwa imembidi kwenda porini kusaka matunda hayo ambayo hata hivyo yameanza kuadimika kwa ajili ya kupunguza njaa iliyoikumba familia zilizo nyingi.

Alisema kutokana na tatizo hilo kuwa ni kubwa kwenye eneo hilo la vijiji,akina mama walio wengi wanatumia mbinu za kuchemsha mawe asubuhi kwa kuyafunika kwenye sufuria hivyo wakiona vile wanajua watapata mlo kwa siku hiyo.

“Ndugu mwana habari hapa tuna njaa ya ajabu unavyoniona naelekea porini kutafuta matunda  kwani nyumbani hakuna chakula,ila kama hata una shilingi 500 naomba ninunue unga tukakoroge uji ili tunywe na familia yangu’’Mkanhwa alisema.

Naye Juma Mwanamboka alimtaka Mbunge wa Jimbo hilo kuishirikisha serikali ili iweze kulishughulikia suala hilo kwa umakini kwa kutafuta ufumbuzi wa haraka kwani familia nyingi zimekuwa zikiadhirika.

Mwanamboka alisema kutokana na njaa hiyo hivi sasa pia vijana wengi wa kiume katika vijiji hivyo wamekuwa wakiitumia fursa hiyo pia kuwarubuni watoto wetu wa kike.

Alisema kwa hali hiyo kuna hatari ya kuibuka kwa mimba wasizotarajia ikiwemo na magonjwa ya kuambukizana kama vile maambukizi ya virusi vya ukimwi hivyo serikali iliangalie hili pia.

Naye Salome Chishome mkazi wa kijiji cha Chunyu alisema wamekuwa wakichuma kisamfu kwenye maeneo ya makaburi ambapo hata hivyo pia kimeanza kuadimika ili kukabiliana na tatizo la njaa.

“Hata hivyo tunamshukuru mungu hapa kwenye makaburi yaliyo mengi kuna miti ya mihogo mingi hivyo ndio tunakitumia kama mboga na kama chakula”alisema.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la hilo George Lubeleje,alisema amewaagiza madiwani  kulijadili suala hilo kama hoja ya dharula katika kikao cha baraza la madiwani kitakachokaa hivi karibuni.

Pia alimtaka Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo,Donoti Nhenzi kulishughulikia suala hilo akishirikiana na kamati ya maafa kwa kuhakikisha wanalitatua tatizo hilo kwa kuwapelekea chakula.

Naye Mkuu wa wilaya hiyo,Mohammed Utaly ambaye ndiye Mwenyekiti wa kamati ya maafa ya wilaya alisema suala la ukosefu wa chakula limekuwa ni tatizo kutokana na ukosefu wa mvua msimu uliopita.

Alisema kutokana na mvua za kutosha na pamoja na wananchi hao kupenda kulima zao la mahindi badala ya mtama na muhogo imechangia kwa kiasi kikubwa kuwepo kwa njaa hiyo.


«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :