Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » KIWANGO CHA UFAULU DARASA LA SABA CHAPANDA DODOMA
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post



NA JOHN BANDA,DODOMA

MKOA wa Dodoma umetangaza majina ya wanafunzi  watakaojiunga na kidato cha kwanza Januari mwakani huku 19,052 wakiwa wamefaulu. 

Akitangaza matokeo hayo jana,Mjini Hapa,Afisa Elimu Mkoa wa Dodoma Juma Kaponda alisema matokeo yanaonesha ufaulu umeongezeka hadi asilimia 54 ambapo mwaka jana ilikuwa asilimia 45.3.

Kaponda alisema wanafunzi waliosajiliwa kufanya mtihani walikuwa 36,273 ambapo wavulana walikuwa 15,745 na wasichana 20,528.

Alisema Halmashauri yenye ongezeko kubwa la ufaulu ni Kondoa yenye asilimia 25 ikifuatiwa na Chemba yenye asilimia 16 huku Chamwino ikishika mkia.

‘’Kwa ujumla mwenendo wa kitaaluma katika halmashauri za kondoa na Chemba zinaleta matumaini makubwa tangu mwaka 2014 ambapo ongezeko la ufaulu katika halmashauri hizo kuwa za kwanza kimkoa.

Kaponda alisema Halmashauri zote hazikufikia malengo ya BRN(Matokeo makubwa sasa) ambapo hali hiyo imefanya Mkoa kubaki katika rangi ya njano.

Pia alisema jumla ya watahiniwa 110 wavulana 45 wasichana 65 sawa na asilimia 0.3 walifanya mtihani bila ya kujua kusoma na kuandika hii ni pungufu na mwaka 2014 ambapo walikuwa 301.

‘’Katika mtihani huu,jumla ya shule 773 zilikuwa na watahiniwa wa mtihani wa darasa la saba idadi ni kati ya shule 757 tulizo nazo katika Mkoa wa Dodoma shule iliyoongoza kwa ongezeko kubwa la alama ni Madaha ya Chemba’’alisema

Alisema katika matokeo hayo somo la English Language ndio wanafunzi walilofanya vibaya zaidi likifuatiwa na Hisabati huku Kiswahili likiongoza kwa ufaulu likifuatiwa na Sayansi.

‘’Ufaulu huu umefanya Mkoa ushike nafasi ya 24 kati ya Mikoa 25,nafasi hii ni mbaya kuliko mwaka jana Halmashauri zilizopanda kinafasi ni Kondoa,Bahi na Chemba’’alisema

Kaponda alisema ufaulu kwa wanafunzi wenye ulemavu umeongezeka kutoka asilimia 75 za mwaka jana mpaka 97 za sasa.


Mhariri mkuu: Denis Kazenzele

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / KIWANGO CHA UFAULU DARASA LA SABA CHAPANDA DODOMA



NA JOHN BANDA,DODOMA

MKOA wa Dodoma umetangaza majina ya wanafunzi  watakaojiunga na kidato cha kwanza Januari mwakani huku 19,052 wakiwa wamefaulu. 

Akitangaza matokeo hayo jana,Mjini Hapa,Afisa Elimu Mkoa wa Dodoma Juma Kaponda alisema matokeo yanaonesha ufaulu umeongezeka hadi asilimia 54 ambapo mwaka jana ilikuwa asilimia 45.3.

Kaponda alisema wanafunzi waliosajiliwa kufanya mtihani walikuwa 36,273 ambapo wavulana walikuwa 15,745 na wasichana 20,528.

Alisema Halmashauri yenye ongezeko kubwa la ufaulu ni Kondoa yenye asilimia 25 ikifuatiwa na Chemba yenye asilimia 16 huku Chamwino ikishika mkia.

‘’Kwa ujumla mwenendo wa kitaaluma katika halmashauri za kondoa na Chemba zinaleta matumaini makubwa tangu mwaka 2014 ambapo ongezeko la ufaulu katika halmashauri hizo kuwa za kwanza kimkoa.

Kaponda alisema Halmashauri zote hazikufikia malengo ya BRN(Matokeo makubwa sasa) ambapo hali hiyo imefanya Mkoa kubaki katika rangi ya njano.

Pia alisema jumla ya watahiniwa 110 wavulana 45 wasichana 65 sawa na asilimia 0.3 walifanya mtihani bila ya kujua kusoma na kuandika hii ni pungufu na mwaka 2014 ambapo walikuwa 301.

‘’Katika mtihani huu,jumla ya shule 773 zilikuwa na watahiniwa wa mtihani wa darasa la saba idadi ni kati ya shule 757 tulizo nazo katika Mkoa wa Dodoma shule iliyoongoza kwa ongezeko kubwa la alama ni Madaha ya Chemba’’alisema

Alisema katika matokeo hayo somo la English Language ndio wanafunzi walilofanya vibaya zaidi likifuatiwa na Hisabati huku Kiswahili likiongoza kwa ufaulu likifuatiwa na Sayansi.

‘’Ufaulu huu umefanya Mkoa ushike nafasi ya 24 kati ya Mikoa 25,nafasi hii ni mbaya kuliko mwaka jana Halmashauri zilizopanda kinafasi ni Kondoa,Bahi na Chemba’’alisema

Kaponda alisema ufaulu kwa wanafunzi wenye ulemavu umeongezeka kutoka asilimia 75 za mwaka jana mpaka 97 za sasa.


Mhariri mkuu: Denis Kazenzele

«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :