Kamati ya uchunguzi ya Urusi imesema leo hii kuwa inachunguza kosa la rubani au la kiufundi kuwa yumkini ndio sababu za kuanguka kwa ndege ya abiria katika eneo la Rostov-on-Don kusini mwa Urusi na kuuwa watu 62 waliokuwemo ndani.
Ndege hiyo ilikuwa ikitokea Dubai.
Halikadhalika Rais wa Urusi Vladimir Putin amesema msaada kwa jamaa wa wale waliouwawa katika ajali ndio jambo litakalopewa kipaumbele kwa sasa.
Shiriki la ndenge hiyo la FlyDubai lenye makaazi yake Dubai limesema kulikuwamo abiria 55 na wahudumu saba ndani ya ndege hiyo ya aina ya Boeing 737 chapa FZ981 na kuongeza kuwa hakuna aliyenusurika.
Taarifa hiyo iliyotolewa katika ukurasa wa kijamii wa Facebook wa shirika hilo, imesema miongoni mwa abiria 44 walikuwa ni raia wa Urusi, wanane raia wa Ukraine, wawili raia wa India na mmoja ni raia wa Uzbekistan.
Kwa mujibu wa taarifa za shirika la habari la serikali la Urusi, ndege hiyo ilianguka na kuwaka moto baada ya jaribio la pili la kutaka kutua katika uwanja wa ndege wa mji huwo.
No comments
Post a Comment