Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » MOURINHO KAIANZA SAFARI KAMA TABIA YAKE ILIVYO
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post


WAKICHEZA huko Vitality Stadium katika Mechi ya kwanza kabisa ya himaya mpya ya Jose Mourinho ya Ligi Kuu England, Manchester United waliitandika Bournemouth Bao 3-1 na kuamsha shangwe za Mashabiki wao kuimba 'Jose Mourinho' mwishoni.

Man United walifunga Bao lao la kwanza Dakika ya 40 baada ya pasi ndefu ya Anders Herrera kuwahi na Beki wa Bournemouth Simon Francis ambae alitoa nyuma kumrudishia Kipa wakeBoruc lakini Juan Mata kuinasa na Kipa Boruc kuokoa na kumgonga tena Simon Francis na kurudi tena kwa Mata aliefunga kilaini.

Bao hilo lilidumu Hadi Haftaimu.

Kipindi cha Pili Dakika ya 59 Kepteni Wayne Rooney akapiga Bao la Pili kwa Kichwa baada ya Krosi ya Valencia kuunganishwa fyongo na Anthony Martial na kumkuta Rooney aliemalizia hadi wavuni.

Bao la 3 la Man United lilipachikwa na Mchezaji Mpya Zlatan Ibrahimovic katika Dakika ya 64 na kuwa Bao lake la kwanza kwa Klabu yake mpya.

Adam Smith aliipa Bournemouth Bao lao pekee Dakika ya 64 na Mechi kwisha Bournemouth 1 Man United 3.

Mwishoni Man United walifanya mabadiliko kwa kumtoa Juan Mata na kumpa Mechi yabkwanza Henrikh Mkhitaryan na kisha akatolewa Anthony Martial na kuongizwa Morgan Schneiderlin nabkufuata Wayne Rooney na kuja Memphis Depay.


-Safari hii Ligi hii haina tena Jina la Mdhamini na itajulikana rasmi kama Ligi Kuu England tofauti na Msimu uliopita ilipoitwa Barclays Premier League kutokana na udhamini wa Barclays.

Mechi inayofuata kwa Man United ni ya Nyumbani kwao Old Trafford Ijumaa ijayo dhidi ya Southampton ikiwa ni Mechi ya Ligi Kuu Englandm
Ligi Kuu England inaendelea baadae Leo kwa mtanange mkali huko Emirates kati ya Arsenal na Liverpool na Jumatatu ipo Mechi 1 kati ya Chelsea na West Ham United huko Stamford Bridge.

VIKOSI:
Bournemouth: Boruc; Francis, Adam Smith, Steve Cook, Daniels; Surman, Arter, Lewis Cook; Ibe, Wilson, King.

Akiba: Federici, Gosling, Ake, Afobe, Gradel, Brad Smith, Grabban.

Manchester United: De Gea; Valencia, Bailly, Blind, Shaw; Fellaini, Ander Herrera; Mata, Rooney, Martial; Ibrahimovic.

Akiba: Romero, Rojo, Memphis, Carrick, Rashford, Mkhitaryan, Schneiderlin.


About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / MOURINHO KAIANZA SAFARI KAMA TABIA YAKE ILIVYO


WAKICHEZA huko Vitality Stadium katika Mechi ya kwanza kabisa ya himaya mpya ya Jose Mourinho ya Ligi Kuu England, Manchester United waliitandika Bournemouth Bao 3-1 na kuamsha shangwe za Mashabiki wao kuimba 'Jose Mourinho' mwishoni.

Man United walifunga Bao lao la kwanza Dakika ya 40 baada ya pasi ndefu ya Anders Herrera kuwahi na Beki wa Bournemouth Simon Francis ambae alitoa nyuma kumrudishia Kipa wakeBoruc lakini Juan Mata kuinasa na Kipa Boruc kuokoa na kumgonga tena Simon Francis na kurudi tena kwa Mata aliefunga kilaini.

Bao hilo lilidumu Hadi Haftaimu.

Kipindi cha Pili Dakika ya 59 Kepteni Wayne Rooney akapiga Bao la Pili kwa Kichwa baada ya Krosi ya Valencia kuunganishwa fyongo na Anthony Martial na kumkuta Rooney aliemalizia hadi wavuni.

Bao la 3 la Man United lilipachikwa na Mchezaji Mpya Zlatan Ibrahimovic katika Dakika ya 64 na kuwa Bao lake la kwanza kwa Klabu yake mpya.

Adam Smith aliipa Bournemouth Bao lao pekee Dakika ya 64 na Mechi kwisha Bournemouth 1 Man United 3.

Mwishoni Man United walifanya mabadiliko kwa kumtoa Juan Mata na kumpa Mechi yabkwanza Henrikh Mkhitaryan na kisha akatolewa Anthony Martial na kuongizwa Morgan Schneiderlin nabkufuata Wayne Rooney na kuja Memphis Depay.


-Safari hii Ligi hii haina tena Jina la Mdhamini na itajulikana rasmi kama Ligi Kuu England tofauti na Msimu uliopita ilipoitwa Barclays Premier League kutokana na udhamini wa Barclays.

Mechi inayofuata kwa Man United ni ya Nyumbani kwao Old Trafford Ijumaa ijayo dhidi ya Southampton ikiwa ni Mechi ya Ligi Kuu Englandm
Ligi Kuu England inaendelea baadae Leo kwa mtanange mkali huko Emirates kati ya Arsenal na Liverpool na Jumatatu ipo Mechi 1 kati ya Chelsea na West Ham United huko Stamford Bridge.

VIKOSI:
Bournemouth: Boruc; Francis, Adam Smith, Steve Cook, Daniels; Surman, Arter, Lewis Cook; Ibe, Wilson, King.

Akiba: Federici, Gosling, Ake, Afobe, Gradel, Brad Smith, Grabban.

Manchester United: De Gea; Valencia, Bailly, Blind, Shaw; Fellaini, Ander Herrera; Mata, Rooney, Martial; Ibrahimovic.

Akiba: Romero, Rojo, Memphis, Carrick, Rashford, Mkhitaryan, Schneiderlin.



«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :