Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» »Unlabelled » MWANAMKE AJITOKEZA KUWANIA URAIS NCHINI RWANDA
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Nchini Rwanda wagombea wa kiti cha urais katika uchaguzi utakaofanyika mwezi wa 8 wanazidi kujitokeza. Diane Rwigara ametangaza rasmi nia yake ya kugombea urais.
Huyu ni Binti wa mfanyabiashara maarufu wa Kinyarwanda Assinapol Rwigara aliyefariki miaka 2 iliyopita katika mazingira ambayo familia yake ilisema ni tatanishi.
Mgombea huyo wa kiti cha urais amesema anataka kukomesha uonevu na kuleta haki na uhuru wa watu kujieleza nchini Rwanda.
Mwanadishi wa BBC Yves Bucyana anasema katika mazungumzo na waandishi wa habari, Bi Diane Rwigara amesema lengo la mkutano huo ni kutangaza rasmi nia yake ya kugombea kiti cha urais katika uchaguzi wa mwezi wa 8 mwaka huu akisema sababu hasa zinazomfanya kupigania kiti hicho.
''Kuna swala la usalama mdogo ambapo baadhi ya watu hutoweka na wengine kuuwawa katika mazingira ya kutatanisha.huwezi kusema kwamba uko katika nchi yenye Amani na usalama wakati watu wanauawa huku wengine wakikimbia nchi," alisema.

Ameongezea kwamba Rwanda hakuna uhuru wa watu kutoa maoni yao na ni tatizo kubwa kwa wakosoaji wa serikali, maswala ambayo yeye anataka kubadilisha:
''Siasa isyobagua kabila au tabaka fulani, ambayo inatoa fursa kwa kila Mnyarwanda na kumpa uhuru wa kutoa maoni yake.Nataka kuondoa dhana kwamba mtu akiwa na msimamo tofauti na serikali basi ataitwa adui wa taifa, hiyo nitaipiga vita katika uongozi wangu," alisema bi Rwigara.
Diane Rwigara mwenye umri wa miaka 35.
Ni binti wa marehemu Assinapol Rwigara, mfanyabiashara alifariki miaka 2 iliyopita kutokana na kile kilichoelezwa na polisi kuwa ajali ya barabarani kauli inayokinzana na ile ya familia yake.


About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / Unlabelled / MWANAMKE AJITOKEZA KUWANIA URAIS NCHINI RWANDA

Nchini Rwanda wagombea wa kiti cha urais katika uchaguzi utakaofanyika mwezi wa 8 wanazidi kujitokeza. Diane Rwigara ametangaza rasmi nia yake ya kugombea urais.
Huyu ni Binti wa mfanyabiashara maarufu wa Kinyarwanda Assinapol Rwigara aliyefariki miaka 2 iliyopita katika mazingira ambayo familia yake ilisema ni tatanishi.
Mgombea huyo wa kiti cha urais amesema anataka kukomesha uonevu na kuleta haki na uhuru wa watu kujieleza nchini Rwanda.
Mwanadishi wa BBC Yves Bucyana anasema katika mazungumzo na waandishi wa habari, Bi Diane Rwigara amesema lengo la mkutano huo ni kutangaza rasmi nia yake ya kugombea kiti cha urais katika uchaguzi wa mwezi wa 8 mwaka huu akisema sababu hasa zinazomfanya kupigania kiti hicho.
''Kuna swala la usalama mdogo ambapo baadhi ya watu hutoweka na wengine kuuwawa katika mazingira ya kutatanisha.huwezi kusema kwamba uko katika nchi yenye Amani na usalama wakati watu wanauawa huku wengine wakikimbia nchi," alisema.

Ameongezea kwamba Rwanda hakuna uhuru wa watu kutoa maoni yao na ni tatizo kubwa kwa wakosoaji wa serikali, maswala ambayo yeye anataka kubadilisha:
''Siasa isyobagua kabila au tabaka fulani, ambayo inatoa fursa kwa kila Mnyarwanda na kumpa uhuru wa kutoa maoni yake.Nataka kuondoa dhana kwamba mtu akiwa na msimamo tofauti na serikali basi ataitwa adui wa taifa, hiyo nitaipiga vita katika uongozi wangu," alisema bi Rwigara.
Diane Rwigara mwenye umri wa miaka 35.
Ni binti wa marehemu Assinapol Rwigara, mfanyabiashara alifariki miaka 2 iliyopita kutokana na kile kilichoelezwa na polisi kuwa ajali ya barabarani kauli inayokinzana na ile ya familia yake.



«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :