Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » JIPU LAKO LIME KAA UPANDE GANI? NATAKA KULITUMBUA
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post



NENO tumbua jipu ni kauli mbiu kama zilivyowahi kuibuka nyingine wakati chaguzi mbalimbali zikiendelea au hata baada ya chaguzi hizo, lakini neon hili limeongezeka zaidi pengine ni kutokana na uelewa wa wananchi wengi juu ya siasa kwa hivi sasa, lakini pia labda ni kutokana na wagombea waliosimama kuwania nafasi ya Urais hasa katika vyama vya CCM na Muungano wa umoja wa katiba ya wananchi {UKAWA}.

Kwa tafsiri sahihi kutoka katika mkusanyiko wa maana mbalimbali neno “JIPU” au furuncles kwa lugha ya wenzetu Ni maambukizi ya kina ya folikuliti au maambukizi ya foilikoli za nywele mara kwa mara unasababishwa na maambukizo ya kibakteria Stafilokokasi aureasi , ambayo husababisha kuvimba kwa eneo chungu lililo juu ya ngozi kutokana na mkusanyiko wa usaha na tishu mfu.

Lakini kwa tafsiri ya sasa unapozungumzia neno “jipu” unazungumzia mtu au kiongozi mwenye mwenendo mbaya katika jamii anayoishi au kuitumikia kama ni kiongozi na neno hili limeibuka mwaka 2015 katika kampeni za aliyekuwa waziri wa ujenzi ambaye kwa sasa ndiye Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr.John Joseph Pombe Magufuli wakati wa kampeni kipindi hicho akipiga pushap shana majukwaan, yote hiyo ilikuwa ni kama sanaa iliyowateka watanzania na kumwamini na kumpatia ridhaa ya kuliongoza taifa hili.

Hadi sasa neno jipu limekuwa na kuonekana wazi kufanya kazi baada ya Mh.Rais yeye mwenyewe kuwatumbua wote walioonekana kubeba jina jipu kwa kuwaondoa katika nafasi zao katika sekta na wizara mbali mbali kwani tumeona TRA,TAKUKURU, Mamlaka ya Bandari na kwingineko, lakini pia wapo viongozi wa chini yake waliofanya kazi hizo wakiwemo Dr Hamis Kigwangala,Mh.Simbachawene,Mh.Seleman Jafo,Paul Makonda na wengineo dhidi ya ubadhilifu wa mali ya umma na kuhusika na kashfa mbalimbali lakini pia usimsahau mzee wa kushtukiza Mh Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa.

Katika kasi hii wengi wanafurahi na kuona kuwa pengine kura zao hazikuharibika kwani walichokihitaji wanakiona sasa kinatekelezeka, lakini kwangu mimi licha ya kuona hayo bado nina swali, “ ikiwa unafurahi kutumbuliwa kwa mtu Fulani kwa kuwa alizuia au alikukosesha haki yako uliyodhani ni yako, wewe vipi unafanya majukumu yako?” jibu si lazima unipe zaidi ya kulitafakari na kubadilika iwapo utagundua jipu hilo unalo maana jipu huwa nalo yeyote Yule ilimradi  ukipat avimelea vya majipu au maambukizi ya kina ya folikuliti kwa hiyo nawe pia unaweza kuwa ni jipu umejichunguza?

Yapo majipu mengi katika jamii kwa mfano nitakupa majipu machache {tabia mbaya kwa wananchi ambapo hutendeka majumbani mwa wengi} kasha ukijipima mtafute daktari wa kukusaidia kutumbua maana wewe huna uwezo wa kujitumbua.

A}wizi – kazi ni kazi kama haina hasara na mikosi!!! Ukikutana na kauli hiyo utaitafsiri kwa njia tofauti, kwani ukimaanisha ilivyo tamkwa utasema hata wizi ni kazi lakini sio sawa kwani wizi ni jipu kutokana na kuwadhulumu haki walio na haki ya kuwa na hicho unachokichukua pasi na ruhusa ya kufanya hivyo, hivyo unaweza kumkuta mtu anamsema Meneja Fulani katumbuliwa jipu na kudai kuwa alishawashinda wakati yeye siku moj aau mbili zilizopita kaiibia ofisi yake au kawaibia watu anaoishi nao kasha anasema ofisa Yule alistahili kutumbuliwa kwani alitutesa na kutusababishia umaskini..wewe pia ni jipu na anayepaswa kukutumbua ni Yule anayekuona.

B}masengenyo- ahahahaha! Binadamu bwana! Kuna tabia mbaya zaidi katika jamii inayowatesa walio wengi, hii ni tabia ya wivu, wivu una hasara yake katika jamii ya wanadamu.

Wivu husababisha umaskini, wivu pia husababisha migongano{migogoro} katika jamii, wivu husababisha kusengenyana, wivu huleta imani za kishirikina, wivu huleta mauaji na matatizo mengine kama hayo na zaidi ya hayo.

Wivu ni jipu kuanzia majumbani kwenda maofisini, katika maeneo ya biashara na kadhalika na palipo na masengenyo daima hakuna maendeleo na pasipokuwepo na maendeleo kwa sababu ya masengenyo hakika hilo nalo ni Jipu na mimi naweza kukuonesha anaepaswa kukutumbua wewe ni jipu.

C}uvivu/uzembe-“kufanya kazi sio kazi na ukiona kazi kufanya kazi basi acha kazi uone ilivyo kazi kupata kazi” Naupenda sana huu msemo lakini pia unanikumbusha kuwa wapo wat wali na kazi ambao wanajihisi kuwa ni muhimu kuliko wengine na endapo wataondoka basi ofisi hiyo itakufa nay eye ana uhakika wa kupata kazi katika ofisi nyingine kutokana na umaarufu au uwezo wake anaojiamini nao, lakini kumbuka ukipoteza kazi usahau kupata kazi maana katika ofisi zote unazodhani kuomba kazi wapo wenye nafasi zao na wanafanya kazi vema, lakini ukiwa mvivu jua wewe unadhoofisha maendeleo ya nchi na jamii yake, wewe ni Jipu na ukiona wewe ni mzembe pia jua unahatarisha kutokufanyika kazi za ofisi au eneo husika au utaharibu sifa ya kazi unayoifanya au kuharibu kabisa sifa ya ofisi hivyo kwanini tusikuite jipu? Wewe ni jipu, hivyo hakuna haja ya kumwita mwenzako jipu angali ukijua pia wewe ni jipu kutokana na uvivu au uzembe wako..kwanini usitumbuliwe?

E}uzinzi”kuna utofauti kati ya uzinzi na uasherati” Lakini sina sababu ya kukuelezea utofauti wake lakini kumbuka tu yote yanahusiana na kushiriki tendo la ndoa nje ya ndoa kama umeoa/kuolewa au kushiriki mapenzi katika wakati ambao hujaruhusiwa kisheria kufanya hivyo. Na kumbuka hiyo ni dhambi hata maandiko matakatifu yanatuambia '' Maana Haya Ndiyo Mapenzi Ya MUNGU, Kutakaswa Kwenu, Mwepukane Na Uasherati- 1 Thesalonike 4:3.'' Tunaamini kuwa hakuna aliye msafi kama pia biblia isemavyo kuwa  1 Kor 5:10-11'' Sisemi msichangamane kabisa na wazinzi wa dunia hii, au na wenye kutamani, au na wanyang'anyi, au na wenye kuabudu sanamu; maana hapo ingewalazimu kutoka katika dunia. Lakini, mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang'anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye.'' Hili nalo ni jipu na hatuna budi kulitumbua ili kupunguza kasi ya umaskini unaosababishwa na magonjwa na vifo vya vijana ambao ni taifa la kesho.

G}ulevi-“unapozungumzia ulevi hatumaanishi pombe pekee, hapa tunazungumzia mambo mbalimbali maana neno ulevi lina maana ya kuwa na matumizi ya kitu Fulani kupit akiasi kinachohitajika, kwa mfano wanaotumia pombe, akinywa alafu asilewe akawa anajitambua haanguzi au hatukani mtu au haongei maneno ya “kipuuzi” bali akiwa na akili zake timamu huyo tunamuita mnywaji sawa na mnywaji wa maji au Sharubati {maji}, lakini wapo walevi wa maji, madawa ya kulevya , ngono,n.k nao hao ni majipu ambayo yanapaswa kutumbuliwa na jamii hapa hatuhitaji nguvu ya serikali bali ya umma.

H}usaliti-kuna watu pasipo kuwa na nyumba ndogo hawana raha, wanajiona sio wanaume waliokamilika, pia wapo wasipokuwa na wanaume nje ya ndoa wanajihisi kuugua ugonjwa unaofanana na maralia au “TB”, hili nalo ni jipu kwani pasipo kujua kuna madhara ya kuwa na wanawake au wanaume wa nje kwani uharibu familia kiuchumi pamoja na kuingiza maradhi katika familia au kwa mpenzi uliyenaye kwani ukiachana na walio katika familia pia wasaliti wapo hata katika hatua ya uchumba au katika mapenzi yasiyo rasmi”Girl friends & Boyfriends” ni hatari kwani baada ya muda kizazi kilichokisiwa kuwa cha baadae hupotelea kusikojulikana na huku nyuma kuacha majonzi.


Sisemi kuwa kila mtu ni jipu lakini kwa kuwa hakuna msafi bali wapo wasio na mawaa mi naamini yapo majipu yaliyozidi na kuwa sumbufu lakini yapo yanayoanza kuiva na yapo yasiyojulikana sasa wanaoyatumbua hao siyo majipu hivyo tuwape orodha ya majipu yanayowahusu lakini ninong’oneze “wapi  jipu lako lime kaa lilipokaa ? nataka kulitumbua”

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / JIPU LAKO LIME KAA UPANDE GANI? NATAKA KULITUMBUA



NENO tumbua jipu ni kauli mbiu kama zilivyowahi kuibuka nyingine wakati chaguzi mbalimbali zikiendelea au hata baada ya chaguzi hizo, lakini neon hili limeongezeka zaidi pengine ni kutokana na uelewa wa wananchi wengi juu ya siasa kwa hivi sasa, lakini pia labda ni kutokana na wagombea waliosimama kuwania nafasi ya Urais hasa katika vyama vya CCM na Muungano wa umoja wa katiba ya wananchi {UKAWA}.

Kwa tafsiri sahihi kutoka katika mkusanyiko wa maana mbalimbali neno “JIPU” au furuncles kwa lugha ya wenzetu Ni maambukizi ya kina ya folikuliti au maambukizi ya foilikoli za nywele mara kwa mara unasababishwa na maambukizo ya kibakteria Stafilokokasi aureasi , ambayo husababisha kuvimba kwa eneo chungu lililo juu ya ngozi kutokana na mkusanyiko wa usaha na tishu mfu.

Lakini kwa tafsiri ya sasa unapozungumzia neno “jipu” unazungumzia mtu au kiongozi mwenye mwenendo mbaya katika jamii anayoishi au kuitumikia kama ni kiongozi na neno hili limeibuka mwaka 2015 katika kampeni za aliyekuwa waziri wa ujenzi ambaye kwa sasa ndiye Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr.John Joseph Pombe Magufuli wakati wa kampeni kipindi hicho akipiga pushap shana majukwaan, yote hiyo ilikuwa ni kama sanaa iliyowateka watanzania na kumwamini na kumpatia ridhaa ya kuliongoza taifa hili.

Hadi sasa neno jipu limekuwa na kuonekana wazi kufanya kazi baada ya Mh.Rais yeye mwenyewe kuwatumbua wote walioonekana kubeba jina jipu kwa kuwaondoa katika nafasi zao katika sekta na wizara mbali mbali kwani tumeona TRA,TAKUKURU, Mamlaka ya Bandari na kwingineko, lakini pia wapo viongozi wa chini yake waliofanya kazi hizo wakiwemo Dr Hamis Kigwangala,Mh.Simbachawene,Mh.Seleman Jafo,Paul Makonda na wengineo dhidi ya ubadhilifu wa mali ya umma na kuhusika na kashfa mbalimbali lakini pia usimsahau mzee wa kushtukiza Mh Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa.

Katika kasi hii wengi wanafurahi na kuona kuwa pengine kura zao hazikuharibika kwani walichokihitaji wanakiona sasa kinatekelezeka, lakini kwangu mimi licha ya kuona hayo bado nina swali, “ ikiwa unafurahi kutumbuliwa kwa mtu Fulani kwa kuwa alizuia au alikukosesha haki yako uliyodhani ni yako, wewe vipi unafanya majukumu yako?” jibu si lazima unipe zaidi ya kulitafakari na kubadilika iwapo utagundua jipu hilo unalo maana jipu huwa nalo yeyote Yule ilimradi  ukipat avimelea vya majipu au maambukizi ya kina ya folikuliti kwa hiyo nawe pia unaweza kuwa ni jipu umejichunguza?

Yapo majipu mengi katika jamii kwa mfano nitakupa majipu machache {tabia mbaya kwa wananchi ambapo hutendeka majumbani mwa wengi} kasha ukijipima mtafute daktari wa kukusaidia kutumbua maana wewe huna uwezo wa kujitumbua.

A}wizi – kazi ni kazi kama haina hasara na mikosi!!! Ukikutana na kauli hiyo utaitafsiri kwa njia tofauti, kwani ukimaanisha ilivyo tamkwa utasema hata wizi ni kazi lakini sio sawa kwani wizi ni jipu kutokana na kuwadhulumu haki walio na haki ya kuwa na hicho unachokichukua pasi na ruhusa ya kufanya hivyo, hivyo unaweza kumkuta mtu anamsema Meneja Fulani katumbuliwa jipu na kudai kuwa alishawashinda wakati yeye siku moj aau mbili zilizopita kaiibia ofisi yake au kawaibia watu anaoishi nao kasha anasema ofisa Yule alistahili kutumbuliwa kwani alitutesa na kutusababishia umaskini..wewe pia ni jipu na anayepaswa kukutumbua ni Yule anayekuona.

B}masengenyo- ahahahaha! Binadamu bwana! Kuna tabia mbaya zaidi katika jamii inayowatesa walio wengi, hii ni tabia ya wivu, wivu una hasara yake katika jamii ya wanadamu.

Wivu husababisha umaskini, wivu pia husababisha migongano{migogoro} katika jamii, wivu husababisha kusengenyana, wivu huleta imani za kishirikina, wivu huleta mauaji na matatizo mengine kama hayo na zaidi ya hayo.

Wivu ni jipu kuanzia majumbani kwenda maofisini, katika maeneo ya biashara na kadhalika na palipo na masengenyo daima hakuna maendeleo na pasipokuwepo na maendeleo kwa sababu ya masengenyo hakika hilo nalo ni Jipu na mimi naweza kukuonesha anaepaswa kukutumbua wewe ni jipu.

C}uvivu/uzembe-“kufanya kazi sio kazi na ukiona kazi kufanya kazi basi acha kazi uone ilivyo kazi kupata kazi” Naupenda sana huu msemo lakini pia unanikumbusha kuwa wapo wat wali na kazi ambao wanajihisi kuwa ni muhimu kuliko wengine na endapo wataondoka basi ofisi hiyo itakufa nay eye ana uhakika wa kupata kazi katika ofisi nyingine kutokana na umaarufu au uwezo wake anaojiamini nao, lakini kumbuka ukipoteza kazi usahau kupata kazi maana katika ofisi zote unazodhani kuomba kazi wapo wenye nafasi zao na wanafanya kazi vema, lakini ukiwa mvivu jua wewe unadhoofisha maendeleo ya nchi na jamii yake, wewe ni Jipu na ukiona wewe ni mzembe pia jua unahatarisha kutokufanyika kazi za ofisi au eneo husika au utaharibu sifa ya kazi unayoifanya au kuharibu kabisa sifa ya ofisi hivyo kwanini tusikuite jipu? Wewe ni jipu, hivyo hakuna haja ya kumwita mwenzako jipu angali ukijua pia wewe ni jipu kutokana na uvivu au uzembe wako..kwanini usitumbuliwe?

E}uzinzi”kuna utofauti kati ya uzinzi na uasherati” Lakini sina sababu ya kukuelezea utofauti wake lakini kumbuka tu yote yanahusiana na kushiriki tendo la ndoa nje ya ndoa kama umeoa/kuolewa au kushiriki mapenzi katika wakati ambao hujaruhusiwa kisheria kufanya hivyo. Na kumbuka hiyo ni dhambi hata maandiko matakatifu yanatuambia '' Maana Haya Ndiyo Mapenzi Ya MUNGU, Kutakaswa Kwenu, Mwepukane Na Uasherati- 1 Thesalonike 4:3.'' Tunaamini kuwa hakuna aliye msafi kama pia biblia isemavyo kuwa  1 Kor 5:10-11'' Sisemi msichangamane kabisa na wazinzi wa dunia hii, au na wenye kutamani, au na wanyang'anyi, au na wenye kuabudu sanamu; maana hapo ingewalazimu kutoka katika dunia. Lakini, mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang'anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye.'' Hili nalo ni jipu na hatuna budi kulitumbua ili kupunguza kasi ya umaskini unaosababishwa na magonjwa na vifo vya vijana ambao ni taifa la kesho.

G}ulevi-“unapozungumzia ulevi hatumaanishi pombe pekee, hapa tunazungumzia mambo mbalimbali maana neno ulevi lina maana ya kuwa na matumizi ya kitu Fulani kupit akiasi kinachohitajika, kwa mfano wanaotumia pombe, akinywa alafu asilewe akawa anajitambua haanguzi au hatukani mtu au haongei maneno ya “kipuuzi” bali akiwa na akili zake timamu huyo tunamuita mnywaji sawa na mnywaji wa maji au Sharubati {maji}, lakini wapo walevi wa maji, madawa ya kulevya , ngono,n.k nao hao ni majipu ambayo yanapaswa kutumbuliwa na jamii hapa hatuhitaji nguvu ya serikali bali ya umma.

H}usaliti-kuna watu pasipo kuwa na nyumba ndogo hawana raha, wanajiona sio wanaume waliokamilika, pia wapo wasipokuwa na wanaume nje ya ndoa wanajihisi kuugua ugonjwa unaofanana na maralia au “TB”, hili nalo ni jipu kwani pasipo kujua kuna madhara ya kuwa na wanawake au wanaume wa nje kwani uharibu familia kiuchumi pamoja na kuingiza maradhi katika familia au kwa mpenzi uliyenaye kwani ukiachana na walio katika familia pia wasaliti wapo hata katika hatua ya uchumba au katika mapenzi yasiyo rasmi”Girl friends & Boyfriends” ni hatari kwani baada ya muda kizazi kilichokisiwa kuwa cha baadae hupotelea kusikojulikana na huku nyuma kuacha majonzi.


Sisemi kuwa kila mtu ni jipu lakini kwa kuwa hakuna msafi bali wapo wasio na mawaa mi naamini yapo majipu yaliyozidi na kuwa sumbufu lakini yapo yanayoanza kuiva na yapo yasiyojulikana sasa wanaoyatumbua hao siyo majipu hivyo tuwape orodha ya majipu yanayowahusu lakini ninong’oneze “wapi  jipu lako lime kaa lilipokaa ? nataka kulitumbua”

«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :