Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » KUHUSU WAKRISTO WENGI WALIOUWAWA HUKO PAKISTANI SIKU YA PASAKA, WAZIRI MKUU AMEIBUKA NA KAULI HII
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post


Waziri Mkuu wa Pakistan Nawaz Sharif ametoa wito kwa kuwepo ushirikiano zaidi kati ya idara za usalama nchini humo ili kukabiliana na ugaidi.

Amesema hayo siku moja baada ya watu zaidi ya 70 kuuawa kwenye shambulio la bomu katika mji wa Lahore. Kiongozi huyo ameahidi kuwaangamiza magaidi hao.

Bw Sharif, aliyekutana na viongozi wa idara za usalama, amesema taifa hilo litaimarisha juhudi za kukabiliana na ugaidi.

Watu kadha wamekamatwa na silaha kupatikana kwenye operesheni iliyofanywa na vikosi vya usalama, jeshi limesema.

Kundi la Jamaat-ul-Ahrar lililotokana na kundi la Taliban limekiri kutekeleza shambulio hilo.

Watu 300 walijeruhiwa na maafisa wa serikali wamesema idadi ya waliofariki inatarajiwa kupanda.
Eneo hilo lilikuwa na watu wengi kuliko kawaida, kwani Wakristo walikuwa wamekusanyika katika bustani kusherehekea Pasaka.

Hata hivyo, wengi wa waliofariki walikuwa Waislamu.
Mmoja wa waliofariki, mvulana Mkristo Sahil Pervez, alizikwa Jumatatu.

Bw Sharif alitembelea majeruhi hospitalini.


Baadaye katika mkutano na maafisa wa usalama, alisema ni jambo la umuhimu mkubwa kuwashinda magaidi.

“Azma yetu kama taifa na serikali inaendelea kuwa thabiti na adui huyu mwenye uoga anajaribu kushambulia watu wasio na silaha,” amesema.

Aliapa kuwa serikali yake itawaangamiza magaidi hao walioua “wanangu”.

Kiongozi wa kanisa Katoliki duniani Papa Francis kwa upande wake ametoa wito kwa serikali ya Pakistan kulinda makundi ya kidini ya wachache nchini humo.

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / KUHUSU WAKRISTO WENGI WALIOUWAWA HUKO PAKISTANI SIKU YA PASAKA, WAZIRI MKUU AMEIBUKA NA KAULI HII


Waziri Mkuu wa Pakistan Nawaz Sharif ametoa wito kwa kuwepo ushirikiano zaidi kati ya idara za usalama nchini humo ili kukabiliana na ugaidi.

Amesema hayo siku moja baada ya watu zaidi ya 70 kuuawa kwenye shambulio la bomu katika mji wa Lahore. Kiongozi huyo ameahidi kuwaangamiza magaidi hao.

Bw Sharif, aliyekutana na viongozi wa idara za usalama, amesema taifa hilo litaimarisha juhudi za kukabiliana na ugaidi.

Watu kadha wamekamatwa na silaha kupatikana kwenye operesheni iliyofanywa na vikosi vya usalama, jeshi limesema.

Kundi la Jamaat-ul-Ahrar lililotokana na kundi la Taliban limekiri kutekeleza shambulio hilo.

Watu 300 walijeruhiwa na maafisa wa serikali wamesema idadi ya waliofariki inatarajiwa kupanda.
Eneo hilo lilikuwa na watu wengi kuliko kawaida, kwani Wakristo walikuwa wamekusanyika katika bustani kusherehekea Pasaka.

Hata hivyo, wengi wa waliofariki walikuwa Waislamu.
Mmoja wa waliofariki, mvulana Mkristo Sahil Pervez, alizikwa Jumatatu.

Bw Sharif alitembelea majeruhi hospitalini.


Baadaye katika mkutano na maafisa wa usalama, alisema ni jambo la umuhimu mkubwa kuwashinda magaidi.

“Azma yetu kama taifa na serikali inaendelea kuwa thabiti na adui huyu mwenye uoga anajaribu kushambulia watu wasio na silaha,” amesema.

Aliapa kuwa serikali yake itawaangamiza magaidi hao walioua “wanangu”.

Kiongozi wa kanisa Katoliki duniani Papa Francis kwa upande wake ametoa wito kwa serikali ya Pakistan kulinda makundi ya kidini ya wachache nchini humo.

«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :