Na Peter Mkwavila, DODOMA.
MWANAFUNZI aliyetarajiwa kuanza kidato cha kwanza shule ya sekondari ya Ilindi wilayani Bahi mkoa wa Dodoma Joisi Samweli, aliyepewa ujauzito na mwalimu wake Adeodatus Rutajama wa shule ya msingi Ilindi ameiomba serikali aendelea na masomo kwa kuwa alichanguliwa kuigia kidato cha kwanza..
Rai hiyo ameitoa walati alipokuwa akitoa ushuhuda wake mbele ya mkuu wa wilaya ya Dodoma kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia yaliyoandaliwa na jeshi la polisi,mkuki na Afnet yaliyofanyika jana Dodoma.
Akisimulia mbele ya mkuu na wananchi kwenye maadhimisho hayo mwanafunzi huyo alisema kuwa anaiomba serikali kurudi shuleni kwa kuwa katika matokeo yake ya darasa la saba ya 2015 alikuwa amefauli na kuchanguliwa kuingia kidato cha kwanza shule ya kata ya Mndemu.
Joisi akisimua kwenye uzinduzi huo alisema kuwa mwalimu huyo alimtendea ukatili huo chumbani kwake anakuishi mwalimu huyo kijijini Ilindi baada ya kumwita na kumwingiza chumbani na kumvua sketi yake kisha akamwingilia kimwili.
“Mwalimu Rutajama alimwangiza mwanafunzi mwezangu niliyekuwa ninasomanaye kuwa ninaitwa nyumbani kwake,na nipofika sembuleni kwake alinivutia chumbani kwake na kunilaza kitandani na kunivua sketi na kuanza kuningilia kimwili”alisema.
Alisema pamoja na kitendo hicho alichofanyiwa cha ukatili cha kuachishwa masomo yake ya kuendelea kidato cha kwanza na kuzalishwa mtoto ninaiomba serikali inifikirie kwa suala la kurudi ili aendelea na masomo yake na ndoto yake aliyekuwanayo iweze kutimia.
Kwa upande wa baba wa aliyekuwa mwanafunzi huyo Ayubu Mdachi mkazi wa kijiji hicho cha Ilindi,ameiomba serikali kufuatilia kwa makini haki ya mtoto wake ambayo inayoonekana kukubikwa na harufu ya rushwa kutoka kwa mwalimu huyo.
Mdachi alisema kuwa mwalimu huyo amefikia hatua ya kumkana mtoto huyo,hivyo ninaiomba serikali ikiwezekana ifanyike vipimo ambavyo vitakavyoweka wazi kama mtoto huyo aliyezaliwa ni damu yake.
“Toka kesi hii ya kufuatilia haki ya mwanangu nimengudua kuwa kuna harufu ya rushwa kutokana na waliopewa dhamana ya kumfuatilia kutaka kumnyima haki mwanangu,hivyo ninakuomba kamanda wa polisi,watetezi wa haki na mkuu wa wilaya kwa niaba ya serikali kuifuatilia kwa ukaribu sula hili”alisema.
Naye Mkuu wa wilaya ya Dodoma Christina Mndeme alisema kuwa kwa upande wake atahakikisha suala hilo analifuatilia kwa ukaribu na umakini ili haki ya mwanafunzi huyo iweze kufanikisha na hata mwalimu aliyefanya kitendo hicho hatua za kisheria zichukuliwe kwake.
“Ninakuomba mwanangu Joisi na baba wa mtoto ofisi yangu ipo wazi kwa suala hili,wakati wowote njoo na mimi ninakusibitishia nitalivalia njunga hadi huyo mwalimu aliyekuzimisha ndoto yako na yeye achukuliwe hatua za kisheria”alisema.
Wakati huo huo Mkurungezi mkuu wa shirika la Afnet Tanzania Sarah Mwaga amesema kuwa mkoa wa Dodoma unaongoza kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia vya vipigo vya wanawake kata ya mikoa mitano ya Tanzania.
Aidha alisema kuwa kwa vitendo vya ukeketaji ikishika nafasi ya pili kitaifa na ndoa za utotoni mkoa huo wa Dodoma ukiwa wa 4 kwa asilimia 51 hii ni pamoja na matukio ya ubakaji,ulawiti na adhabu zilizo kubwa kupita kiasi kwa watoto.
MWISHO.

No comments
Post a Comment