Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos



Ayman Safadi alisema alimuambia waziri wa mashauri wa nchi za kigeni wa Marekani Rex Tillerson kuwa hatua kama hiyo inaweza kuzua ghadhabu kubwa kwa nchi za kiarabu na ulimwengu wa kiisalmu.

Kuna uvumi kuwa Rais Donald Trump atatangaza hilo hivi karibuni na kutimiza ahadi yake aliyotoa wakati wa kampeni.

Jared Kushner, mkwe wa Trump alisema kuwa bado hakuna uamuzi uliofanywa.

Katika mtandao wa Twitter, Bw Safadi alisema: #Nilizungumza na waziri Rex Tillerson kuhusu hatari ya kuutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel. 

Hatua kama hiyo inaweza kusababisha ghadhabu kwenye nchi za kiarabu na kwa ulimwengi wa kiislamu na kuzua misukosuko na pia kuhujumu jitihada za amani."
 
Hakuna jibu lolote kutoka kwa wizara ya mashauri ya nchi za kigeni nchini Marekani.
Naye rais wa Palestina Mahmoud Abbas anajaribu kupata uungwaji mkono wa kimataifa katika kumshawishi Trump asifanye tangazo kama hilo.

Ofisi yake ilisema kwa aliwapigia simu Jumapili viongozi wa dunia wakiwemo rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan.

"Alitaka kulezea harari za uamuzi wowote wa kuhamisha ubalozo wa Marekani kwenda Jerusalem au kuutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Isael," mshauri wa Bw. Abbas, Majdi al-Khalidi aliliambia shirika la AFP.

Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni nchini Jardan ameonya Marekani kuhusu hatari ya kuutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel.

Korea Kaskazini imesema Rais Donald Trump wa Marekani na serikali yake "wanabembeleza vitokee vita vya nyuklia" huku Washington na muitifaki wake katika Peninsula ya Korea, yaani Korea Kusini zikijiandaa kufanya manuva makubwa ya kijeshi ya angani.

Wizara ya Mambo ya Nje ya Korea Kaskazini imeeleza katika taarifa iliyotoa hapo jana kuwa Trump anaanzisha mchezo hatari wa kamari ya nyuklia katika Peninsula ya Korea na kumwita rais huyo wa Marekani 'jini mbaya wa nyuklia' na 'mvurugaji amani ya dunia'.


Taarifa hiyo ya wizara ya mambo ya nje ya Korea Kaskazini imetolewa katika hali ambayo Marekani na Korea Kusini zinajiandaa kwa mazoezi ya kijeshi yaliyopewa jina la Vigilant Ace yaliyopangwa kuanza Jumatatu ya kesho. Askari wapatao 12,000 wa jeshi la Marekani na ndege za kivita 230 wanatazamiwa kushiriki kwenye manuva hayo.


Hayo yanajiri huku kauli za vitisho zinazotolewa na Marekani dhidi ya Korea Kaskazini zikikabiliwa na ukosoaji mkali.


Baada ya Korea Kaskazini kulifanyia majaribio kombora lake la balistiki la masafa marefu zaidi, mapema wiki hii balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa Nikki Haley aliionya serikali ya Pyongyang kuwa nchi hiyo inaweza "kuangamizwa kikamilifu" endapo vita vitatokea kati yake na Washington.


Hata hivyo matamshi hayo ya Haley yalikosolewa vikali na Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia Sergei Lavrov, ambaye siku ya Ijumaa alisema: "kama kuna mtu aliyedhamiria kikweli kutumia nguvu, kama alivyoeleza mwakilishi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa ili kuiangamiza Korea Kaskazini.. nadhani atakuwa anachezea moto na kufanya kosa kubwa".


Korea Kaskazini inakabiliwa na vikwazo mbalimbali vya kimataifa vya kuishinikiza isimamishe mipango yake ya nyuklia na makombora. Hata hivyo imepuuza mashinikizo yote yanayotolewa dhidi yake huku ikiapa kuwa haitoachana na mipango yake ya nyuklia na makombora kutokana na vitisho na uadui wa Marekani dhidi ya nchi hiyo.


Imebainika kuwa, baadhi ya raia wa Kiafrika wanaopigwa mnada katika magendo ya binadamu nchini Libya wananyofolewa viungo vyao vya mwili na kuuzwa.

Wakili na mwanaharakati mashuhuri Bobby Banson amenukuliwa na tovuti ya habari ya GhanaWeb akisema kuwa, binafsi ameshuhudia kanda ya video inayoonyesha mmoja wa 'watumwa' hao akieleza jinsi viungo vya mwili vya mwenzake vilivyong'olewa na kuuzwa.


Amebainisha kuwa: "Ukweli wa mambo ni kuwa, baadhi ya raia hao wa Afrika hawauzwi kwa ajili ya kwenda kufanya kazi Ulaya, bali kwa ajili ya biashara ya viungo vya binadamu kama maini na mapafu."


Wakili huyo na mtetezi wa haki za binadamu ameongeza kuwa, wahajiri hao waliojikuta kwenye mtego wa magendo ya binadamu wanapewa dawa za kulala na kisha viungo vyao vinachukuliwa."
Wahajiri wa Afrika wanaouzwa kama bidhaa nchini Libya


Hivi karibuni, televisheni ya CNN ilirusha hewani mubashara mnada wa kuuza Waafrika huko nchini Libya ambapo kila mtu alikuwa akiuzwa kwa dola zisizopungua 400 za Kimarekani.
Duru mbali mbali za kimataifa, ukiwemo Umoja wa Afrika na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa zimekosoa vikali biashara hiyo ya utumwa mambo leo inayofanyika nchini Libya.



Wafungwa kumi na tisa, wengi wao wanaokabiliwa na mashtaka ya ubakaji, wametoroka jela mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo usiku wa kuamkia leo, na kusababisha hofu ya kulipiza kisasi kwa waathirika wa vitendo vyao, vyanzo vya serikali za ndani vimesema.



Kwa mujibu wa msimamizi wa gereza Gerard Nkwana, katika jimbo la Kivu Kusini Wafungwa hao 19 walitoroka katika gereza la Kalehe lenye wafungwa 20.


Pascal Nabulera, mkuu wa shirika la kijamii jamii la Kalehe, ametangazia RFI kuwa Watu wanaofika mahakamani kufungua kesi na mashahidi sasa wanawasiwasi wa kulipiziwa kisasi na wafungwa hao waliotoroka.



Nchi ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo yenye umasikini na inayopambana na mgawanyiko wa kisiasa na kikabila pamoja na machafuko mashariki mwa nchi inakabiliwa na matatizo makubwa katika mfumo wake wa mahakama.



Mnamo Mei, wafungwa 4,000 walitoroka katika gereza la Makala huko Kinshasa, mji mkuu, wakati 900 wakitoroka kutoka jela huko Beni katika jimbo la Kivu Kaskazini mwezi Juni.



Yuhi VI Bushaija, 56, akizungumza na The Sunday Times nchini Uingereza amesema kuwa ana ndoto za kurudi nchini Rwanda kama mfalme.


Bushaija amesema kuwa alishangaa baada ya kusikia kuwa ndiye atakayechukua nafasi ya mfalme baada ya kifo cha mjomba wake,Kigeli V Ndahindurwa mwezi wa Januari 2017 nchini Marekani.


Kwenye mazungumzo haya,Bushaija ameleza kuwa hatakubali kumaliza milenia akiwa ukimbizini na kuwa ana ndoto za kurudi nchini Rwamda kama mfalme asiyekuwa wa ukimbizini.
...
Bushaija ameleza”Nina ndoto za kurudi nchini Rwanda kama mfalme asiyekuwa wa ukimbizini siku moja”.
Pia ameongeza kwamba ataendelea kutii mila na desturi vya Wanyarwanda na kusaidia Wanyarwanda popote walipo.

Pamoja na haya,Bushaija ameonyesha upendo wake kwa familia ya ufalme wa Uimgereza Kupitia ujumbe alioutuma ili kumtakia mwanafalme Harry na mchumba wake,Meghan Markle kwa niaba ya wanyarwanda kwa kusema”Kwa niaba ya Wanyarwanda,nawatakia mema kwenye ndoa yenu.Ningetaka kuja kwenye harusi yenu lakini inawezekana kuwa kuna wageni wa kutosha”.


Yuhi VI Bushaija alifunga ndoa na mwanamke Lilian,49, walibalikiwa watoto watatu;msichana mmoja na wavulana wawili.Alizaliwa nchini Rwanda na kulelewa nchini Uganda alipohamia na kuenda Kenya kisha akaenda nchini Uingereza mwaka 2000.


Bushaija ametangaza kurudi nchini Rwanda kama mfalme wakati ambapo Rwanda ni Jamhuri tangu mwaka 1962.

Rais Donald Trump amezua shutuma kwamba huenda alizuia haki kutendeka baada ya kutuma ujumbe katika mtandao wa Twitter kwamba alimfuta kazi mshauri wake wa maswala ya usalama Michael Flynn kwa sababu aliwadanganya maafisa wa FBI.

Baadhi ya wataalam wa maswala ya sheria wanasema kuwa matamshi yake yalionyesha kuwa bwana Trump alijua kwamba mshauri wake wa zamani alikuwa amewahadaa wachunguzi wakati alipomtaka mkurugenzi wa zamani wa FBI James Comey kusitisha uchunguzi dhidi yake.


Rais huyo alisisitiza kuwa vitendo vya mshauri wake wa zamani vilifuata sheria.


Siku ya ijumaa Michael Flynn alikuwa mwanachama wa kwanza wa utawala wa rais Trump kushtakiwa kufuatia uchunguzi kuhusu hatua ya Urusi kuingilia uchaguzi wa urais wa Marekani mwaka jana.


Wakati huohuo Chombo cha habari cha Marekani ABC, kimemsimamisha kazi kwa muda mwandishi wake wa maswala ya uchunguzi , Brian Ross kufuatia makosa katika ripoti yake kuhusu bwana Michael Flyn ambayo ilisababisha kuanguka kwa sarafu ya dola na soko la hisa nchini Marekani kwa muda .


Siku ya Ijumaa Chombo hicho cha habari kiliripoti kwamba bwana Flyn alitarajiwa kutoa ushahidi uliodai kwamba rais Donald Trump alimuagiza kuwasiliana na Urusi.


Kampuni hiyo baadaye ilirekebisha ripoti hiyo ikisema kuwa haikuwa imekaguliwa na kwamba ilikuwa ya makosa.


Mwandishi huyo sasda amesimamishwa kazi kwa mwezi mmoja bila malipo.

Takriban watu 13 wamefariki baada ya mashua ya uvuvi kugonga na meli kubwa na kusababisha mashua hiyo kupinduka nje ya pwani ya Korea Kusini.

Watu wengine wawili hawajulikani waliko na walinzi wa pwani ya Korea Kusini wanasema kuwa oporesheni ya kuwatafuta na kuwaokoa inaendelea.


Mashua hiyo ya uvuvi ya Seonchang-1 ilikuwa imewabeba abiria 20 na wahudumia wawili wakati ajali hiyo ilitokea.


Picha zilionyesha mashua hiyo ikiwa imepinduka.

Ndege za helikopta na na meli kadhaa zinashiriki katika shughuli za kuitafuta.


Kisa hicho kinatajwa kuwa kibaya ziadi nchini Korea Kusini tangu watu 15 waangamiae baharini eneo la Jeju mwaka 2015.


Kabla ya mwaka huo feri ya abiria ilipinduka ambapo zaidi ya watu 300 walifariki wengi wao watoto wa shule.



Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa amefanyia baraza lake la mawaziri mabadiliko siku mbili baada ya kulitangaza baraza jipya

Wakosoaji wanasema kuwa orodha ya kwanza ilionyesha kuwa mnangagwa hakuwa na mpango wa kuleta mabadiliko nchini humo.


Wizara za elimu na kazi sasa zimefanyiwa mabadiliko ili kuambatana na katiba.
Lakini makamanda wa jeshi ndo walipewa wizara za mashauri ya nchi za kigeni na ardhi.


Siku 10 zilizopita alirudi kutoka uhamishoni kufuatia mapinduzi ya kijeshi dhidi ya Robert Mugabe na kuahidi kuhudumia raia wote kwa njia sawa.

Siku ya Jumamosoi serikali ilitangaza kuwa wizara mbili zemefanyiwa mabadiliko kuhakikisha kuwa katiba imefuatwa kwa misingi na jinsia, kikanda na mahitaji maalumu.


Ripoti zinasema kuwa orodha kwanza hakufuata katiba ambayo inataka kuwepo mawaziri wasiokuwa wabunge.


Baadhi ya wafuasi wa upinzani walisherehekea hatua ya kumuona waziri wa elimu Lazarus Dokora akiondolewa wakisema amechangia kushuka kwa viwango vya elimu miaka michache iliyopita.
Naibu wake Paul Mavima amechukua mahala pake.

HABARI KIMATAIFA



Ayman Safadi alisema alimuambia waziri wa mashauri wa nchi za kigeni wa Marekani Rex Tillerson kuwa hatua kama hiyo inaweza kuzua ghadhabu kubwa kwa nchi za kiarabu na ulimwengu wa kiisalmu.

Kuna uvumi kuwa Rais Donald Trump atatangaza hilo hivi karibuni na kutimiza ahadi yake aliyotoa wakati wa kampeni.

Jared Kushner, mkwe wa Trump alisema kuwa bado hakuna uamuzi uliofanywa.

Katika mtandao wa Twitter, Bw Safadi alisema: #Nilizungumza na waziri Rex Tillerson kuhusu hatari ya kuutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel. 

Hatua kama hiyo inaweza kusababisha ghadhabu kwenye nchi za kiarabu na kwa ulimwengi wa kiislamu na kuzua misukosuko na pia kuhujumu jitihada za amani."
 
Hakuna jibu lolote kutoka kwa wizara ya mashauri ya nchi za kigeni nchini Marekani.
Naye rais wa Palestina Mahmoud Abbas anajaribu kupata uungwaji mkono wa kimataifa katika kumshawishi Trump asifanye tangazo kama hilo.

Ofisi yake ilisema kwa aliwapigia simu Jumapili viongozi wa dunia wakiwemo rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan.

"Alitaka kulezea harari za uamuzi wowote wa kuhamisha ubalozo wa Marekani kwenda Jerusalem au kuutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Isael," mshauri wa Bw. Abbas, Majdi al-Khalidi aliliambia shirika la AFP.

Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni nchini Jardan ameonya Marekani kuhusu hatari ya kuutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel.

Korea Kaskazini imesema Rais Donald Trump wa Marekani na serikali yake "wanabembeleza vitokee vita vya nyuklia" huku Washington na muitifaki wake katika Peninsula ya Korea, yaani Korea Kusini zikijiandaa kufanya manuva makubwa ya kijeshi ya angani.

Wizara ya Mambo ya Nje ya Korea Kaskazini imeeleza katika taarifa iliyotoa hapo jana kuwa Trump anaanzisha mchezo hatari wa kamari ya nyuklia katika Peninsula ya Korea na kumwita rais huyo wa Marekani 'jini mbaya wa nyuklia' na 'mvurugaji amani ya dunia'.


Taarifa hiyo ya wizara ya mambo ya nje ya Korea Kaskazini imetolewa katika hali ambayo Marekani na Korea Kusini zinajiandaa kwa mazoezi ya kijeshi yaliyopewa jina la Vigilant Ace yaliyopangwa kuanza Jumatatu ya kesho. Askari wapatao 12,000 wa jeshi la Marekani na ndege za kivita 230 wanatazamiwa kushiriki kwenye manuva hayo.


Hayo yanajiri huku kauli za vitisho zinazotolewa na Marekani dhidi ya Korea Kaskazini zikikabiliwa na ukosoaji mkali.


Baada ya Korea Kaskazini kulifanyia majaribio kombora lake la balistiki la masafa marefu zaidi, mapema wiki hii balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa Nikki Haley aliionya serikali ya Pyongyang kuwa nchi hiyo inaweza "kuangamizwa kikamilifu" endapo vita vitatokea kati yake na Washington.


Hata hivyo matamshi hayo ya Haley yalikosolewa vikali na Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia Sergei Lavrov, ambaye siku ya Ijumaa alisema: "kama kuna mtu aliyedhamiria kikweli kutumia nguvu, kama alivyoeleza mwakilishi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa ili kuiangamiza Korea Kaskazini.. nadhani atakuwa anachezea moto na kufanya kosa kubwa".


Korea Kaskazini inakabiliwa na vikwazo mbalimbali vya kimataifa vya kuishinikiza isimamishe mipango yake ya nyuklia na makombora. Hata hivyo imepuuza mashinikizo yote yanayotolewa dhidi yake huku ikiapa kuwa haitoachana na mipango yake ya nyuklia na makombora kutokana na vitisho na uadui wa Marekani dhidi ya nchi hiyo.


Imebainika kuwa, baadhi ya raia wa Kiafrika wanaopigwa mnada katika magendo ya binadamu nchini Libya wananyofolewa viungo vyao vya mwili na kuuzwa.

Wakili na mwanaharakati mashuhuri Bobby Banson amenukuliwa na tovuti ya habari ya GhanaWeb akisema kuwa, binafsi ameshuhudia kanda ya video inayoonyesha mmoja wa 'watumwa' hao akieleza jinsi viungo vya mwili vya mwenzake vilivyong'olewa na kuuzwa.


Amebainisha kuwa: "Ukweli wa mambo ni kuwa, baadhi ya raia hao wa Afrika hawauzwi kwa ajili ya kwenda kufanya kazi Ulaya, bali kwa ajili ya biashara ya viungo vya binadamu kama maini na mapafu."


Wakili huyo na mtetezi wa haki za binadamu ameongeza kuwa, wahajiri hao waliojikuta kwenye mtego wa magendo ya binadamu wanapewa dawa za kulala na kisha viungo vyao vinachukuliwa."
Wahajiri wa Afrika wanaouzwa kama bidhaa nchini Libya


Hivi karibuni, televisheni ya CNN ilirusha hewani mubashara mnada wa kuuza Waafrika huko nchini Libya ambapo kila mtu alikuwa akiuzwa kwa dola zisizopungua 400 za Kimarekani.
Duru mbali mbali za kimataifa, ukiwemo Umoja wa Afrika na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa zimekosoa vikali biashara hiyo ya utumwa mambo leo inayofanyika nchini Libya.



Wafungwa kumi na tisa, wengi wao wanaokabiliwa na mashtaka ya ubakaji, wametoroka jela mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo usiku wa kuamkia leo, na kusababisha hofu ya kulipiza kisasi kwa waathirika wa vitendo vyao, vyanzo vya serikali za ndani vimesema.



Kwa mujibu wa msimamizi wa gereza Gerard Nkwana, katika jimbo la Kivu Kusini Wafungwa hao 19 walitoroka katika gereza la Kalehe lenye wafungwa 20.


Pascal Nabulera, mkuu wa shirika la kijamii jamii la Kalehe, ametangazia RFI kuwa Watu wanaofika mahakamani kufungua kesi na mashahidi sasa wanawasiwasi wa kulipiziwa kisasi na wafungwa hao waliotoroka.



Nchi ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo yenye umasikini na inayopambana na mgawanyiko wa kisiasa na kikabila pamoja na machafuko mashariki mwa nchi inakabiliwa na matatizo makubwa katika mfumo wake wa mahakama.



Mnamo Mei, wafungwa 4,000 walitoroka katika gereza la Makala huko Kinshasa, mji mkuu, wakati 900 wakitoroka kutoka jela huko Beni katika jimbo la Kivu Kaskazini mwezi Juni.



Yuhi VI Bushaija, 56, akizungumza na The Sunday Times nchini Uingereza amesema kuwa ana ndoto za kurudi nchini Rwanda kama mfalme.


Bushaija amesema kuwa alishangaa baada ya kusikia kuwa ndiye atakayechukua nafasi ya mfalme baada ya kifo cha mjomba wake,Kigeli V Ndahindurwa mwezi wa Januari 2017 nchini Marekani.


Kwenye mazungumzo haya,Bushaija ameleza kuwa hatakubali kumaliza milenia akiwa ukimbizini na kuwa ana ndoto za kurudi nchini Rwamda kama mfalme asiyekuwa wa ukimbizini.
...
Bushaija ameleza”Nina ndoto za kurudi nchini Rwanda kama mfalme asiyekuwa wa ukimbizini siku moja”.
Pia ameongeza kwamba ataendelea kutii mila na desturi vya Wanyarwanda na kusaidia Wanyarwanda popote walipo.

Pamoja na haya,Bushaija ameonyesha upendo wake kwa familia ya ufalme wa Uimgereza Kupitia ujumbe alioutuma ili kumtakia mwanafalme Harry na mchumba wake,Meghan Markle kwa niaba ya wanyarwanda kwa kusema”Kwa niaba ya Wanyarwanda,nawatakia mema kwenye ndoa yenu.Ningetaka kuja kwenye harusi yenu lakini inawezekana kuwa kuna wageni wa kutosha”.


Yuhi VI Bushaija alifunga ndoa na mwanamke Lilian,49, walibalikiwa watoto watatu;msichana mmoja na wavulana wawili.Alizaliwa nchini Rwanda na kulelewa nchini Uganda alipohamia na kuenda Kenya kisha akaenda nchini Uingereza mwaka 2000.


Bushaija ametangaza kurudi nchini Rwanda kama mfalme wakati ambapo Rwanda ni Jamhuri tangu mwaka 1962.

Rais Donald Trump amezua shutuma kwamba huenda alizuia haki kutendeka baada ya kutuma ujumbe katika mtandao wa Twitter kwamba alimfuta kazi mshauri wake wa maswala ya usalama Michael Flynn kwa sababu aliwadanganya maafisa wa FBI.

Baadhi ya wataalam wa maswala ya sheria wanasema kuwa matamshi yake yalionyesha kuwa bwana Trump alijua kwamba mshauri wake wa zamani alikuwa amewahadaa wachunguzi wakati alipomtaka mkurugenzi wa zamani wa FBI James Comey kusitisha uchunguzi dhidi yake.


Rais huyo alisisitiza kuwa vitendo vya mshauri wake wa zamani vilifuata sheria.


Siku ya ijumaa Michael Flynn alikuwa mwanachama wa kwanza wa utawala wa rais Trump kushtakiwa kufuatia uchunguzi kuhusu hatua ya Urusi kuingilia uchaguzi wa urais wa Marekani mwaka jana.


Wakati huohuo Chombo cha habari cha Marekani ABC, kimemsimamisha kazi kwa muda mwandishi wake wa maswala ya uchunguzi , Brian Ross kufuatia makosa katika ripoti yake kuhusu bwana Michael Flyn ambayo ilisababisha kuanguka kwa sarafu ya dola na soko la hisa nchini Marekani kwa muda .


Siku ya Ijumaa Chombo hicho cha habari kiliripoti kwamba bwana Flyn alitarajiwa kutoa ushahidi uliodai kwamba rais Donald Trump alimuagiza kuwasiliana na Urusi.


Kampuni hiyo baadaye ilirekebisha ripoti hiyo ikisema kuwa haikuwa imekaguliwa na kwamba ilikuwa ya makosa.


Mwandishi huyo sasda amesimamishwa kazi kwa mwezi mmoja bila malipo.

Takriban watu 13 wamefariki baada ya mashua ya uvuvi kugonga na meli kubwa na kusababisha mashua hiyo kupinduka nje ya pwani ya Korea Kusini.

Watu wengine wawili hawajulikani waliko na walinzi wa pwani ya Korea Kusini wanasema kuwa oporesheni ya kuwatafuta na kuwaokoa inaendelea.


Mashua hiyo ya uvuvi ya Seonchang-1 ilikuwa imewabeba abiria 20 na wahudumia wawili wakati ajali hiyo ilitokea.


Picha zilionyesha mashua hiyo ikiwa imepinduka.

Ndege za helikopta na na meli kadhaa zinashiriki katika shughuli za kuitafuta.


Kisa hicho kinatajwa kuwa kibaya ziadi nchini Korea Kusini tangu watu 15 waangamiae baharini eneo la Jeju mwaka 2015.


Kabla ya mwaka huo feri ya abiria ilipinduka ambapo zaidi ya watu 300 walifariki wengi wao watoto wa shule.



Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa amefanyia baraza lake la mawaziri mabadiliko siku mbili baada ya kulitangaza baraza jipya

Wakosoaji wanasema kuwa orodha ya kwanza ilionyesha kuwa mnangagwa hakuwa na mpango wa kuleta mabadiliko nchini humo.


Wizara za elimu na kazi sasa zimefanyiwa mabadiliko ili kuambatana na katiba.
Lakini makamanda wa jeshi ndo walipewa wizara za mashauri ya nchi za kigeni na ardhi.


Siku 10 zilizopita alirudi kutoka uhamishoni kufuatia mapinduzi ya kijeshi dhidi ya Robert Mugabe na kuahidi kuhudumia raia wote kwa njia sawa.

Siku ya Jumamosoi serikali ilitangaza kuwa wizara mbili zemefanyiwa mabadiliko kuhakikisha kuwa katiba imefuatwa kwa misingi na jinsia, kikanda na mahitaji maalumu.


Ripoti zinasema kuwa orodha kwanza hakufuata katiba ambayo inataka kuwepo mawaziri wasiokuwa wabunge.


Baadhi ya wafuasi wa upinzani walisherehekea hatua ya kumuona waziri wa elimu Lazarus Dokora akiondolewa wakisema amechangia kushuka kwa viwango vya elimu miaka michache iliyopita.
Naibu wake Paul Mavima amechukua mahala pake.