Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » ULIMWENGU: TUTAWATOA NA KUINGIA FAINALI.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Thomas Emmanuel Ulimwengu amesema klabu yake, TP Mazembe ya DRC inakabiliwa na mtihani mgumu katika Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika, kwani wapinzani wao El Merreikh ya Sudan ni wazuri.
Akizungumza na BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE leo kwa simu kutoka Lubumbashi, Ulimwengu amesema pamoja na ukweli huo, lakini wamepania kuwang’oa.
“Merreikh ni wazuri, hilo hata sisi tunalijua, lakini tutawatoa tu,”amesema Uli na alipoulizwa watawezaje iwapo walishindwa kufurukuta kwa timu nyingine ya Sudan, El Hilal akasema; “Ile ilikuwa hatua ya makundi, sasa ni mtoano,”.


Thomas Ulimwengu amekiri Merreikh ni wazuri, lakini amesema TP Mazembe itawatoa
Ulimwengu amesema wanafahamu ubora wa timu za Sudan hususan Merreikh na mbinu zao zote za ndani na nje ya Uwanja, lakini wamejipanga kikamilifu kuhakikisha wanawatoa. 
TP Mazembe itamenyana na El Merreikh katika Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika, mchezo wa kwanza ukichezwa Septemba 25, mwaka huu mjini Khartoum na marudiano Oktoba 2 mjini Lubumbashi.
Huo ni mtihani mkubwa kwa Mazembe, kwani imekuwa ikisumbuliwa mno na timu za Sudan- katika hatua ya makundi mwaka huu ilipangwa na El Hilal na haikushinda hata mchezo mmoja.
Mchezo wa kwanza Lubumbashi ililazimishwa sare kabla ya kufungwa 1-0 mchezo wa marudiano Sudan- na saa wanakutana na timu ambayo inaaminika ndiyo bora zaidi nchini humo. 
Nusu Fainali nyingine ya Ligi ya Mabingwa Afrika itakuwa kati ya El Hilal ya Sudan na USM Alger ya Algeria, nao pia mechi ya kwanza itakuwa Septemba 25 na marudiano Oktoba 2, mwaka huu.


About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / ULIMWENGU: TUTAWATOA NA KUINGIA FAINALI.

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Thomas Emmanuel Ulimwengu amesema klabu yake, TP Mazembe ya DRC inakabiliwa na mtihani mgumu katika Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika, kwani wapinzani wao El Merreikh ya Sudan ni wazuri.
Akizungumza na BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE leo kwa simu kutoka Lubumbashi, Ulimwengu amesema pamoja na ukweli huo, lakini wamepania kuwang’oa.
“Merreikh ni wazuri, hilo hata sisi tunalijua, lakini tutawatoa tu,”amesema Uli na alipoulizwa watawezaje iwapo walishindwa kufurukuta kwa timu nyingine ya Sudan, El Hilal akasema; “Ile ilikuwa hatua ya makundi, sasa ni mtoano,”.


Thomas Ulimwengu amekiri Merreikh ni wazuri, lakini amesema TP Mazembe itawatoa
Ulimwengu amesema wanafahamu ubora wa timu za Sudan hususan Merreikh na mbinu zao zote za ndani na nje ya Uwanja, lakini wamejipanga kikamilifu kuhakikisha wanawatoa. 
TP Mazembe itamenyana na El Merreikh katika Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika, mchezo wa kwanza ukichezwa Septemba 25, mwaka huu mjini Khartoum na marudiano Oktoba 2 mjini Lubumbashi.
Huo ni mtihani mkubwa kwa Mazembe, kwani imekuwa ikisumbuliwa mno na timu za Sudan- katika hatua ya makundi mwaka huu ilipangwa na El Hilal na haikushinda hata mchezo mmoja.
Mchezo wa kwanza Lubumbashi ililazimishwa sare kabla ya kufungwa 1-0 mchezo wa marudiano Sudan- na saa wanakutana na timu ambayo inaaminika ndiyo bora zaidi nchini humo. 
Nusu Fainali nyingine ya Ligi ya Mabingwa Afrika itakuwa kati ya El Hilal ya Sudan na USM Alger ya Algeria, nao pia mechi ya kwanza itakuwa Septemba 25 na marudiano Oktoba 2, mwaka huu.



«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :