Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » VURUGU KATIKA KAMPENI ZA KISIASA ZA SAMBAA MIKOA MINNE.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

VURUGU zinazoendelea ndani ya umoja wa vyama vinne vya upinzani (Ukawa), kuhusu kuachiana majimbo na kata baada ya kusambaa katika mikoa ya Mtwara, Tabora na Kilimanjaro, sasa zimegonga hodi mkoani Morogoro.

Hali hiyo ambayo imevuruga hadi majimbo ya wenyeviti wenza wa Ukawa, ni tofauti na mtafaruku mwingine unaoendelea ndani ya chama kimoja katika safu za uongozi wa juu, ambazo zimepewa jina la ‘kushuka njiani wakati safari ikiendelea’.

Mkoa wa Morogoro una majimbo 11 ya uchaguzi, ambapo CUF katika mgawo huo ilipewa majimbo mawili ambayo ni Kilosa na Morogoro Kusini Mashariki na Chadema ikanyakua majimbo tisa.

Morogoro

Akizungumza na gazeti hili mjini Morogoro jana, mgombea wa Ubunge wa Jimbo la Kilosa, Abeid Mlapakolo (CUF), alisema pamoja na kuwa na makubaliano hayo, ameshangazwa kuona Chadema imemsimamisha mgombea ambaye anaendelea kufanya kampeni katika kata mbalimbali zilizomo kwenye jimbo hilo.

Kwa mujibu wa Mlapakolo, mgombea huyo wa ubunge wa Chadema, Rajab Msabaha, tayari ameshasambaza mabango na vipeperushi maeneo mbalimbali ndani ya jimbo hilo na amekuwa akifanya kampeni kinyume na makubaliano yaliyofikiwa na viongozi wa Ukawa.

Mlapakolo alidai mbali na kupiga kampeni, Msabaha pia alishiriki katika mapokezi ya mgombea wa urais wa Chadema anayeungwa mkono na Ukawa, Edward Lowassa alipowasili Kata ya Dumila iliyopo katika Jimbo la Kilosa Septemba 15, mwaka huu na wafuasi wake kadhaa.

“Jimboni ni vurugu tupu, wafuasi wa Chadema wananivurugia shughuli za kampeni...mimi ndiye mgombea halali wa Ukawa Jimbo la Kilosa, lakini ndugu zangu hawa wamemweka mgombea wao wa ubunge,” alisema na kuongeza.

Vurugu hizo zimemkuta pia mgombea wa ubunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki, Salama Omary (CUF) ambaye amesema licha ya jimbo hilo kupewa CUF, Chadema nao wamemsimamisha mgombea wa ubunge kinyume na makubaliano.

Salama alisema bado mgombea wa ubunge wa Chadema, David Lugakingira, anaendelea kufanya kampeni za uchaguzi licha ya viongozi wake kumtaka asifanye hiyo.

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / VURUGU KATIKA KAMPENI ZA KISIASA ZA SAMBAA MIKOA MINNE.

VURUGU zinazoendelea ndani ya umoja wa vyama vinne vya upinzani (Ukawa), kuhusu kuachiana majimbo na kata baada ya kusambaa katika mikoa ya Mtwara, Tabora na Kilimanjaro, sasa zimegonga hodi mkoani Morogoro.

Hali hiyo ambayo imevuruga hadi majimbo ya wenyeviti wenza wa Ukawa, ni tofauti na mtafaruku mwingine unaoendelea ndani ya chama kimoja katika safu za uongozi wa juu, ambazo zimepewa jina la ‘kushuka njiani wakati safari ikiendelea’.

Mkoa wa Morogoro una majimbo 11 ya uchaguzi, ambapo CUF katika mgawo huo ilipewa majimbo mawili ambayo ni Kilosa na Morogoro Kusini Mashariki na Chadema ikanyakua majimbo tisa.

Morogoro

Akizungumza na gazeti hili mjini Morogoro jana, mgombea wa Ubunge wa Jimbo la Kilosa, Abeid Mlapakolo (CUF), alisema pamoja na kuwa na makubaliano hayo, ameshangazwa kuona Chadema imemsimamisha mgombea ambaye anaendelea kufanya kampeni katika kata mbalimbali zilizomo kwenye jimbo hilo.

Kwa mujibu wa Mlapakolo, mgombea huyo wa ubunge wa Chadema, Rajab Msabaha, tayari ameshasambaza mabango na vipeperushi maeneo mbalimbali ndani ya jimbo hilo na amekuwa akifanya kampeni kinyume na makubaliano yaliyofikiwa na viongozi wa Ukawa.

Mlapakolo alidai mbali na kupiga kampeni, Msabaha pia alishiriki katika mapokezi ya mgombea wa urais wa Chadema anayeungwa mkono na Ukawa, Edward Lowassa alipowasili Kata ya Dumila iliyopo katika Jimbo la Kilosa Septemba 15, mwaka huu na wafuasi wake kadhaa.

“Jimboni ni vurugu tupu, wafuasi wa Chadema wananivurugia shughuli za kampeni...mimi ndiye mgombea halali wa Ukawa Jimbo la Kilosa, lakini ndugu zangu hawa wamemweka mgombea wao wa ubunge,” alisema na kuongeza.

Vurugu hizo zimemkuta pia mgombea wa ubunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki, Salama Omary (CUF) ambaye amesema licha ya jimbo hilo kupewa CUF, Chadema nao wamemsimamisha mgombea wa ubunge kinyume na makubaliano.

Salama alisema bado mgombea wa ubunge wa Chadema, David Lugakingira, anaendelea kufanya kampeni za uchaguzi licha ya viongozi wake kumtaka asifanye hiyo.


«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :