Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » AJALI YAUA 12 NA 28 KUJERUHIWA MKOANI IRINGA LEO
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

 
Abiria 12 wamefariki dunia leo mkoani Iringa  na wengine 28 wamejeruhiwa vibaya baada ya basi la abiria la kampuni ya New Force kugongana na lori maeneo ya Igeme, Kilolo mchana wa leo. 
 
Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi mkoani Iringa, basi la abiria la New Force lilikuwa linatokea jijini Dar es Salaam kuelekea Tunduma, mkoani Mbeya, na baada ya kugongana na gari hilo la mizigo, lilipinduka. 

Kufuatia ajali hiyo watu wasiopungua 12 wamefariki dunia papo hapo huku makumi ya wengine wakijeruhiwa. Taarifa zaidi zinasema, majeruhi 28 hali zao ni mbaya sana. 

Jeshi la Polisi mkoani Iringa limethibisha kutokea ajali hiyo na kuongeza kuwa majeruhi wamewahishwa hospitali ya wilaya ya Kilolo huku wengine waliokuwa taabani wamekimbizwa hospitali ya mkoa wa Iringa kwa ajili ya matibabu. 

Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi Iringa, madereva wa basi na lori ni miongoni mwa watu waliojeruhiwa katika ajali hiyo na uchunguzi unaendelea. 

Tanzania imekuwa ikishuhudia ajali za mara kwa mara za barabarani ambapo makumi ya watu wamekuwa wakipoteza maisha yao na wengine kujeruhiwa au hata kupata vilema vya maisha. Uchunguzi uliofanywa unaonesha kuwa, uzembe wa madereva na mwendo wa kasi ndizo sababu kuu mbili zinazosababisha mlolongo wa ajali za barabarani nchini Tanzania.

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / AJALI YAUA 12 NA 28 KUJERUHIWA MKOANI IRINGA LEO

 
Abiria 12 wamefariki dunia leo mkoani Iringa  na wengine 28 wamejeruhiwa vibaya baada ya basi la abiria la kampuni ya New Force kugongana na lori maeneo ya Igeme, Kilolo mchana wa leo. 
 
Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi mkoani Iringa, basi la abiria la New Force lilikuwa linatokea jijini Dar es Salaam kuelekea Tunduma, mkoani Mbeya, na baada ya kugongana na gari hilo la mizigo, lilipinduka. 

Kufuatia ajali hiyo watu wasiopungua 12 wamefariki dunia papo hapo huku makumi ya wengine wakijeruhiwa. Taarifa zaidi zinasema, majeruhi 28 hali zao ni mbaya sana. 

Jeshi la Polisi mkoani Iringa limethibisha kutokea ajali hiyo na kuongeza kuwa majeruhi wamewahishwa hospitali ya wilaya ya Kilolo huku wengine waliokuwa taabani wamekimbizwa hospitali ya mkoa wa Iringa kwa ajili ya matibabu. 

Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi Iringa, madereva wa basi na lori ni miongoni mwa watu waliojeruhiwa katika ajali hiyo na uchunguzi unaendelea. 

Tanzania imekuwa ikishuhudia ajali za mara kwa mara za barabarani ambapo makumi ya watu wamekuwa wakipoteza maisha yao na wengine kujeruhiwa au hata kupata vilema vya maisha. Uchunguzi uliofanywa unaonesha kuwa, uzembe wa madereva na mwendo wa kasi ndizo sababu kuu mbili zinazosababisha mlolongo wa ajali za barabarani nchini Tanzania.

«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :