Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » CAR YATAKA UCHAGUZI KUAHIRISHWA
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Serikali ya mpito nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati imependekeza uchaguzi mkuu nchini humo uahirishwe kwa siku tatu.

Uchaguzi wa urais na ubunge ulipangiwa kufanyika Jumapili lakini serikali inasema maandalizi hayajakamilika na inataka uahirishwe hadi Desemba 30.

Pendekezo hilo lilitolewa Alhamisi kwenye mkutano uliohudhuriwa na wawakilishi wa wagombea, vyama vya siasa, tume ya uchaguzi na jamii ya kimataifa.

“Tarehe 30 Desemba itakuwa bora kwetu,” mkuu wa tume ya uchaguzi Marie-Madeleine
N'kouet Hoornaert alisema alipoulizwa na Rais wa mpito Catherine Samba Panza kuhusu wakati mwafaka wa kufanyika kwa uchaguzi huo.

Mabadiliko yoyote kwenye siku ya uchaguzi yatahitajika kuidhinishwa na Mahakama ya Kikatiba kwani sheria ya sasa inataka uchaguzi ufanyike siku a Jumapili.

Haijabainika ni lini mahakama hiyo ingekutana kujadili hilo.

Umoja wa Mataifa umesema kuahirishwa kwa uchaguzi huo, ambao tayari umecheleweshwa, hakutaathiri pakubwa mchakato wa kuwatafuta viongozi wapya.

“Siwezi kutaja hilo kama pigo” kwa shughuli hii ya kisiasa, msemaji wa UN Stephane Dujarric amesema.

Alieleza kuwa karatasi zote za kura ziliwasili mji mkuu Bangui Jumatano na walinda Amani wa UN kwa jina MINUSCA wataendelea kufikisha karatasi hizo maeneo mbalimbali ya nchi.

Uchaguzi huo unatarajiwa kurejesha uthabiti kwenye taifa hilo lililotikiswa na machafuko tangu waasi wa Kiislamu walipompindua kiongozi Mkristo Francois Bozize mwaka 2013.

Jumatatu, maafisa wa uchaguzi walisema kura ya maamuzi iliyokuwa imeandaliwa kuidhinisha uchaguzi wa urais na ubunge ilikuwa imeungwa mkono na asilimia 93 ya wapiga kura.

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / CAR YATAKA UCHAGUZI KUAHIRISHWA

Serikali ya mpito nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati imependekeza uchaguzi mkuu nchini humo uahirishwe kwa siku tatu.

Uchaguzi wa urais na ubunge ulipangiwa kufanyika Jumapili lakini serikali inasema maandalizi hayajakamilika na inataka uahirishwe hadi Desemba 30.

Pendekezo hilo lilitolewa Alhamisi kwenye mkutano uliohudhuriwa na wawakilishi wa wagombea, vyama vya siasa, tume ya uchaguzi na jamii ya kimataifa.

“Tarehe 30 Desemba itakuwa bora kwetu,” mkuu wa tume ya uchaguzi Marie-Madeleine
N'kouet Hoornaert alisema alipoulizwa na Rais wa mpito Catherine Samba Panza kuhusu wakati mwafaka wa kufanyika kwa uchaguzi huo.

Mabadiliko yoyote kwenye siku ya uchaguzi yatahitajika kuidhinishwa na Mahakama ya Kikatiba kwani sheria ya sasa inataka uchaguzi ufanyike siku a Jumapili.

Haijabainika ni lini mahakama hiyo ingekutana kujadili hilo.

Umoja wa Mataifa umesema kuahirishwa kwa uchaguzi huo, ambao tayari umecheleweshwa, hakutaathiri pakubwa mchakato wa kuwatafuta viongozi wapya.

“Siwezi kutaja hilo kama pigo” kwa shughuli hii ya kisiasa, msemaji wa UN Stephane Dujarric amesema.

Alieleza kuwa karatasi zote za kura ziliwasili mji mkuu Bangui Jumatano na walinda Amani wa UN kwa jina MINUSCA wataendelea kufikisha karatasi hizo maeneo mbalimbali ya nchi.

Uchaguzi huo unatarajiwa kurejesha uthabiti kwenye taifa hilo lililotikiswa na machafuko tangu waasi wa Kiislamu walipompindua kiongozi Mkristo Francois Bozize mwaka 2013.

Jumatatu, maafisa wa uchaguzi walisema kura ya maamuzi iliyokuwa imeandaliwa kuidhinisha uchaguzi wa urais na ubunge ilikuwa imeungwa mkono na asilimia 93 ya wapiga kura.

«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :