Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » MATEKA WA IRAN KULIPWA KWA MIAKA 36
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Wamarekani waliozuiliwa mateka nchini Iran watalipwa fidia miaka 36 baada ya kisa hicho, ripoti zinasema.

Kila mmoja kati ya mateka hao 53, au jamaa zake, atapokea fidia ya $4.4m (£3m), kwa mujibu wa mswada wa matumizi ya pesa Marekani ambao ulipitishwa Ijumaa.

Waathiriwa wa mashambulio mengine ya kigaidi yaliyofadhiliwa na dila, kama vile mashambulio ya bomu katika balozi za Marekani Afrika Mashariki mwaka 1998 pia watakuwa na nafasi ya kulipwa fidia.

Wamarekani hao walizuiliwa mateka siku 444, na kisa hicho kilipelekea Marekani kukatiza uhusiano wake na Iran.

Uamuzi wa kulipa fidia umetokea baada ya mwafaka tata uliotiwa saini kati ya mataifa yenye ushawishi mkubwa duniani na Iran kuhusu mpango wake wa nyuklia.

Matekani hao wamepigania fidia kwa miaka mingi lakini mwafaka uliofanikisha kuachiliwa kwao ulikuwa na kifungu cha kuwazuia kuwasilisha madai ya fidia.

Majaribio yao mara kwa mara yalizuiwa na mahakama, ikiwa ni pamoja na rufaa iliyokataliwa na Mahakama ya Juu.

Bunge halikuweza kupitisha sheria za kuwalipa fidia.

Pesa watakazolipwa sasa huenda zikatoka kwa faini kubwa ya $9bn iliyotozwa benki ya Paribas ya Ufaransa kwa kukiuka vikwazo vilivyowekewa Iran, Sudan na Cuba, gazeti la New York Times limeripoti.

Jumla ya $1bn zitatumiwa kufidia waathiriwa wa ugaidi na $2.8bn zitatendwa kusaidia waathiriwa wa shambulio la 9/11 na familia zao.

Sheria hiyo mpya inatoa fursa ya kulipwa $10,000 kwa kila siku ambayo mateka alizuiliwa, huku wanandoa na watoto nao wakilipwa hadi $600,000. Malipo ya kwanza yatatolewa katika kipindi cha mwaka mmoja.

Mateka 36 kati ya 53 waliozuiliwa mateka ubalozi wa Marekani mjini Tehran ulipovamiwa bado wako hai.

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / MATEKA WA IRAN KULIPWA KWA MIAKA 36

Wamarekani waliozuiliwa mateka nchini Iran watalipwa fidia miaka 36 baada ya kisa hicho, ripoti zinasema.

Kila mmoja kati ya mateka hao 53, au jamaa zake, atapokea fidia ya $4.4m (£3m), kwa mujibu wa mswada wa matumizi ya pesa Marekani ambao ulipitishwa Ijumaa.

Waathiriwa wa mashambulio mengine ya kigaidi yaliyofadhiliwa na dila, kama vile mashambulio ya bomu katika balozi za Marekani Afrika Mashariki mwaka 1998 pia watakuwa na nafasi ya kulipwa fidia.

Wamarekani hao walizuiliwa mateka siku 444, na kisa hicho kilipelekea Marekani kukatiza uhusiano wake na Iran.

Uamuzi wa kulipa fidia umetokea baada ya mwafaka tata uliotiwa saini kati ya mataifa yenye ushawishi mkubwa duniani na Iran kuhusu mpango wake wa nyuklia.

Matekani hao wamepigania fidia kwa miaka mingi lakini mwafaka uliofanikisha kuachiliwa kwao ulikuwa na kifungu cha kuwazuia kuwasilisha madai ya fidia.

Majaribio yao mara kwa mara yalizuiwa na mahakama, ikiwa ni pamoja na rufaa iliyokataliwa na Mahakama ya Juu.

Bunge halikuweza kupitisha sheria za kuwalipa fidia.

Pesa watakazolipwa sasa huenda zikatoka kwa faini kubwa ya $9bn iliyotozwa benki ya Paribas ya Ufaransa kwa kukiuka vikwazo vilivyowekewa Iran, Sudan na Cuba, gazeti la New York Times limeripoti.

Jumla ya $1bn zitatumiwa kufidia waathiriwa wa ugaidi na $2.8bn zitatendwa kusaidia waathiriwa wa shambulio la 9/11 na familia zao.

Sheria hiyo mpya inatoa fursa ya kulipwa $10,000 kwa kila siku ambayo mateka alizuiliwa, huku wanandoa na watoto nao wakilipwa hadi $600,000. Malipo ya kwanza yatatolewa katika kipindi cha mwaka mmoja.

Mateka 36 kati ya 53 waliozuiliwa mateka ubalozi wa Marekani mjini Tehran ulipovamiwa bado wako hai.

«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :