Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » WALIYOYASEMA MAASKOFU WA DODOMA SIKU YA CHRISTMAS JUU YA DK MAGUFULI NA UONGOZI WAKE
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Na John Banda Dodoma

MAASKOFU Mkoani Dodoma wamewaomba Watanzania kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Magufuli aendelee kuisafisha Nchi ambayo iligubikwa na harufu ya ufisadi, rushwa pamoja na kutokuwajibika kwa watendaji wake. 

Kauli hiyo imetolewa jana Mjini hapa na Maaskofu hao kwa nyakati tofauti katika ibada ya kuzaliwa Yesu Kristo.

Kwa upande wake Askofu Amos Kinyunyu wa Kanisa la KKKT Dayosisi ya Dodoma aliwataka Watanzania kuzidi kumuombea Rais Magufuli kutokana na utendaji kazi unaowagusa Watanzania wa hali ya chini.

Alisema wao kama kanisa wataendelea kumuombea ili aweze kufanya kazi  anayoendelea kufanya sasa hivi kwani hata vitabu vitakatifu vinataka usawa katika uchumi wa kipato kwa kila mtu.

‘’Tunawaomba Watanzania wazidi kumuombea Rais wetu kasi aliyonayo aendelee kuwa nayo kwani Mungu anapenda haki katika maisha pamoja na uchumi uliosawa’’

‘’Wakati mwingine hii kauli ya hapa kazi tu inakuwa hata sisi inatuogopesha lakini Mungu ataendelea kumlinda na kumwongoza’’alisema

Naye Mchungaji kiongozi wa Kanisa la Tanzania Assembles of God (CCC)Miuji Dodoma,Samson Mkuyi alisema utawala wa Rais Magufuli unaonekana kuwa ni jibu la Watanzania wengi pamoja na kanisa.

Mchungaji Mkuyi alisema wanafurahishwa na utendaji kazi wake hasa kwenye upande wa maadili ikizingatiwa kuwa kanisa linataka maadili ya kiroho na kimwili.

‘’Tulianza kuyaomba haya miaka mitano sisi kama kanisa tunamwambia asiogope kwani Mungu yupo pamoja na yeye,sisi tunaendelea kumuombea ili mungu aendelee kumpa ulinzi’’alisema

Kwa upande wake Askofu la Kanisa la Anglikani Central Tanganyika Dayosisi ya Kati,Dk Dickson Chilongani aliwataka Watanzania kumuombea Rais Magufuli pamoja na Baraza lake la Mawaziri  ili waweze kuwafanyia kazi Watanzania.

‘’Rais ameonekana kutumbua majipu yaliyokuwa yamejificha katika hili tutaendelea kumuombea ili aweze kuyayatumbua zaidi,pia na kuwafanya watendaji wafanye kazi kwa usahihi’’alisema
mwisho

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / WALIYOYASEMA MAASKOFU WA DODOMA SIKU YA CHRISTMAS JUU YA DK MAGUFULI NA UONGOZI WAKE

Na John Banda Dodoma

MAASKOFU Mkoani Dodoma wamewaomba Watanzania kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Magufuli aendelee kuisafisha Nchi ambayo iligubikwa na harufu ya ufisadi, rushwa pamoja na kutokuwajibika kwa watendaji wake. 

Kauli hiyo imetolewa jana Mjini hapa na Maaskofu hao kwa nyakati tofauti katika ibada ya kuzaliwa Yesu Kristo.

Kwa upande wake Askofu Amos Kinyunyu wa Kanisa la KKKT Dayosisi ya Dodoma aliwataka Watanzania kuzidi kumuombea Rais Magufuli kutokana na utendaji kazi unaowagusa Watanzania wa hali ya chini.

Alisema wao kama kanisa wataendelea kumuombea ili aweze kufanya kazi  anayoendelea kufanya sasa hivi kwani hata vitabu vitakatifu vinataka usawa katika uchumi wa kipato kwa kila mtu.

‘’Tunawaomba Watanzania wazidi kumuombea Rais wetu kasi aliyonayo aendelee kuwa nayo kwani Mungu anapenda haki katika maisha pamoja na uchumi uliosawa’’

‘’Wakati mwingine hii kauli ya hapa kazi tu inakuwa hata sisi inatuogopesha lakini Mungu ataendelea kumlinda na kumwongoza’’alisema

Naye Mchungaji kiongozi wa Kanisa la Tanzania Assembles of God (CCC)Miuji Dodoma,Samson Mkuyi alisema utawala wa Rais Magufuli unaonekana kuwa ni jibu la Watanzania wengi pamoja na kanisa.

Mchungaji Mkuyi alisema wanafurahishwa na utendaji kazi wake hasa kwenye upande wa maadili ikizingatiwa kuwa kanisa linataka maadili ya kiroho na kimwili.

‘’Tulianza kuyaomba haya miaka mitano sisi kama kanisa tunamwambia asiogope kwani Mungu yupo pamoja na yeye,sisi tunaendelea kumuombea ili mungu aendelee kumpa ulinzi’’alisema

Kwa upande wake Askofu la Kanisa la Anglikani Central Tanganyika Dayosisi ya Kati,Dk Dickson Chilongani aliwataka Watanzania kumuombea Rais Magufuli pamoja na Baraza lake la Mawaziri  ili waweze kuwafanyia kazi Watanzania.

‘’Rais ameonekana kutumbua majipu yaliyokuwa yamejificha katika hili tutaendelea kumuombea ili aweze kuyayatumbua zaidi,pia na kuwafanya watendaji wafanye kazi kwa usahihi’’alisema
mwisho

«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :