Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » HIZI HAPA HABARI ZA KIMATAIFA KWA MUDA HUU DECEMBER 04/2015
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

unaweza kupata habari zote hapa za kimataifa kupitia kazenzele1.blogspot.com au kupitia page ya denis kazenzele au omwatani hizi ni fb.




South Africa

Rais wa Uchina Xi Jinping amesema taifa lake litatoa ufadhili wa dola bilioni 60 kwa nchi za Afrika.

Tangazo hilo amelitoa kwenye mkutano mkuu wa ushirikiano kati ya Uchina na nchi za bara Afrika, ambao umeanza leo jijini Johannesburg. Viongozi kadha wa mataifa ya Afrika wanahudhuria.

Tangazo la fedha hizo za mabilioni ya dola ambazo zitatolewa kupitia ruzuku, mikopo na ufadhili wa miradi ya maendeleo lilisubiriwa, lakini kiasi cha fedha kilichoahidiwa kimezidi matarajio.

Sehemu kubwa ya usaidizi huu wa kifedha sana utatolewa kupitia miradi ya miundo mbinu, kusaidia kusisimua ukuaji wa kiuchumi, lakini maelezo zaidi hayajatolewa.

Kiongozi mwenza wa mkutano huo Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amesifu ushirikiano kati ya Uchina na nchi za Afrika.

Amesema watu wanaoishi Uchina na Afrika ni theluthi moja ya watu wote duniani, na kwamba hilo ni soko kubwa la bidhaa.

Uchina, nchi yenye uchumi wa pili kwa ukubwa duniani, imetoa msururu wa mikopo kwa nchi za Afrika, ambazo nazo huuzia taifa hilo mafuta na bidhaa nyingine muhimu.
Hata hivyo, idadi ya bidhaa ambazo mataifa hayo huuzia Uchina imekuwa ikipungua.

Uwekezaji wa Uchina Afrika ulishuka asilimia 40 nusu ya kwanza ya mwaka huu, kwa mujibu wa wizara ya uchumi ya Uchina.

Ziara ya Bw Xi barani Afrika imetazamwa na wengi kama hatua ya kuyahakikishia mataifa ya Afrika kwamba Uchina itaendelea kuwekeza katika bara hilo licha ya kupungua kasi kwa ukuaji wa uchumi wa Uchina.

Mapema wiki hii Uchina na Afrika Kusini zilitia saini mikataba na mikopo ya thamani ya $6.5bn (£4.3bn), inayoangazia zaidi miundo mbinu.

Jumla ya mikataba 26 ilitiwa saini Jumatano, $2.5bn zikienda kwa shirika la reli la serikali.

Kabla ya kutua Afrika Kusini, Bw Xi alizuru Zimbabwe Jumanne, ambako pia aliahidi taifa hilo mikopo ya kusaidia kuinua uchumi wake uliodorora.

Bbcswahili


Cairo
 
Watu 16 wameuawa katika mji mkuu wa Mirsi, Cairo, baada ya bomu kulipuliwa kwenye mgahawa mmoja, ripoti zinasema.

Shambulio hilo limetokea katika eneo la Agouza, katikati mwa jiji hilo.

Gazeti la The Cairo Post linasema watu watatu waliokuwa wamejifunika nyuso zao walirusha bomu mgahawani na kisha kutoroka.

Shirika la habari la Reuters limemnukuu afisa mmoja wa usalama, ambaye hakutajwa jina lake, akisema mmoja wa washukiwa ni mfanyakazi wa zamani wa mgahawa huo.

Mgawaha huo ulikuwa ghorofa ya chini ya ardhi kwenye jengo hilo, jambo lililoifanya vigumu kwa watu kutoroka.

Wahasiriwa walifariki kutokana na majeraha ya moto au kwa kutokana na moshi. Watu watano wamejeruhiwa.

Mji wa Cairo umeshambuliwa mara kadha na watu wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa Kiislamu.

Juhudi za wanamgambo hao wa Kiislamu zilizidi baada ya kung’olewa mamlakani kwa Rais Mohammed Morsi mwaka 2013.

Bbcswahili


Bangkok
Polisi nchini Thailand wanachunguza ripoti kuwa wanamgambo kumi kutoka kundi la wapiganaji wa Islamic state wameingia nchini humo na wanapanga kushambulia sehemu zinazomilikiwa na Urusi.

Shirika la habari nchini urusi la FSB linaamini kuwa kundi hilo limesafiri kutoka nchini Syria.

Sita kati yao wanaripotiwa kuelekea maeneo ya kifahari ya Pattaya na Phuket huku wengine wakiwa hawajulikani waliko.

Polisi nchini Thailand wanasema kwa hawajafanikiwa kuthibitisha uwepo wa raia hao wa Syria. Zaidi ya watu milioni moja unusu raia wa Urusi walizuru Thailand mwaka 2013.

Bbcswahili


Washington

Waziri wa Ulinzi wa Marekani Ash Carter ametangaza kuwa nafasi zote za kazi za kijeshi za kivita sasa zitakuwa wazi pia kwa wanawake wa Marekani.

Carter amesema huduma za kijeshi za Marekani hazitaweza tena kupunguza nusu ya watu wenye ujuzi na vipaji.

Amesema wanawake sasa wanaweza kuendesha magari ya deraya, mizinga na kuongoza askari wa nchi kavu kwenye mapambano.

Mpango huo wa kiistoria unakwenda kinyume na hoja ya mwenyekiti wa Umoja wa Wakuu wa majeshi kwamba Kikosi cha askari wa majini wanaweza kuruhusiwa kuwatenga wanawake katika baadhi ya majukumu kwenye mapambano ya mstari mbele vitani.

Bbcswahili


berlin

Jeshi la Ujerumani linatarajiwa kupeleka ndege sita za upelelezi nchini Syria, kama sehemu ya muungano wa kimataifa katika mapambano dhidi ya kundi lenye itikadi kali la Dola la Kiislamu-IS. 

Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani, Ursula von der Leyen, amethibitisha kuwa ndege za kujaza mafuta pia zitapelekwa nchini humo, pamoja na manowari moja ya kuilinda manowari inayobeba ndege za kijeshi za Ufaransa. 

Amesema mashambulizi ya anga na majeshi ya ardhini, ulikuwa mkakati imara katika mapambano dhidi ya IS. 

Aidha, wanajeshi 1,200 wa Ujerumani pia watapelekwa Syria. 

Von der Leyen amesema lengo la kuwepo kwa wanajeshi hao watakaopelekwa mwezi Januari, ni kupambana na kukabiliana na IS, na kuwazuia wanamgambo kufanya mashambulizi mengine ya kigaidi. 

Bunge la Ujerumani leo linatarajiwa kuidhinisha kupelekwa wanajeshi hao nchini Syria kupambana na IS.

dwswahili


Washington

Shirika la Upelelezi la Marekani-FBI, linachunguza iwapo shambulizi la California lina uhusiano wowote na vitendo vya kigaidi. 

Siku ya Jumatano, watu 14 waliuawa kwa kupigwa risasi na watu wawili waliokuwa na silaha nzito katika sherehe za Krismasi zilizofanyika kwenye kituo cha kuwahudumia watu wenye ulemavu kilichoko San Bernardino. 

Maafisa wa kijasusi wameripoti kuwa watu hao walikuwa wakifanya mawasiliano na wanamgambo wenye itikadi kali za Kiislamu kupitia kwenye mtandao wa mawasiliano ya kijamii. 

Polisi wamesema washambuliaji hao walikuwa na risasi za kutosha na mabomu ya kuwaua mamia ya watu wakati walipofanya shambulizi hilo. 

Tangu kutokea kwa shambulizi hilo, polisi wamepata mabomu na silaha nyingine katika nyumba ya washambuliaji. 

Kutokana na shambulizi hilo, Rais Barack Obama wa Marekani kwa mara nyingine tena amewatolea wito Wamarekani kupitia upya sheria za kudhibiti matumizi ya bunduki.

Dwswahili



Nairobi

Serikali itapoteza jumla ya shilingi bilioni 60 zinazotokana na maua mboga na matunda yanayozwa katika mataifa ya kingeni, baada ya mataifa ya Uropa kuanza kutekeleza sheria mpya kuhusu bidhaa zinazouzwa nchini humo. 

Mataifa ya Uropa ambayo ni moja wapo ya soko kuu la maua na matunda kutoka humu nchini yamepiga marufuku utumizi wa baadhi ya kemikali zinazotumiwa humu nchini katika upanzi wa maua hali inayosababisha bidhaa hizo kukosa soko katika mataifa ya kigeni. 

Meneja wa muungano wa wauzaji wa mboga maua na matunda Francis Wario ameishauri serikali kuwaelimisha wakulima wa bidhaa hizo kuhusu kemikali zilizoidhinishwa ili kuzuia bidhaa zinazotoka humu nchini kupigwa marufuku Uropa.

Cri

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / HIZI HAPA HABARI ZA KIMATAIFA KWA MUDA HUU DECEMBER 04/2015

unaweza kupata habari zote hapa za kimataifa kupitia kazenzele1.blogspot.com au kupitia page ya denis kazenzele au omwatani hizi ni fb.




South Africa

Rais wa Uchina Xi Jinping amesema taifa lake litatoa ufadhili wa dola bilioni 60 kwa nchi za Afrika.

Tangazo hilo amelitoa kwenye mkutano mkuu wa ushirikiano kati ya Uchina na nchi za bara Afrika, ambao umeanza leo jijini Johannesburg. Viongozi kadha wa mataifa ya Afrika wanahudhuria.

Tangazo la fedha hizo za mabilioni ya dola ambazo zitatolewa kupitia ruzuku, mikopo na ufadhili wa miradi ya maendeleo lilisubiriwa, lakini kiasi cha fedha kilichoahidiwa kimezidi matarajio.

Sehemu kubwa ya usaidizi huu wa kifedha sana utatolewa kupitia miradi ya miundo mbinu, kusaidia kusisimua ukuaji wa kiuchumi, lakini maelezo zaidi hayajatolewa.

Kiongozi mwenza wa mkutano huo Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amesifu ushirikiano kati ya Uchina na nchi za Afrika.

Amesema watu wanaoishi Uchina na Afrika ni theluthi moja ya watu wote duniani, na kwamba hilo ni soko kubwa la bidhaa.

Uchina, nchi yenye uchumi wa pili kwa ukubwa duniani, imetoa msururu wa mikopo kwa nchi za Afrika, ambazo nazo huuzia taifa hilo mafuta na bidhaa nyingine muhimu.
Hata hivyo, idadi ya bidhaa ambazo mataifa hayo huuzia Uchina imekuwa ikipungua.

Uwekezaji wa Uchina Afrika ulishuka asilimia 40 nusu ya kwanza ya mwaka huu, kwa mujibu wa wizara ya uchumi ya Uchina.

Ziara ya Bw Xi barani Afrika imetazamwa na wengi kama hatua ya kuyahakikishia mataifa ya Afrika kwamba Uchina itaendelea kuwekeza katika bara hilo licha ya kupungua kasi kwa ukuaji wa uchumi wa Uchina.

Mapema wiki hii Uchina na Afrika Kusini zilitia saini mikataba na mikopo ya thamani ya $6.5bn (£4.3bn), inayoangazia zaidi miundo mbinu.

Jumla ya mikataba 26 ilitiwa saini Jumatano, $2.5bn zikienda kwa shirika la reli la serikali.

Kabla ya kutua Afrika Kusini, Bw Xi alizuru Zimbabwe Jumanne, ambako pia aliahidi taifa hilo mikopo ya kusaidia kuinua uchumi wake uliodorora.

Bbcswahili


Cairo
 
Watu 16 wameuawa katika mji mkuu wa Mirsi, Cairo, baada ya bomu kulipuliwa kwenye mgahawa mmoja, ripoti zinasema.

Shambulio hilo limetokea katika eneo la Agouza, katikati mwa jiji hilo.

Gazeti la The Cairo Post linasema watu watatu waliokuwa wamejifunika nyuso zao walirusha bomu mgahawani na kisha kutoroka.

Shirika la habari la Reuters limemnukuu afisa mmoja wa usalama, ambaye hakutajwa jina lake, akisema mmoja wa washukiwa ni mfanyakazi wa zamani wa mgahawa huo.

Mgawaha huo ulikuwa ghorofa ya chini ya ardhi kwenye jengo hilo, jambo lililoifanya vigumu kwa watu kutoroka.

Wahasiriwa walifariki kutokana na majeraha ya moto au kwa kutokana na moshi. Watu watano wamejeruhiwa.

Mji wa Cairo umeshambuliwa mara kadha na watu wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa Kiislamu.

Juhudi za wanamgambo hao wa Kiislamu zilizidi baada ya kung’olewa mamlakani kwa Rais Mohammed Morsi mwaka 2013.

Bbcswahili


Bangkok
Polisi nchini Thailand wanachunguza ripoti kuwa wanamgambo kumi kutoka kundi la wapiganaji wa Islamic state wameingia nchini humo na wanapanga kushambulia sehemu zinazomilikiwa na Urusi.

Shirika la habari nchini urusi la FSB linaamini kuwa kundi hilo limesafiri kutoka nchini Syria.

Sita kati yao wanaripotiwa kuelekea maeneo ya kifahari ya Pattaya na Phuket huku wengine wakiwa hawajulikani waliko.

Polisi nchini Thailand wanasema kwa hawajafanikiwa kuthibitisha uwepo wa raia hao wa Syria. Zaidi ya watu milioni moja unusu raia wa Urusi walizuru Thailand mwaka 2013.

Bbcswahili


Washington

Waziri wa Ulinzi wa Marekani Ash Carter ametangaza kuwa nafasi zote za kazi za kijeshi za kivita sasa zitakuwa wazi pia kwa wanawake wa Marekani.

Carter amesema huduma za kijeshi za Marekani hazitaweza tena kupunguza nusu ya watu wenye ujuzi na vipaji.

Amesema wanawake sasa wanaweza kuendesha magari ya deraya, mizinga na kuongoza askari wa nchi kavu kwenye mapambano.

Mpango huo wa kiistoria unakwenda kinyume na hoja ya mwenyekiti wa Umoja wa Wakuu wa majeshi kwamba Kikosi cha askari wa majini wanaweza kuruhusiwa kuwatenga wanawake katika baadhi ya majukumu kwenye mapambano ya mstari mbele vitani.

Bbcswahili


berlin

Jeshi la Ujerumani linatarajiwa kupeleka ndege sita za upelelezi nchini Syria, kama sehemu ya muungano wa kimataifa katika mapambano dhidi ya kundi lenye itikadi kali la Dola la Kiislamu-IS. 

Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani, Ursula von der Leyen, amethibitisha kuwa ndege za kujaza mafuta pia zitapelekwa nchini humo, pamoja na manowari moja ya kuilinda manowari inayobeba ndege za kijeshi za Ufaransa. 

Amesema mashambulizi ya anga na majeshi ya ardhini, ulikuwa mkakati imara katika mapambano dhidi ya IS. 

Aidha, wanajeshi 1,200 wa Ujerumani pia watapelekwa Syria. 

Von der Leyen amesema lengo la kuwepo kwa wanajeshi hao watakaopelekwa mwezi Januari, ni kupambana na kukabiliana na IS, na kuwazuia wanamgambo kufanya mashambulizi mengine ya kigaidi. 

Bunge la Ujerumani leo linatarajiwa kuidhinisha kupelekwa wanajeshi hao nchini Syria kupambana na IS.

dwswahili


Washington

Shirika la Upelelezi la Marekani-FBI, linachunguza iwapo shambulizi la California lina uhusiano wowote na vitendo vya kigaidi. 

Siku ya Jumatano, watu 14 waliuawa kwa kupigwa risasi na watu wawili waliokuwa na silaha nzito katika sherehe za Krismasi zilizofanyika kwenye kituo cha kuwahudumia watu wenye ulemavu kilichoko San Bernardino. 

Maafisa wa kijasusi wameripoti kuwa watu hao walikuwa wakifanya mawasiliano na wanamgambo wenye itikadi kali za Kiislamu kupitia kwenye mtandao wa mawasiliano ya kijamii. 

Polisi wamesema washambuliaji hao walikuwa na risasi za kutosha na mabomu ya kuwaua mamia ya watu wakati walipofanya shambulizi hilo. 

Tangu kutokea kwa shambulizi hilo, polisi wamepata mabomu na silaha nyingine katika nyumba ya washambuliaji. 

Kutokana na shambulizi hilo, Rais Barack Obama wa Marekani kwa mara nyingine tena amewatolea wito Wamarekani kupitia upya sheria za kudhibiti matumizi ya bunduki.

Dwswahili



Nairobi

Serikali itapoteza jumla ya shilingi bilioni 60 zinazotokana na maua mboga na matunda yanayozwa katika mataifa ya kingeni, baada ya mataifa ya Uropa kuanza kutekeleza sheria mpya kuhusu bidhaa zinazouzwa nchini humo. 

Mataifa ya Uropa ambayo ni moja wapo ya soko kuu la maua na matunda kutoka humu nchini yamepiga marufuku utumizi wa baadhi ya kemikali zinazotumiwa humu nchini katika upanzi wa maua hali inayosababisha bidhaa hizo kukosa soko katika mataifa ya kigeni. 

Meneja wa muungano wa wauzaji wa mboga maua na matunda Francis Wario ameishauri serikali kuwaelimisha wakulima wa bidhaa hizo kuhusu kemikali zilizoidhinishwa ili kuzuia bidhaa zinazotoka humu nchini kupigwa marufuku Uropa.

Cri


«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :