Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » CHAMA CHA ANGELA MERKEL CHASHINDWA
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Chama cha Chansela wa Ujerumani Angela Merkel kimeshindwa katika uchaguzi wa majimbo, matokeo ya utafiti wa baada ya uchaguzi yanaonesha.
Matokeo hayo yanaonesha chama cha Christian Democrats kimeshindwa katika majimbo ya Baden-Wuerttemberg naRhineland Palatinate, lakini bado kimeendelea kutawala Saxony-Anhalt.
Chama cha AfD kinachowapinga wahamiaji, kimeimarika pakubwa katika majimbo yote matatu.
Uchaguzi huo ulitazamwa na wengi kama kigezo cha uungwaji mkono wa sera ya Chansela Merkel ya kuwapokea wakimbizi.
Zaidi ya wakimbizi na wahamiaji milioni moja waliingia Ujerumani mwaka 2015.
Naibu Chansela wa Ujerumani alisema Jumamosi kwamba kuimarika kwa AfD hakutabadili sera za serikali yake kuhusu uhamiaji.
“Huu ni msimamo wazi ambao tutaendelea kuutetea, wa kutetea utu na ubinadamu. Hatutabadili msimamo wetu sasa.”
Lakini mjini Berlin Jumamosi, karibu waandamanaji 2,000 wa mrengo wa kulia walibeba bendera za Ujerumani na kuimba "Merkel sharti aondoke!" na "Sisi ndio watu!"
Pigo hilo kwa Chansela Merkel limetokea siku chache kabla ya mkutano mkuu wa Umoja wa Ulaya wa kukamilisha mkataba kati ya EU na Uturuki wa kudhibiti kuingia kwa wahamiaji na wakimbizi.
Mkataba huo, ambao utapelekea wahamiaji wanaowasili nchini Ugiriki wakirejeshwa Uturuki, unakabiliwa na changamoto za kisheria na kisiasa.
Wanasheria wanajizatiti kutafuta mpango ambao utatimiza masharti ya kimataifa kuhusu wakimbizi.
Umoja wa Mataifa na makundi ya kutetea haki za kibinadamu wametaja mpango huo kuwa usiofuata maadili na haramu.

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / CHAMA CHA ANGELA MERKEL CHASHINDWA

Chama cha Chansela wa Ujerumani Angela Merkel kimeshindwa katika uchaguzi wa majimbo, matokeo ya utafiti wa baada ya uchaguzi yanaonesha.
Matokeo hayo yanaonesha chama cha Christian Democrats kimeshindwa katika majimbo ya Baden-Wuerttemberg naRhineland Palatinate, lakini bado kimeendelea kutawala Saxony-Anhalt.
Chama cha AfD kinachowapinga wahamiaji, kimeimarika pakubwa katika majimbo yote matatu.
Uchaguzi huo ulitazamwa na wengi kama kigezo cha uungwaji mkono wa sera ya Chansela Merkel ya kuwapokea wakimbizi.
Zaidi ya wakimbizi na wahamiaji milioni moja waliingia Ujerumani mwaka 2015.
Naibu Chansela wa Ujerumani alisema Jumamosi kwamba kuimarika kwa AfD hakutabadili sera za serikali yake kuhusu uhamiaji.
“Huu ni msimamo wazi ambao tutaendelea kuutetea, wa kutetea utu na ubinadamu. Hatutabadili msimamo wetu sasa.”
Lakini mjini Berlin Jumamosi, karibu waandamanaji 2,000 wa mrengo wa kulia walibeba bendera za Ujerumani na kuimba "Merkel sharti aondoke!" na "Sisi ndio watu!"
Pigo hilo kwa Chansela Merkel limetokea siku chache kabla ya mkutano mkuu wa Umoja wa Ulaya wa kukamilisha mkataba kati ya EU na Uturuki wa kudhibiti kuingia kwa wahamiaji na wakimbizi.
Mkataba huo, ambao utapelekea wahamiaji wanaowasili nchini Ugiriki wakirejeshwa Uturuki, unakabiliwa na changamoto za kisheria na kisiasa.
Wanasheria wanajizatiti kutafuta mpango ambao utatimiza masharti ya kimataifa kuhusu wakimbizi.
Umoja wa Mataifa na makundi ya kutetea haki za kibinadamu wametaja mpango huo kuwa usiofuata maadili na haramu.

«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :