Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » RAIS JOHN POMBE MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA MKUU WA MKOA PWANI
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo, kufuatia vifo vya wafanyakazi sita wa halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, vilivyosababishwa na ajali ya barabarani, iliyotokea leo tarehe 21 Machi, 2016 katika eneo la Kerege Wilayani humo. 

Ajali hiyo imetokea majira ya saa tano za asubuhi, baada ya Lori la kubebea mchanga kuyagonga magari mawili ya Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo ambayo yalikuwa katika Msafara wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na serikali za mitaa, iliyokuwa akitoka kukagua mradi wa Maji wa Mapinga. 

Katika salamu hizo Rais Magufuli amesema amepokea kwa mshituko mkubwa taarifa za vifo vya wafanyakazi hao wa halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, ambao wamepoteza maisha wakiwa wanatekeleza majukumu ya kikazi. 

“Kupitia kwako Mkuu wa Mkoa wa Pwani naomba kutoa pole nyingi kwa familia za marehemu wote, ndugu, jamaa, marafiki na wote walioguswa na vifo hivyo, naomba Mwenyezi Mungu awape moyo wa subira, uvumilivu na ustahimilivu kutokana na kuondokewa na wapendwa wao” Amesema Rais Magufuli. 

Dkt. Magufuli amewaombea marehemu wote wapumzishwe mahali pema peponi. Amina 

Aidha, Rais Magufuli amewapa pole wafanyakazi wengine wanane ambao wameumia katika ajali hiyo, na amewaombea wapone haraka. 


Gerson Msigwa 
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU 
Dar es salaam 
21 Machi, 2016

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / RAIS JOHN POMBE MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA MKUU WA MKOA PWANI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo, kufuatia vifo vya wafanyakazi sita wa halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, vilivyosababishwa na ajali ya barabarani, iliyotokea leo tarehe 21 Machi, 2016 katika eneo la Kerege Wilayani humo. 

Ajali hiyo imetokea majira ya saa tano za asubuhi, baada ya Lori la kubebea mchanga kuyagonga magari mawili ya Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo ambayo yalikuwa katika Msafara wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na serikali za mitaa, iliyokuwa akitoka kukagua mradi wa Maji wa Mapinga. 

Katika salamu hizo Rais Magufuli amesema amepokea kwa mshituko mkubwa taarifa za vifo vya wafanyakazi hao wa halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, ambao wamepoteza maisha wakiwa wanatekeleza majukumu ya kikazi. 

“Kupitia kwako Mkuu wa Mkoa wa Pwani naomba kutoa pole nyingi kwa familia za marehemu wote, ndugu, jamaa, marafiki na wote walioguswa na vifo hivyo, naomba Mwenyezi Mungu awape moyo wa subira, uvumilivu na ustahimilivu kutokana na kuondokewa na wapendwa wao” Amesema Rais Magufuli. 

Dkt. Magufuli amewaombea marehemu wote wapumzishwe mahali pema peponi. Amina 

Aidha, Rais Magufuli amewapa pole wafanyakazi wengine wanane ambao wameumia katika ajali hiyo, na amewaombea wapone haraka. 


Gerson Msigwa 
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU 
Dar es salaam 
21 Machi, 2016

«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :