Michuano ya Mpinduzi Cup inazidi kushika kasi hapa visiwani Zanzibar baada ya kushuhudia Simba vs Taifa Jangombe zikikamilisha mchezo wa tatu wa Kundi A.
Simba imeitwanga Taifa Jang’ombe kwa mabao 2-1 katika mechezo wake wa kwanza wa michuano hiyo kwenye Uwanja wa Amaan mjini Zanzibar.
Simba walikuwa wa kwanza kupata bao kupiitia Muzamiru Yassin katika dakika ya 28 ambaye aliuwahi mpira uliotemwa na kipa na kuukwamisha kambani.
Ikionekana kama timu hizo zitaenda mapumziko Simba ikiongoza kwa bao 1-0,Juma Luizio alipachika bao la pili akiwa katikati ya msimu wa mabeki wa Taifa.
Kipindi cha pili kilionekana kina mashambulizi mengi ya kupokezana lakini beki msomi, Noverty Lufunga alifanya yake baada ya kujifunga akiunganisha langoni mwake mpira wa kona.
Michuano hiyo itaendelea tena Leo kwa michezo miwili mchezo wa mapema utakuwa kati ya Zimamoto na Azam Fc majira ya saa kumi jioni na Usiku saa 2:30 Mabingwa watetezi wa Vodacom Tanzania bara timu ya Yanga itashuka dimbani kucheza na Jamhuri ya visiwani Pemba
No comments
Post a Comment