Timu ya Toto African imezinduka Leo na kupata ushindi wa kwanza tangu mzunguko wa pili uanze baada ya kuwatandika wapiga debe ‘Stand United’ jumla ya magoli 2-1 mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara uliochezwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Kipindi cha kwanza kilikuwa cha sare kwa timu zote mbili hadi zinakwenda mapumziko hakuna aliyeweza kuwa mshindi wa mwenzake.
Cha pili kilikuwa kizuri kwa wenyeji Toto kwani waliweza kupata magoli mawili huku Stand United nao wakipata la kufutia machozi hadi mpira unamalizika Toto wameibuka na ushindi wa 2-1 na kuanza mwaka 2017 vizuri na kuanza licha ya kushinda ila bado wapo katika hali ya kushuka daraja.
Kwa Matokeo hayo Toto African wamefikisha jumla ya pointi 16 na kubaki katika nafasi ya 15 ya msimamo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara huku nafasi ya mwisho ikishikwa na wanajeshi timu ya JKT Ruvu wenye pointi 14.
Mechi nyingine ilikuwa kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam timu ya African Lyon imebanwa mbavu na JKT Ruvu baada ya kutoka sare ya bila kufungana 0-0 kwa matokeo Lyon wamefikisha alama 20 wakati JKT Ruvu nao wana alama 14 na kuendelea kuburuza mkia mwa Ligi yenye jumla ya timu 16.
No comments
Post a Comment