John banda Njombe
MAMA
 na wajomba wawili wa Mtoto Peter Mturua wakazi wa Igagala halmashauri 
ya Wanging’ombe, wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa mauaji ya mtoto 
wao huyo kwa kuiba pesa na betri ya solar.
Kamanda
 wa polisi mkoa wa Njombe Wilbrod Mutafungwa amemtaja mama huyo kuwa ni 
Devota Mhagama (38), na wajomba ni Motestu Mwajombe (26), na Wilium 
Msigwa (18) wakazi wa kijiji cha Igagala kata ya Ulembwe wilaya ya 
Wanging’ombe.
Akisimulia
 kisa cha kuuawa Peter amesema kuwa mtoto huyo  aliuwawa  Disemba 23, 
mwaka huu majira ya saa 1:40 usiku, mtoto huyo alituhumiwa kuiba 
shilingi 40,000 na betri ya sola ambayo alikuwa akitumia mama yake 
nyumbani kwao.
Alisema
 kuwa marehemu alipigwa kwa kuchangiwa na Mama, wajomba na kusababisha 
kifo chake baada ya kubaini kuwa pesa zilizo kuwa zimehifadhiwa na mama 
yake na kusema kuwa watuhumiwa watafikishwa mahakamani uchunguzi 
ukikamilika.
Na John Banda
No comments
Post a Comment