Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » HIZI HAPA ZA KIMATAIFA KWA LEO.....................
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post



MARCH 29/TUESDAY
CYPRUS
Mwanamume aliyeteka nyara ndege ya shirika la Misri la EgyptAir na kuishurutisha kutua Cyprus amekamatwa, wizara ya mashauri ya kigeni ya Cyprus imetangaza.
Mwanamume huyo alidai kwamba alikuwa na mkanda wa kujilipua na kumwamuru rubani wa ndege hiyo kuielekeza Cyprus au Uturuki.
Ndege hiyo, iliyokuwa safarini kutoka Alexandria hadi mjini Cairo, mwishowe ilitua uwanja wa Larnaca nchini Cyprus.
Abiria karibu wote walikuwa wamefanikiwa kuondoka kutoka kwenye ndege hiyo.
Ripoti zinasema kuwa mtekaji wa ndege ya EgyptAir anataka kuongea na mkewe walietengana naye anayeishi Cyprus ambaye kwa sasa anadaiwa kuelekea katika uwanja huo wa ndege.
Rais wa Cyprus Nicos Anastasiades amewaambia waandishi wa habari kwamba tukio hilo la utekaji nyara halikuwa la kigaidi.
Akijibu maswali ya waandishi iwapo mtekaji huyo alishinikizwa na mapenzi, alicheka na kusema, ''kila mara kuna mwanamke anayehusishwa''.
Shirika la habari la Cyprus CYBC linasema kuwa mtekaji huyo huenda alikuwa na malengo yake ya kibinafsi, mtekaji huyo alikuwa na mkewe waliyetengana nchini Cyprus.
Walioshuhudia wanasema kuwa mtekaji huyo alirusha barua katika uwanja huo wa ndege ilioandikwa Kiarabu akiomba ipelekwe kwa mwanamke huyo.






UFARANSA
Jeshi la wanamaji wa Ufaransa linalopiga doria kaskazini mwa bahari hindi limekamata silaha kutoka kwa meli moja iliokuwa ikielekea Somalia.
Silaha hizo ni pamoja na mamia ya bunduki pamoja na silaha za kupambana na vifaru.
Hatua hiyo inajiri wiki kadhaa baada ya wanamaji wa Australia kukamata silaha nyingi zilizokuwa zikielekea Somalia.
Meli hiyo ilionekana na ndege za wanamaji wa Ufaransa ambayo ni mojawapo wa vikosi vya kimataifa vinavyopiga doria katika bahari Hindi.
Vikosi hivyo vya Ufaransa vilikamata silaha hizo chini ya vikwazo vya Umoja wa Mataifa kuzuia silaha kutowafikia wapiganaji wa wa al-shabab.
Muungano huo wa wanamaji umepongeza kukamatwa kwa silaha hizo kama mafanikio makubwa ijapokuwa haujatoa habari zozote kuhusu wale wanaosafirisha silaha hizo.


ITALIA
Wenyeji wa mji mmoja mdogo nchini Italia wamekuwa wakisheherekea kuzaliwa kwa mtoto wa kwanza mjini humo tangu miaka ya 80.
Meya wa mji wa Ostana, ulioko Kaskazini mwa Italia ambayo iko katika maeneo ya milima ya Piedmont aliwaongoza wenyeji kusherehekea ndoto yao kukamilika kwa kuzaliwa kwa kizazi kipya.
Ostana imeshudia kupungua kwa idadi ya wenyeji wake katika karne iliyopita kwa hivyo kuzaliwa kwa ''Pablo'' katika hospitalini moja ya Turin imeongezea idadi ya wenyeji kufikia 85.
Jarida la La Stampa linasema japo wanasheherekea sio wote wanaoishi mjini humo.

Meya Giacomo Lombardo anasema kuwa miaka ya nyuma Ostana ilikuwa na wenyeji 1,000 lakini idadi hiyo ya watu imekuwa ikipungua kila kukicha hadi kufikia 85 sasa.
''Mara ya mwisho mtoto kuzaliwa hapo ni mwaka 1987''
 amesema Kati ya mwaka wa 1975 -1976 watoto 17 walizaliwa katika mji huo.
Kwa sasa wenyeji wa mji huo wa Ostana wameanza kuweka mikakati ya kuimarisha idadi ya watoto wanaozaliwa kwa kuunda nafasi mpya za kazi.
Wazazi wa Pablo, Silvia na Jose walikuwa wamepanga kuondoka Italia kabla ya wenyeji kuwapa nafasi ya kuwa meneja wa uhifadhi wa misitu Ostana.
Kwa sasa wanapiga msasa sheria itakayowaruhusu wenyeji wasilipe kodi mbali na kutoa nyumba za bure kwa wenyeji wanaotafuta kazi.



SOMALIA
Jeshi la wanamaji wa Ufaransa linalopiga doria kaskazini mwa bahari hindi limekamata silaha kutoka kwa meli moja iliokuwa ikielekea Somalia.
Silaha hizo ni pamoja na mamia ya bunduki pamoja na silaha za kupambana na vifaru.
Hatua hiyo inajiri wiki kadhaa baada ya wanamaji wa Australia kukamata silaha nyingi zilizokuwa zikielekea Somalia.
Meli hiyo ilionekana na ndege za wanamaji wa Ufaransa ambayo ni mojawapo wa vikosi vya kimataifa vinavyopiga doria katika bahari Hindi.
Vikosi hivyo vya Ufaransa vilikamata silaha hizo chini ya vikwazo vya Umoja wa Mataifa kuzuia silaha kutowafikia wapiganaji wa wa al-shabab.

Muungano huo wa wanamaji umepongeza kukamatwa kwa silaha hizo kama mafanikio makubwa ijapokuwa haujatoa habari zozote kuhusu wale wanaosafirisha silaha hizo.



NIGER

Wapinzani nchini Niger wametangaza azma yao kwa ajili ya kufanya mazungumzo na Rais Mahamadou Issoufou wa nchi hiyo.

Chama kikuu cha upinzani ambacho pia kimetangaza kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu uliopita nchini humo, kimeyasema hayo baada ya kukutana na Brigi Rafini, Waziri Mkuu wa nchi hiyo.

Katika taarifa yake, chama hicho kinachoongozwa na Hama Amadou, kimetangaza utayarifu wake kwa ajili ya kuzungumza na rais huyo aliyeibuka mshindi katika uchaguzi huo.

Aidha chama hicho kimetaka mazungumzo hayo yawe ya kweli na jadi kwa ajili ya kumaliza mgogoro wa kisiasa ambao unaendelea nchini Niger tangu kujiri uchaguzi mkuu uliopita.

Rais Mahamadou Issoufou aliibuka mshindi baada ya kupata asilimia 94/92 ya kura katika uchaguzi wa duru ya pili uliofanyika tarehe 20 mwezi Machi mwaka huu.

Chama kikuu hicho cha upinzani kiliutaja uchaguzi huo kuwa wa kimaonyesho suala ambalo lilisababisha chama hicho kuususia.






About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / HIZI HAPA ZA KIMATAIFA KWA LEO.....................



MARCH 29/TUESDAY
CYPRUS
Mwanamume aliyeteka nyara ndege ya shirika la Misri la EgyptAir na kuishurutisha kutua Cyprus amekamatwa, wizara ya mashauri ya kigeni ya Cyprus imetangaza.
Mwanamume huyo alidai kwamba alikuwa na mkanda wa kujilipua na kumwamuru rubani wa ndege hiyo kuielekeza Cyprus au Uturuki.
Ndege hiyo, iliyokuwa safarini kutoka Alexandria hadi mjini Cairo, mwishowe ilitua uwanja wa Larnaca nchini Cyprus.
Abiria karibu wote walikuwa wamefanikiwa kuondoka kutoka kwenye ndege hiyo.
Ripoti zinasema kuwa mtekaji wa ndege ya EgyptAir anataka kuongea na mkewe walietengana naye anayeishi Cyprus ambaye kwa sasa anadaiwa kuelekea katika uwanja huo wa ndege.
Rais wa Cyprus Nicos Anastasiades amewaambia waandishi wa habari kwamba tukio hilo la utekaji nyara halikuwa la kigaidi.
Akijibu maswali ya waandishi iwapo mtekaji huyo alishinikizwa na mapenzi, alicheka na kusema, ''kila mara kuna mwanamke anayehusishwa''.
Shirika la habari la Cyprus CYBC linasema kuwa mtekaji huyo huenda alikuwa na malengo yake ya kibinafsi, mtekaji huyo alikuwa na mkewe waliyetengana nchini Cyprus.
Walioshuhudia wanasema kuwa mtekaji huyo alirusha barua katika uwanja huo wa ndege ilioandikwa Kiarabu akiomba ipelekwe kwa mwanamke huyo.






UFARANSA
Jeshi la wanamaji wa Ufaransa linalopiga doria kaskazini mwa bahari hindi limekamata silaha kutoka kwa meli moja iliokuwa ikielekea Somalia.
Silaha hizo ni pamoja na mamia ya bunduki pamoja na silaha za kupambana na vifaru.
Hatua hiyo inajiri wiki kadhaa baada ya wanamaji wa Australia kukamata silaha nyingi zilizokuwa zikielekea Somalia.
Meli hiyo ilionekana na ndege za wanamaji wa Ufaransa ambayo ni mojawapo wa vikosi vya kimataifa vinavyopiga doria katika bahari Hindi.
Vikosi hivyo vya Ufaransa vilikamata silaha hizo chini ya vikwazo vya Umoja wa Mataifa kuzuia silaha kutowafikia wapiganaji wa wa al-shabab.
Muungano huo wa wanamaji umepongeza kukamatwa kwa silaha hizo kama mafanikio makubwa ijapokuwa haujatoa habari zozote kuhusu wale wanaosafirisha silaha hizo.


ITALIA
Wenyeji wa mji mmoja mdogo nchini Italia wamekuwa wakisheherekea kuzaliwa kwa mtoto wa kwanza mjini humo tangu miaka ya 80.
Meya wa mji wa Ostana, ulioko Kaskazini mwa Italia ambayo iko katika maeneo ya milima ya Piedmont aliwaongoza wenyeji kusherehekea ndoto yao kukamilika kwa kuzaliwa kwa kizazi kipya.
Ostana imeshudia kupungua kwa idadi ya wenyeji wake katika karne iliyopita kwa hivyo kuzaliwa kwa ''Pablo'' katika hospitalini moja ya Turin imeongezea idadi ya wenyeji kufikia 85.
Jarida la La Stampa linasema japo wanasheherekea sio wote wanaoishi mjini humo.

Meya Giacomo Lombardo anasema kuwa miaka ya nyuma Ostana ilikuwa na wenyeji 1,000 lakini idadi hiyo ya watu imekuwa ikipungua kila kukicha hadi kufikia 85 sasa.
''Mara ya mwisho mtoto kuzaliwa hapo ni mwaka 1987''
 amesema Kati ya mwaka wa 1975 -1976 watoto 17 walizaliwa katika mji huo.
Kwa sasa wenyeji wa mji huo wa Ostana wameanza kuweka mikakati ya kuimarisha idadi ya watoto wanaozaliwa kwa kuunda nafasi mpya za kazi.
Wazazi wa Pablo, Silvia na Jose walikuwa wamepanga kuondoka Italia kabla ya wenyeji kuwapa nafasi ya kuwa meneja wa uhifadhi wa misitu Ostana.
Kwa sasa wanapiga msasa sheria itakayowaruhusu wenyeji wasilipe kodi mbali na kutoa nyumba za bure kwa wenyeji wanaotafuta kazi.



SOMALIA
Jeshi la wanamaji wa Ufaransa linalopiga doria kaskazini mwa bahari hindi limekamata silaha kutoka kwa meli moja iliokuwa ikielekea Somalia.
Silaha hizo ni pamoja na mamia ya bunduki pamoja na silaha za kupambana na vifaru.
Hatua hiyo inajiri wiki kadhaa baada ya wanamaji wa Australia kukamata silaha nyingi zilizokuwa zikielekea Somalia.
Meli hiyo ilionekana na ndege za wanamaji wa Ufaransa ambayo ni mojawapo wa vikosi vya kimataifa vinavyopiga doria katika bahari Hindi.
Vikosi hivyo vya Ufaransa vilikamata silaha hizo chini ya vikwazo vya Umoja wa Mataifa kuzuia silaha kutowafikia wapiganaji wa wa al-shabab.

Muungano huo wa wanamaji umepongeza kukamatwa kwa silaha hizo kama mafanikio makubwa ijapokuwa haujatoa habari zozote kuhusu wale wanaosafirisha silaha hizo.



NIGER

Wapinzani nchini Niger wametangaza azma yao kwa ajili ya kufanya mazungumzo na Rais Mahamadou Issoufou wa nchi hiyo.

Chama kikuu cha upinzani ambacho pia kimetangaza kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu uliopita nchini humo, kimeyasema hayo baada ya kukutana na Brigi Rafini, Waziri Mkuu wa nchi hiyo.

Katika taarifa yake, chama hicho kinachoongozwa na Hama Amadou, kimetangaza utayarifu wake kwa ajili ya kuzungumza na rais huyo aliyeibuka mshindi katika uchaguzi huo.

Aidha chama hicho kimetaka mazungumzo hayo yawe ya kweli na jadi kwa ajili ya kumaliza mgogoro wa kisiasa ambao unaendelea nchini Niger tangu kujiri uchaguzi mkuu uliopita.

Rais Mahamadou Issoufou aliibuka mshindi baada ya kupata asilimia 94/92 ya kura katika uchaguzi wa duru ya pili uliofanyika tarehe 20 mwezi Machi mwaka huu.

Chama kikuu hicho cha upinzani kiliutaja uchaguzi huo kuwa wa kimaonyesho suala ambalo lilisababisha chama hicho kuususia.







«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :