Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » SALL ASEMA PESA ZA EU HAZIITOSHI AFRIKA
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Rais wa Senegal Macky Sall amesema hazina ya $1.9bn (£1.2bn) iliyoundwa na mataifa ya Ulaya ni hatua nzuri lakini akasema pesa hizo hazitoshi.

Hazina hiyo ni moja ya hatua zilizoafikiwa kati ya viongozi wa Ulaya na Afrika kukabiliana na tatizo la wahamiaji ambao wamekuwa wakielekea Ulaya.

Viongozi hao wamesema lengo lao ni kukabiliana na mizizi ya tatizo la wahamiaji.

Mkutano huo uliitishwa baada ya wahamiaji 800 kufa maji meli yao ilipozama baharini baada ya kuondoka Libya.

Rais Sall, ambaye kwa sasa anaongoza muungano wa mataifa ya Afrika Magharibi, aliambia wanahabari pembezoni mwa mkutano huo kwamba pesa hizo zilizoahidiwa “hazitoshi bara lote la Afrika”.

Lakini baadaye, akizungumza katika kikao na wanahabari alisema amefurahishwa na hazina hiyo, lakini akasema angependa kuona pesa zaidi zikitolewa.

Rais wa Niger Mahamadou Issoufou alikariri matamshi ya kiongozi huyo wa Senegal na akaongeza kuwa uongozi wa ulimwengu unafaa kufanyiwa mageuzi, na biashara duniani ifanywe kuwa ya haki zaidi.

Rais wa Baraza la EU Donald Tusk amesema mkutano huo uliofanyika Malta umekubalia kuhusu “orodha ndefu ya hatua zitakazotekelezwa kufikia mwisho wa 2016”.

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / SALL ASEMA PESA ZA EU HAZIITOSHI AFRIKA

Rais wa Senegal Macky Sall amesema hazina ya $1.9bn (£1.2bn) iliyoundwa na mataifa ya Ulaya ni hatua nzuri lakini akasema pesa hizo hazitoshi.

Hazina hiyo ni moja ya hatua zilizoafikiwa kati ya viongozi wa Ulaya na Afrika kukabiliana na tatizo la wahamiaji ambao wamekuwa wakielekea Ulaya.

Viongozi hao wamesema lengo lao ni kukabiliana na mizizi ya tatizo la wahamiaji.

Mkutano huo uliitishwa baada ya wahamiaji 800 kufa maji meli yao ilipozama baharini baada ya kuondoka Libya.

Rais Sall, ambaye kwa sasa anaongoza muungano wa mataifa ya Afrika Magharibi, aliambia wanahabari pembezoni mwa mkutano huo kwamba pesa hizo zilizoahidiwa “hazitoshi bara lote la Afrika”.

Lakini baadaye, akizungumza katika kikao na wanahabari alisema amefurahishwa na hazina hiyo, lakini akasema angependa kuona pesa zaidi zikitolewa.

Rais wa Niger Mahamadou Issoufou alikariri matamshi ya kiongozi huyo wa Senegal na akaongeza kuwa uongozi wa ulimwengu unafaa kufanyiwa mageuzi, na biashara duniani ifanywe kuwa ya haki zaidi.

Rais wa Baraza la EU Donald Tusk amesema mkutano huo uliofanyika Malta umekubalia kuhusu “orodha ndefu ya hatua zitakazotekelezwa kufikia mwisho wa 2016”.


«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :