Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » ELIMU BURE IMEMPOKONYA ULAJI MKURUGENZI MANISPAA YA DODOMA, HILI NALO LIMETOKA SASA LIMEBAKI MOJA DODOMA
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tamisemi George Simbachawene akishuka kwenye gari mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika shule ya msingi Dodoma Makulu, alipogundua madudu yaliyomfuta kazi Mkurugenzi wa Manispaa Agostino Kalinga
Na John Banda, Dodoma
WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI)George Simbachawene amemvua cheo cha Ukurugenzi Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Agustino Kalinga kwa kushindwa kuwasimia watumishi waliopo chini yake.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI George Simbachawene akisoma Barua aliyopewa mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi ya Dodoma Janeth Justine kwa ajili ya kuchangisha michango ya uendeshaji wa shule kwa wazazi, alipofanya ziara ya kushtukiza January 22,2016 IMETENGENEZWA NA BANDA BLOG
Pia Waziri huyo amemsimamisha kazi Ofisa elimu  vifaa na takwimu msingi wa manispaa hiyo Josephine Akimu kwa kosa la kudharau maelekezo ya kiongozi wake kwa kusaini barua kwa niaba ya Mkurugenzi huku akitumia jina la Afisa elimu wake bila ridhaa yake.

Hatua hiyo ilitangazwa jana mjini hapa na Waziri Simbachawene wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Waziri huyo alisema kuwa kutokana na kubainika kwa kasoro katika Shule ya msingi Dodoma Makulu ya kuandikwa kwa barua toka ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ikielekeza uchangishwaji fedha kwa wazazi wa michango ya maji,umeme na mlinzi michango ambayo ilishafutwa na Serikali.

“Mkurugenzi huyu wa Manispaa ya Dodoma Kalinga ameshindwa kuwasimamia watumishi walio chini yake hadi kusababisha kuandikwa na kusambazwa barua kwa walimu wakuu wa shule za msingi Manispaa ya Dodoma ambayo inatofautiana na maelekezo ya serikali yaliyopo kwenye mwongozo,”alisema

Pia alisisitiza kuwa Mkurugenzi huyo  ameshindwa kusimamia utekelezaji wa maelekezo sahihi ya serikali kuhusu utoaji wa elimu msingi bila malipo hivyo namvua cheo hicho ili hatua nyingine ziweze kuchukuliwa .

Aidha Waziri huyo amempa onyo  Ofisa wa elimu msingi wa Manispaa ya Dodoma  Scola Kapinga kwa kosa la kutokuwa makini na idara yake hadi kusababisha barua hiyo kuandikwa na kupelekwa shuleni bila yeye kuwa na taarifa.

“Nawaagiza wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa mamlaka za Serikali za mitaa kuendelea kuwaelimisha wakuu wa shule za msingi na sekondari katika maeneo yao kuhusu utoaji wa elimu bure bila malipo.

Wiki iliyopita Waziri  George Simbachawene akiambatana na  Naibu katibu mkuu Tamisemi elimu,Bernard Makali alifanya ziara ya kushtukiza katika  Shule ya msingi Dodoma Makulu kujionea hali halisi ya mgawanyo wa fedha za elimu bure na kubaini barua toka Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma iliyoandikwa na Ofisa elimu msingi kuelekeza  michango ya  fedha za maji,umeme na mlinzi kwa wazazi.

Imeandaliwa na John Banda
Imehaririwa na Denice J. Kazenzele
January 25/2016

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / ELIMU BURE IMEMPOKONYA ULAJI MKURUGENZI MANISPAA YA DODOMA, HILI NALO LIMETOKA SASA LIMEBAKI MOJA DODOMA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tamisemi George Simbachawene akishuka kwenye gari mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika shule ya msingi Dodoma Makulu, alipogundua madudu yaliyomfuta kazi Mkurugenzi wa Manispaa Agostino Kalinga
Na John Banda, Dodoma
WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI)George Simbachawene amemvua cheo cha Ukurugenzi Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Agustino Kalinga kwa kushindwa kuwasimia watumishi waliopo chini yake.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI George Simbachawene akisoma Barua aliyopewa mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi ya Dodoma Janeth Justine kwa ajili ya kuchangisha michango ya uendeshaji wa shule kwa wazazi, alipofanya ziara ya kushtukiza January 22,2016 IMETENGENEZWA NA BANDA BLOG
Pia Waziri huyo amemsimamisha kazi Ofisa elimu  vifaa na takwimu msingi wa manispaa hiyo Josephine Akimu kwa kosa la kudharau maelekezo ya kiongozi wake kwa kusaini barua kwa niaba ya Mkurugenzi huku akitumia jina la Afisa elimu wake bila ridhaa yake.

Hatua hiyo ilitangazwa jana mjini hapa na Waziri Simbachawene wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Waziri huyo alisema kuwa kutokana na kubainika kwa kasoro katika Shule ya msingi Dodoma Makulu ya kuandikwa kwa barua toka ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ikielekeza uchangishwaji fedha kwa wazazi wa michango ya maji,umeme na mlinzi michango ambayo ilishafutwa na Serikali.

“Mkurugenzi huyu wa Manispaa ya Dodoma Kalinga ameshindwa kuwasimamia watumishi walio chini yake hadi kusababisha kuandikwa na kusambazwa barua kwa walimu wakuu wa shule za msingi Manispaa ya Dodoma ambayo inatofautiana na maelekezo ya serikali yaliyopo kwenye mwongozo,”alisema

Pia alisisitiza kuwa Mkurugenzi huyo  ameshindwa kusimamia utekelezaji wa maelekezo sahihi ya serikali kuhusu utoaji wa elimu msingi bila malipo hivyo namvua cheo hicho ili hatua nyingine ziweze kuchukuliwa .

Aidha Waziri huyo amempa onyo  Ofisa wa elimu msingi wa Manispaa ya Dodoma  Scola Kapinga kwa kosa la kutokuwa makini na idara yake hadi kusababisha barua hiyo kuandikwa na kupelekwa shuleni bila yeye kuwa na taarifa.

“Nawaagiza wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa mamlaka za Serikali za mitaa kuendelea kuwaelimisha wakuu wa shule za msingi na sekondari katika maeneo yao kuhusu utoaji wa elimu bure bila malipo.

Wiki iliyopita Waziri  George Simbachawene akiambatana na  Naibu katibu mkuu Tamisemi elimu,Bernard Makali alifanya ziara ya kushtukiza katika  Shule ya msingi Dodoma Makulu kujionea hali halisi ya mgawanyo wa fedha za elimu bure na kubaini barua toka Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma iliyoandikwa na Ofisa elimu msingi kuelekeza  michango ya  fedha za maji,umeme na mlinzi kwa wazazi.

Imeandaliwa na John Banda
Imehaririwa na Denice J. Kazenzele
January 25/2016

«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :