HII YA MBWANA ALLY SAMATA ALIYENYAKUWA TUZO YA MCHEZAJI BORA AFRIKA.
MICHEZO IJUMAA YA WIKI HII NI HESHIMA KWA WATANZANIA LAKINI PIA VIPI KUHUSU MOTISHA?
By Nasri Bakari Januari 10,2016
Ilikuwa ni usiku wa kuamkia ijumaa ya tarehe 8/1/2016 siku ambayo watanzania tangu tupate uhuru hatujawahi kufurahi katika michezo tulipolipuka kwa shangwe na nderemo baada ya kusikia jina la mtanzania Mbwana Ally Samatta likitajwa kuwa ndo mchezaji bora waafrika kwa wachezaji wa ndani waoooh!!!!! Kuanzia hapo kila mtanzania akaona hakuna linaloshindikana chini ya jua.
Mfalme huyo wa soka anayechezea TP Mazembe baada ya kuipeperusha vyema bendera ya Taifa ikulu ya Tanzania nayo imeliona hilo na ikaamua kutuma salamu za pongezi zilizotolewa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa shirikisho la soka tz.
Barua ilisomeaka hivi:
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za pongezi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye kufuatia mchezaji wa timu ya Taifa ya mpira wa miguu Mbwana Ally Samatta Kutwaa tuzo ya ya mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza barani Afrika iliyotolewa katika mji wa Abuja Nigeria jana usiku.
Mhe. Rais Magufuli amemtaka Waziri Nape Nnauye amfikishie salamu zake za pongezi kwa mchezaji huyo ambaye pia ni mchezaji wa kulipwa wa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Amesema tuzo hiyo imemjengea heshima na kuleta sifa kwa Mbwana Samatta mwenyewe,wanasoka hapa nchini na Tanzania kwa ujumla katika medali ya Soka Kimataifa.
Aidha. Rais amewasihi wachezazaji wa Soka wote na wadau wa michezo huo kuongeza juhudi za kuendeleza mchezo huo ili upige hatua zaidi za kimaendeleo.
Imetolewa na;
Gerson Msigwa
Katibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ,IKULU
Dar es Salaam
08 Januari,2016
% lakini swali ni kwamba baada ya salamu hizo ikulu pamoja na walioipokea {TFF} inafanya jitihada gani ili kuhakikisha kina samatta wanapatikana kwa wingi tanzania? maana inawezekana kina samatta wakapatikana tena miaka 80 ijayo kama mipango y atff na serikali haitokuwa vizuri katika kukuza soka la tanzania, kwani umesahau kuwa walikuwepo kina samatta kipindi cha nyuma waliofikia fursa kama ya ulimwengu au mchezaji mwingine aliyecheza nje ya tanzania kwa mafanikio lakini akarejea nyumbani pasipo kuwa na mafanikio makubwa licha ya kukosa usaidizi kutoka mamlaka husika? tusingoje mafanikio yaletwe na mtu binafsi alafu tufurahie kupongeza au kupongezwa ni jambo la hatari na sifa za zima moto.
imehaririwa na denis kazenzele
No comments
Post a Comment