KILICHOIFANYA timu ya CDA “watoto wa Nyumbani” ya Dodoma inayoshiriki ligi Daraja la kwanza kupokwa pointi Tatu kutokana na kumchezesha mchezaji aliyekuwa na kadi tatu za Njano ni kutokana na kutokuwepo mtunza kumbukumbu wa clubu hiyo.
Juzi kamati ya uendeshaji na usimamizi wa ligi kuu iliipa ushindi wa pointi tatu na mabao matatu Polisi Dodoma dhidi ya Mji Mkuu [CDA] iliyomchezesha Peter Ngowi kinyume cha kanuni za 37[4] na 14[37] Desemba 26 kwenye uwanja wa Mgambo Mpwapwa.
Akizungumza mjini humo Afsa habari wa CDA Jaliru Mateleka alisema makosa yaliyofanyika siku hiyo ni kutokuwa na.
kumbukumbu zozote kutokana na mhusika kuwa safarini na hivyo kujikuta wakiitumbukiza timu kwenye kupokwa pointi kwenye mchezo huo waliokuwa wameshinda 2.1.
“makosa yalifanyika na hakuna mtu aliyekuwa anakumbuka ka Ngowi alikuwa na kadi tatu za njano ndiyo maana mwalimu akampanga lakini kama angekuwepo mtunza kumbukumbu wa Club haya yote yasingetokea.
Tumekubali kunyang’anywa pointi kikanuni hatuna jinsi maana hilo ni sawa na maji yaliyomwagika kwa sasa tunaganga yajayo”, alisema
Kwa upande wake Michael Matebene wa Polisi alisema.
wamefurahishwa na kupata pointi 3 za ubwete toka kwa wenzao CDA lakini akaonya kuwa ukiona mwenzako ananyolewa wewe tia maji, hivyo akazitaka Clubu za soka kuwa makini na kanuni za ligi husika ili kuepuka kupokwa pointi.
No comments
Post a Comment