Wakati mvua zinazidi kunyesha kwa kasi hapa nchini, ndivyo maisha wa watu yanavyozidi kuwa magumu,pia miudombinu inaharibika na kujikuta wengi wakikosa mahitaji muhimu ya kijamii.
huko mpunguzi moja kati ya kata zenye shida ya miundombinu hasa ya barabara {daraja}kumetokea hasara kwa mara ya pili mwezi huu baada y akubomoka kwa nyumba zaidi ya 100 tarehe moja kutokana na mvua, leo tena mvua ya jana usiku imesababisha kufika huko na kujionea jinsi nyumba zaidi ya 10 nyingine zikiwa chini na kuwaacha wananchi kuwa katika sintofahamu nyingine huku lawama zikisalia kwa viongozi wao kuanzia wa manispaa hadi kitaifa.
fuatilia kwa picha hapa matukio yalivyokuwa.
picha na John Banda
askari akisaidiana na wananchi kuhamisha magogo yaliyowekwa njiani na watu wenye asira na viongozi kutokana na kushindwa kuzuia mafuriko hayo yasijirudie tena. |
hayo ndio mazingira ya wakaazi wa mpunguzi yalivyo kwa sasa baada ya mvua ya jana usiku |
No comments
Post a Comment