Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » » MTANZANIA ANAYETUHUMIWA KWA UGAIDI NCHINI KENYA BWANA RASHIDI MBERESERO KESI YAKE YAANZA KUSIKILIZWA.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

  

Mtanzania anayetuhumiwa kwa ugaidi nchini Kenya Rashidi Mberesero

Na Nasri Bakari

Shahidi katika kesi ya shambulio la kigaidi lililofanyika mwaka jana katika Chuo Kikuu cha Garissa, Kenya ameiambia mahakama kuwa Mtanzania Rashidi Mberesero anayetuhumiwa kushiriki, alikuwa akiswali katika msikiti ulio karibu na chuo hicho kwa siku tatu mfululizo.


Kolombo Adao ambaye ni imamu wa Msikiti wa Garissa alidai mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Mlimani, Daniel Ogembo kuwa Mberesero aliondoka katika mazingira ya kutatanisha Aprili 2 mwaka jana huku akiacha begi lake msikitini.


Alikuwa mwerevu mno na aliweza kuisoma Quran. Nilikutana naye mara ya kwanza asubuhi ya Machi 30, 2015 wakati nafungua msikiti,”alieleza shahidi huyo.


Kwa mujibu wa Adao, Mberesero alikuwa muumini wa kipekee kwani kila siku alikuwa akifika msikitini saa 10:35 alfajiri, wakati mwingine kabla ya adhana.


Shahidi huyo alidai kwamba Aprili Mosi mwaka jana alipofungua msikiti asubuhi alimkuta Mberesero akiwa ameshafika na alimpa kipaza sauti aweze kuwaita waumini wanaotakiwa kuswali asubuhi siku hiyo.


Nilikuwa naumwa kifua siku hiyo. Kwa hiyo nilimpa kipaza sauti atangaze kwa sababu alikuwa anaijua vyema Quran, shahidi huyo alidai.


Kuhusu sababu za Mberesero kuwapo Garissa, Adao aliiambia mahakama kuwa aliambiwa na kijana huyo kuwa alikwenda kumsalimia mjomba wake lakini alifukuzwa kwa kuwa ni Mwislamu.


Alinieleza kuwa baba yake ni Mdigo wa Tanga na mama yake ni Mkamba wa Kenya,” alieleza Adao.


Kwa maelezo ya shahidi huyo, siku ya tukio Mberesero ambaye alizoea kuvaa kanzu alionekana amevaa mavazi ya kawaida na kofia kama mtu anayeficha uso.


Mahakama ilielezwa kuwa siku ya tukio aliingia msikitini na kuweka begi lake kwenye kona ya msikiti lakini hakusali na baadaye aliondoka na kuliacha.    

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / / MTANZANIA ANAYETUHUMIWA KWA UGAIDI NCHINI KENYA BWANA RASHIDI MBERESERO KESI YAKE YAANZA KUSIKILIZWA.

  

Mtanzania anayetuhumiwa kwa ugaidi nchini Kenya Rashidi Mberesero

Na Nasri Bakari

Shahidi katika kesi ya shambulio la kigaidi lililofanyika mwaka jana katika Chuo Kikuu cha Garissa, Kenya ameiambia mahakama kuwa Mtanzania Rashidi Mberesero anayetuhumiwa kushiriki, alikuwa akiswali katika msikiti ulio karibu na chuo hicho kwa siku tatu mfululizo.


Kolombo Adao ambaye ni imamu wa Msikiti wa Garissa alidai mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Mlimani, Daniel Ogembo kuwa Mberesero aliondoka katika mazingira ya kutatanisha Aprili 2 mwaka jana huku akiacha begi lake msikitini.


Alikuwa mwerevu mno na aliweza kuisoma Quran. Nilikutana naye mara ya kwanza asubuhi ya Machi 30, 2015 wakati nafungua msikiti,”alieleza shahidi huyo.


Kwa mujibu wa Adao, Mberesero alikuwa muumini wa kipekee kwani kila siku alikuwa akifika msikitini saa 10:35 alfajiri, wakati mwingine kabla ya adhana.


Shahidi huyo alidai kwamba Aprili Mosi mwaka jana alipofungua msikiti asubuhi alimkuta Mberesero akiwa ameshafika na alimpa kipaza sauti aweze kuwaita waumini wanaotakiwa kuswali asubuhi siku hiyo.


Nilikuwa naumwa kifua siku hiyo. Kwa hiyo nilimpa kipaza sauti atangaze kwa sababu alikuwa anaijua vyema Quran, shahidi huyo alidai.


Kuhusu sababu za Mberesero kuwapo Garissa, Adao aliiambia mahakama kuwa aliambiwa na kijana huyo kuwa alikwenda kumsalimia mjomba wake lakini alifukuzwa kwa kuwa ni Mwislamu.


Alinieleza kuwa baba yake ni Mdigo wa Tanga na mama yake ni Mkamba wa Kenya,” alieleza Adao.


Kwa maelezo ya shahidi huyo, siku ya tukio Mberesero ambaye alizoea kuvaa kanzu alionekana amevaa mavazi ya kawaida na kofia kama mtu anayeficha uso.


Mahakama ilielezwa kuwa siku ya tukio aliingia msikitini na kuweka begi lake kwenye kona ya msikiti lakini hakusali na baadaye aliondoka na kuliacha.    


«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :