Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » KOREA KASKAZINI YAITISHIA KOREA KUSINI NA MAREKANI
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post


Korea Kaskazini imetishia kutekeleza mashambulio ya nyuklia dhidi ya Korea Kusini na Marekani iwapo nchi hizo mbili zitaendelea na mazoezi ya pamoja ya kijeshi.

Mazoezi hayo, ambayo hufanyika kila mwaka, mwaka huu yatashirikisha wanajeshi 300,000.
Serikali ya Korea Kaskazini imetoa taarifa ya ikitishia kutekeleza “shambulio la nyuklia kwa ajili ya haki”.

Ni kawaida kwa Pyongyang kutoa vitisho vya aina hiyo na wataalamu wanatilia shaka uwezo wa Korea Kaskazini kuwa na makombora ya nyuklia.

Hisia hupanda kati ya Korea Kaskazini na Korea Kusini na Marekani kila mazoezi hayo ya pamoja ya kijeshi yanapofanyika.

Pyongyang hutazama mazoezi hayo kama mazoezi ya kujiandaa kuivamia.

Mwaka uliopita, Korea Kaskazini ilitishia kugeuza Washington kuwa “bahari ya moto”.

Wizara ya ulinzi ya Korea Kusini imeionya Pyongyang dhidi ya “hatua za haraka zisizo za busara ambazo zinaweza zikailetea maangamizi”.


Mazoezi ya mwaka huu, yanayoshirikisha wanajeshi 300,000 wa Korea Kusini na 15,000 wa Marekani, ndiyo makubwa zaidi kuwahi kufanyika.

Yanaandaliwa siku chache tu baada ya Umoja wa Mataifa kuidhinisha vikwazo vipya dhidi ya Korea Kaskazini kutokana na hatua yake ya kufanyia majaribio bomu la nyuklia na kufyatua makombora.

Korea Kaskazini ilijibu vikwazo hivyo kwa kutangaza itaweka tayari silaha zake za nyuklia na pia ikavyatua makombora ya masafa mafupi baharini.


About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / KOREA KASKAZINI YAITISHIA KOREA KUSINI NA MAREKANI


Korea Kaskazini imetishia kutekeleza mashambulio ya nyuklia dhidi ya Korea Kusini na Marekani iwapo nchi hizo mbili zitaendelea na mazoezi ya pamoja ya kijeshi.

Mazoezi hayo, ambayo hufanyika kila mwaka, mwaka huu yatashirikisha wanajeshi 300,000.
Serikali ya Korea Kaskazini imetoa taarifa ya ikitishia kutekeleza “shambulio la nyuklia kwa ajili ya haki”.

Ni kawaida kwa Pyongyang kutoa vitisho vya aina hiyo na wataalamu wanatilia shaka uwezo wa Korea Kaskazini kuwa na makombora ya nyuklia.

Hisia hupanda kati ya Korea Kaskazini na Korea Kusini na Marekani kila mazoezi hayo ya pamoja ya kijeshi yanapofanyika.

Pyongyang hutazama mazoezi hayo kama mazoezi ya kujiandaa kuivamia.

Mwaka uliopita, Korea Kaskazini ilitishia kugeuza Washington kuwa “bahari ya moto”.

Wizara ya ulinzi ya Korea Kusini imeionya Pyongyang dhidi ya “hatua za haraka zisizo za busara ambazo zinaweza zikailetea maangamizi”.


Mazoezi ya mwaka huu, yanayoshirikisha wanajeshi 300,000 wa Korea Kusini na 15,000 wa Marekani, ndiyo makubwa zaidi kuwahi kufanyika.

Yanaandaliwa siku chache tu baada ya Umoja wa Mataifa kuidhinisha vikwazo vipya dhidi ya Korea Kaskazini kutokana na hatua yake ya kufanyia majaribio bomu la nyuklia na kufyatua makombora.

Korea Kaskazini ilijibu vikwazo hivyo kwa kutangaza itaweka tayari silaha zake za nyuklia na pia ikavyatua makombora ya masafa mafupi baharini.



«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :