Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » MACHIFU WASHIKWA UCHAWI JIJINI MBEYA
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Na. Ezekiel Kamanga,Chunya.

Wanakijiji wa kijiji cha  Ifumbo wilayani Chunya mkoani Mbeya wanawashikilia wazee wa mila(machifu) kwa tuhuma ya  kujihusisha na imani za kishirikina na kutupia majini shuleni na kusababisha wanafunzi kuzimia kwa kile kinachodaiwa uongozi wa shule ya hauwaaliki kwenye mahafali na kuwaheshimu kama machifu wa kijiji.

Wakizungumza  wananchi wa kijiji hicho akiwemo Braisoni Mwansimba walisema kuwa tatizo hilo la kuzimia kwa wanafunzi katika shule hilo lilianza tangu mwaka jana mwezi wa nne na lilianza kwa mtoto mmoja hadi kufikia 20 kwa siku hali iliwashitua wakazi wote kijijini hapo na kwamba wanafunzi  wanapozimia  huwa wanaweweseka  huku wakitembelea tumbo  mithili ya nyoka.

Waliendelea kueleza kuwa kutokana na tatizo hilo kuzidi halmashauri ya kijiji na wananchi wote waliamua kuwaita  wazee hao ili kutatua tatizo hilo lakini wazee hao walisema kuwa wameamua kufanya hivyo kutokana na kwamba uongozi wa shule na kijiji hicho kutowaalika katika pindi mahafali yanapofanyika shuleni halo na shughuli zingine za kijiji na ndio chanzo cha kufanya hivyo shuleni halo.

Akizungumzia suala hilo mkuu wa shule hiyo Malema alisema kuwa kutokana na kuzidi kwa tatizo hilo uongozi wa kijiji uliamua kutafuta ufumbuzi kwa kijiji jirani cha ikukwa na kubaini kuwa wazee wa mila ndio chanzo na ndipo walipoamua kupeleka wagaga wa jadi kutoka mbozi na ikukwa ili wazee hao wanyweshe  dawa ili kuwatoa uchawi na waliponyweshwa hiyo dawa tatizo hilo lilizidi hali iliyowalazimu kuwaita tena.

Aliendelea kueleza kuwa mbali na tatizo hilo kudumu kwa muda mrefu kama mwaka sasa mwenyekiti wa kijiji alipokuwa akiambiawa tatizo bado aliendelea kufumbia macho kwa madai kwamba atakapogombea tena 2020 ataangushwa hadi diwani alipoingilia kati mara baada ya uchaguzi wa octoba 2015.

Aidha diwani  wa kata hiyo Michael Zanzi alifafanua kuwa kutokana na juhudi hizo za kutafuta ufumbuzi katika vijiji jirani tatizo hilo limeweza kupungua kwa kiasi kutoka wanafuzi 20 hadi kufikia mtoto mmoja au wawili kwa siku kwani walifanikisha kuwanyweshwa kabwela wazee waliokuwa wakituhumiwa na kutawapatia dawa za kienyeji wanafunzi wa shule huyo na kwamba siku ya jumapili watakaa na wazee hao ili kuhakikisha tatizo hilo linapungua kama si kuisha kabisa.


About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / MACHIFU WASHIKWA UCHAWI JIJINI MBEYA

Na. Ezekiel Kamanga,Chunya.

Wanakijiji wa kijiji cha  Ifumbo wilayani Chunya mkoani Mbeya wanawashikilia wazee wa mila(machifu) kwa tuhuma ya  kujihusisha na imani za kishirikina na kutupia majini shuleni na kusababisha wanafunzi kuzimia kwa kile kinachodaiwa uongozi wa shule ya hauwaaliki kwenye mahafali na kuwaheshimu kama machifu wa kijiji.

Wakizungumza  wananchi wa kijiji hicho akiwemo Braisoni Mwansimba walisema kuwa tatizo hilo la kuzimia kwa wanafunzi katika shule hilo lilianza tangu mwaka jana mwezi wa nne na lilianza kwa mtoto mmoja hadi kufikia 20 kwa siku hali iliwashitua wakazi wote kijijini hapo na kwamba wanafunzi  wanapozimia  huwa wanaweweseka  huku wakitembelea tumbo  mithili ya nyoka.

Waliendelea kueleza kuwa kutokana na tatizo hilo kuzidi halmashauri ya kijiji na wananchi wote waliamua kuwaita  wazee hao ili kutatua tatizo hilo lakini wazee hao walisema kuwa wameamua kufanya hivyo kutokana na kwamba uongozi wa shule na kijiji hicho kutowaalika katika pindi mahafali yanapofanyika shuleni halo na shughuli zingine za kijiji na ndio chanzo cha kufanya hivyo shuleni halo.

Akizungumzia suala hilo mkuu wa shule hiyo Malema alisema kuwa kutokana na kuzidi kwa tatizo hilo uongozi wa kijiji uliamua kutafuta ufumbuzi kwa kijiji jirani cha ikukwa na kubaini kuwa wazee wa mila ndio chanzo na ndipo walipoamua kupeleka wagaga wa jadi kutoka mbozi na ikukwa ili wazee hao wanyweshe  dawa ili kuwatoa uchawi na waliponyweshwa hiyo dawa tatizo hilo lilizidi hali iliyowalazimu kuwaita tena.

Aliendelea kueleza kuwa mbali na tatizo hilo kudumu kwa muda mrefu kama mwaka sasa mwenyekiti wa kijiji alipokuwa akiambiawa tatizo bado aliendelea kufumbia macho kwa madai kwamba atakapogombea tena 2020 ataangushwa hadi diwani alipoingilia kati mara baada ya uchaguzi wa octoba 2015.

Aidha diwani  wa kata hiyo Michael Zanzi alifafanua kuwa kutokana na juhudi hizo za kutafuta ufumbuzi katika vijiji jirani tatizo hilo limeweza kupungua kwa kiasi kutoka wanafuzi 20 hadi kufikia mtoto mmoja au wawili kwa siku kwani walifanikisha kuwanyweshwa kabwela wazee waliokuwa wakituhumiwa na kutawapatia dawa za kienyeji wanafunzi wa shule huyo na kwamba siku ya jumapili watakaa na wazee hao ili kuhakikisha tatizo hilo linapungua kama si kuisha kabisa.



«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :