Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » WATUMWA LIBYA WANANYOFOLEWA VIUNGO VYAO VYA MWILI
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post


Imebainika kuwa, baadhi ya raia wa Kiafrika wanaopigwa mnada katika magendo ya binadamu nchini Libya wananyofolewa viungo vyao vya mwili na kuuzwa.

Wakili na mwanaharakati mashuhuri Bobby Banson amenukuliwa na tovuti ya habari ya GhanaWeb akisema kuwa, binafsi ameshuhudia kanda ya video inayoonyesha mmoja wa 'watumwa' hao akieleza jinsi viungo vya mwili vya mwenzake vilivyong'olewa na kuuzwa.


Amebainisha kuwa: "Ukweli wa mambo ni kuwa, baadhi ya raia hao wa Afrika hawauzwi kwa ajili ya kwenda kufanya kazi Ulaya, bali kwa ajili ya biashara ya viungo vya binadamu kama maini na mapafu."


Wakili huyo na mtetezi wa haki za binadamu ameongeza kuwa, wahajiri hao waliojikuta kwenye mtego wa magendo ya binadamu wanapewa dawa za kulala na kisha viungo vyao vinachukuliwa."
Wahajiri wa Afrika wanaouzwa kama bidhaa nchini Libya


Hivi karibuni, televisheni ya CNN ilirusha hewani mubashara mnada wa kuuza Waafrika huko nchini Libya ambapo kila mtu alikuwa akiuzwa kwa dola zisizopungua 400 za Kimarekani.
Duru mbali mbali za kimataifa, ukiwemo Umoja wa Afrika na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa zimekosoa vikali biashara hiyo ya utumwa mambo leo inayofanyika nchini Libya.

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / WATUMWA LIBYA WANANYOFOLEWA VIUNGO VYAO VYA MWILI


Imebainika kuwa, baadhi ya raia wa Kiafrika wanaopigwa mnada katika magendo ya binadamu nchini Libya wananyofolewa viungo vyao vya mwili na kuuzwa.

Wakili na mwanaharakati mashuhuri Bobby Banson amenukuliwa na tovuti ya habari ya GhanaWeb akisema kuwa, binafsi ameshuhudia kanda ya video inayoonyesha mmoja wa 'watumwa' hao akieleza jinsi viungo vya mwili vya mwenzake vilivyong'olewa na kuuzwa.


Amebainisha kuwa: "Ukweli wa mambo ni kuwa, baadhi ya raia hao wa Afrika hawauzwi kwa ajili ya kwenda kufanya kazi Ulaya, bali kwa ajili ya biashara ya viungo vya binadamu kama maini na mapafu."


Wakili huyo na mtetezi wa haki za binadamu ameongeza kuwa, wahajiri hao waliojikuta kwenye mtego wa magendo ya binadamu wanapewa dawa za kulala na kisha viungo vyao vinachukuliwa."
Wahajiri wa Afrika wanaouzwa kama bidhaa nchini Libya


Hivi karibuni, televisheni ya CNN ilirusha hewani mubashara mnada wa kuuza Waafrika huko nchini Libya ambapo kila mtu alikuwa akiuzwa kwa dola zisizopungua 400 za Kimarekani.
Duru mbali mbali za kimataifa, ukiwemo Umoja wa Afrika na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa zimekosoa vikali biashara hiyo ya utumwa mambo leo inayofanyika nchini Libya.


«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :