Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » WAZIRI MKUU IRAQ AAHIDI KUIONDOA IS
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post


Waziri mkuu wa Iraq Haider al-Abadi amesema wapiganaji wa Islamic State (IS) watafurushwa kutoka kwa maeneo yote nchini humo.

Hii ni baada ya wanajeshi kufanikiwa kuukomboa mji wa Ramadi kutoka kwa wapiganaji hao.

Kwenye hotuba kupitia runinga, Bw Abadi ameapa kuukomboa mji wa pili kwa ukubwa nchini Iraq, mji wa Mosul, akisema hilo litakuwa “pigo kubwa na la mwisho” kwa IS.

Marekani iyamesifu majeshi ya Iraq kwa kuukomboa mji wa Ramadi.

Waziri wa mashauri ya kigeni wa Marekani John Kerry amesema IS wamepata pito kubwa.

Wapiganaji hao wa Kiislamu waliuteka mji wa Ramadi mwezi Mei, kitendo kilicholiaibisha sana jeshi.
Wanajeshi wa Iraq wamekuwa wakipigana kuukomboa mji huo ulioko kilomita 90 magharibi mwa Baghdad kwa wiki kadha.

Picha zilizoonyeshwa runingani Jumatatu ziliwaonyesha wanajeshi wakipandisha bendera ya Iraq kwenye afisi kuu ya serikali katikati mwa mji huo.

Msemaji wa jeshi Brigidia Jenerali Yahya Rasul amesema wanajeshi hao walikuwa “wameuokomboa” mji wa Ramadi katika ushindi wa kihistoria.

Maafisa wa Iraq hawakutoa idadi yoyote kuhusu waliofariki kwenye vita hivyo.

"2016 utakuwa mwaka wa ushindi mkubwa na wa kabisa, pale Daesh (IS) watakapotimuliwa kutoka Iraq,” alisema Bw Abadi kwenye runinga.

"Twaja kuukomboa mji wa Mosul na hilo litakuwa pigo kubwa na la kuangamisa Daesh (nchini Iraq),” akaongeza.

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / WAZIRI MKUU IRAQ AAHIDI KUIONDOA IS


Waziri mkuu wa Iraq Haider al-Abadi amesema wapiganaji wa Islamic State (IS) watafurushwa kutoka kwa maeneo yote nchini humo.

Hii ni baada ya wanajeshi kufanikiwa kuukomboa mji wa Ramadi kutoka kwa wapiganaji hao.

Kwenye hotuba kupitia runinga, Bw Abadi ameapa kuukomboa mji wa pili kwa ukubwa nchini Iraq, mji wa Mosul, akisema hilo litakuwa “pigo kubwa na la mwisho” kwa IS.

Marekani iyamesifu majeshi ya Iraq kwa kuukomboa mji wa Ramadi.

Waziri wa mashauri ya kigeni wa Marekani John Kerry amesema IS wamepata pito kubwa.

Wapiganaji hao wa Kiislamu waliuteka mji wa Ramadi mwezi Mei, kitendo kilicholiaibisha sana jeshi.
Wanajeshi wa Iraq wamekuwa wakipigana kuukomboa mji huo ulioko kilomita 90 magharibi mwa Baghdad kwa wiki kadha.

Picha zilizoonyeshwa runingani Jumatatu ziliwaonyesha wanajeshi wakipandisha bendera ya Iraq kwenye afisi kuu ya serikali katikati mwa mji huo.

Msemaji wa jeshi Brigidia Jenerali Yahya Rasul amesema wanajeshi hao walikuwa “wameuokomboa” mji wa Ramadi katika ushindi wa kihistoria.

Maafisa wa Iraq hawakutoa idadi yoyote kuhusu waliofariki kwenye vita hivyo.

"2016 utakuwa mwaka wa ushindi mkubwa na wa kabisa, pale Daesh (IS) watakapotimuliwa kutoka Iraq,” alisema Bw Abadi kwenye runinga.

"Twaja kuukomboa mji wa Mosul na hilo litakuwa pigo kubwa na la kuangamisa Daesh (nchini Iraq),” akaongeza.

«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :