Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » WANA CCM ZANZIBAR WATAKIWA KUJIANDAA NA UCHAGUZI WA MARUDIO
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post


Chama cha Mapinduzi kimewataka wanachama wake visiwani Zanzibar kujiandaa kwa marudio ya uchaguzi.

Tamko hilo limetolewa huku mazungumzo hakiendelea kutafuta suluhu ya mzozo kuhusu matokeo ya uchaguzi wa Oktoba 25 ambayo yalifutiliwa mbali.

Wito wa wafuasi kujiandaa kwa marudio ya uchaguzi umetolewa baada ya kikao cha kamati maalum ya halmashauri kuu ya taifa ya CCM Zanzibar katika afisi kuu za chama Kisiwandui.

“Kikao kimewataka wana CCM kujiimarisha, kujiweka tayari na hatimaye kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi wa marudio, ili kukiletea ushindi wa kishindo Chama Cha Mapinduzi Zanzibar kuanzia Rais, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Madiwani wakati utakapowadia,” taarifa iliyotolewa baada ya mkutano huo inasema.

Chama hicho hata hivyo kinasema kinaridhishwa na mazungumzo yanayoendelea kuhusu mzozo huo Zanzibar.

“Kikao pia kimeridhia majadiliano yanayoendelea kuhusu hali ya Kisiasa Zanzibar yanayoshirikisha Viongozi kadhaa wakiwemo Marais Wastaafu wa Zanzibar,” taarifa hiyo, iliyotolewa na katibu wa kamati maalum ya halmashauri hiyo Bw Waride Bakari Jabu inaongeza.

Jumamosi, Rais wa Muungano wa Tanzania John Magufuli alikutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein.

Akizungumza baada ya mkutano huo, Dkt Shein alisema lengo la mazungumzo hayo ilikuwa ni kumpasha Rais Magufuli juu ya hali ya mazungumzo ya kisiasa Zanzibar.

Mazungumzo hayo yalianza tarehe 9 Novemba na, kwa mujibu wa Dkt Shein, bado yanaendelea.

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / WANA CCM ZANZIBAR WATAKIWA KUJIANDAA NA UCHAGUZI WA MARUDIO


Chama cha Mapinduzi kimewataka wanachama wake visiwani Zanzibar kujiandaa kwa marudio ya uchaguzi.

Tamko hilo limetolewa huku mazungumzo hakiendelea kutafuta suluhu ya mzozo kuhusu matokeo ya uchaguzi wa Oktoba 25 ambayo yalifutiliwa mbali.

Wito wa wafuasi kujiandaa kwa marudio ya uchaguzi umetolewa baada ya kikao cha kamati maalum ya halmashauri kuu ya taifa ya CCM Zanzibar katika afisi kuu za chama Kisiwandui.

“Kikao kimewataka wana CCM kujiimarisha, kujiweka tayari na hatimaye kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi wa marudio, ili kukiletea ushindi wa kishindo Chama Cha Mapinduzi Zanzibar kuanzia Rais, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Madiwani wakati utakapowadia,” taarifa iliyotolewa baada ya mkutano huo inasema.

Chama hicho hata hivyo kinasema kinaridhishwa na mazungumzo yanayoendelea kuhusu mzozo huo Zanzibar.

“Kikao pia kimeridhia majadiliano yanayoendelea kuhusu hali ya Kisiasa Zanzibar yanayoshirikisha Viongozi kadhaa wakiwemo Marais Wastaafu wa Zanzibar,” taarifa hiyo, iliyotolewa na katibu wa kamati maalum ya halmashauri hiyo Bw Waride Bakari Jabu inaongeza.

Jumamosi, Rais wa Muungano wa Tanzania John Magufuli alikutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein.

Akizungumza baada ya mkutano huo, Dkt Shein alisema lengo la mazungumzo hayo ilikuwa ni kumpasha Rais Magufuli juu ya hali ya mazungumzo ya kisiasa Zanzibar.

Mazungumzo hayo yalianza tarehe 9 Novemba na, kwa mujibu wa Dkt Shein, bado yanaendelea.

«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :