Baada ya
kusimama kwa wiki mbili kupisha michuano ya Kombe la Mapinduzi visiwani
Zanzibar, Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania mzunguko wa kumi na nne (14) unatarajiwa
kuendelea wikiendi hii kwa michezo 8 kuchezwa katika viwanja mbalimbali, huku
timu 16 zikichuana kusaka pointi 3 muhimu.
Jumamosi
uwanja wa Karume jijini Dar es salaam, Maafande wa JKT Ruvu watawakaribisha
Maafande wa Mgambo Shooting, Toto Africans watawakaribisha Tanzania Prisosns
uwanja wa CCM Kirumba, huku Stand United wakicheza dhidi ya Kagera Sugar uwanja
wa Kamabarage mjini Shinyanga.
Uwanja wa
Tafa jijini Dar es salaam, Simba SC watawakaribisha wakata miwa wa Mtibwa Sugar
saa 10 jioni, Mbeya City watakua wenyeji wa Mwadui FC uwanja wa Sokoine jijini
Mbeya, Coastal Union dhidi ya Majimaji uwanja wa Mkwakwani, huku mchezo kati ya
Azam FC dhidi ya African Sports ukianza saa 1 usiku.
Jumapili
ligi hiyo itaendelea kwa mchezo mmoja uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam,
ambapo Young African watawakaribisha Ndanda FC kutoka Mtwara.
No comments
Post a Comment