Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos

» » VIJANA WA VYUO VIKUU WATAKIWA KUWAKUMBUKA WENYE UHITAJI MAALUMU NCHINI BADALA YA KUJITUPA KATIKA ANASA
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Na Peter Mkwavila.....Dodoma

VIJANA wanaosoma vyuo vikuu wameshauriwa kuwakumbuka watu wenye mahitaji maalumu katika kuwapatia misaada mbalimbali badala ya kuelekeza kwenye mambo ya anasa.


Ushauri huo umetolewa na jana,Mjini hapa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa Chuo cha Mipango(IRDP) Veronica Mwembezi wakati alipokuwa wakikabidhi misaada mbalimbali kwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi wa kituo cha Upendo Miyuji.


Aliitaja misaada iliyotolewa na jumuiya hiyo ya wanawake ni pamoja na vyakula vikiwemo unga wa kula,sukari,mchele,mafuta ya kula na nguo vyote vikigharimu zaidi ya laki tano..


Alisema jamii ya watu wenye mahitaji maalumu wanachangamoto nyingi zikiwemo za kiafya na kielimu ambazo vijana wasomi wa vyuo vikuu wanaweza kuzitatua kwa kujitoa kifedha na kimali pia.


“Lakini cha kusikitisha leo hii vijana hao wasomi walio wengi wapo tayari kujitoa kwenye burudani ya mambo ya anasa,badala ya kuelekeza kwa watu hao wenye mahitaji maalumu kama vile watoto wanaoishi katika mazingira magumu,yatima,wajane, wazee na wale wanaoishi na viruzi vya ukimwi”alisema.


Hata hivyo kwa upande wa serikali pia imetakiwa kuongeza nguvu kwa taaisisi mbalimbali zinazojishughulisha na kuwasaidia jamii ya watu wenye mahitaji hayo.


Kwa upande wake msimamizi wa kituo hicho ya watoto Br Getachew ameviomba vyuo vikuu vingine kuviangalia vituo hivyo vya kulelea watoto kwa jicho la huruma kutokana na hali mbaya iliyopo ya uendeshaji.


Alisema kuwa kwa asilimia kubwa ya vituo vyenye mahitaji maalumu  vimekuwa vikikabiliana na changamoto ya ukosefu wa misaada mbalimbali ikiwemo kwa upande wa elimu afya na hata kwenye mavazi pia.

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

/ / VIJANA WA VYUO VIKUU WATAKIWA KUWAKUMBUKA WENYE UHITAJI MAALUMU NCHINI BADALA YA KUJITUPA KATIKA ANASA

Na Peter Mkwavila.....Dodoma

VIJANA wanaosoma vyuo vikuu wameshauriwa kuwakumbuka watu wenye mahitaji maalumu katika kuwapatia misaada mbalimbali badala ya kuelekeza kwenye mambo ya anasa.


Ushauri huo umetolewa na jana,Mjini hapa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa Chuo cha Mipango(IRDP) Veronica Mwembezi wakati alipokuwa wakikabidhi misaada mbalimbali kwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi wa kituo cha Upendo Miyuji.


Aliitaja misaada iliyotolewa na jumuiya hiyo ya wanawake ni pamoja na vyakula vikiwemo unga wa kula,sukari,mchele,mafuta ya kula na nguo vyote vikigharimu zaidi ya laki tano..


Alisema jamii ya watu wenye mahitaji maalumu wanachangamoto nyingi zikiwemo za kiafya na kielimu ambazo vijana wasomi wa vyuo vikuu wanaweza kuzitatua kwa kujitoa kifedha na kimali pia.


“Lakini cha kusikitisha leo hii vijana hao wasomi walio wengi wapo tayari kujitoa kwenye burudani ya mambo ya anasa,badala ya kuelekeza kwa watu hao wenye mahitaji maalumu kama vile watoto wanaoishi katika mazingira magumu,yatima,wajane, wazee na wale wanaoishi na viruzi vya ukimwi”alisema.


Hata hivyo kwa upande wa serikali pia imetakiwa kuongeza nguvu kwa taaisisi mbalimbali zinazojishughulisha na kuwasaidia jamii ya watu wenye mahitaji hayo.


Kwa upande wake msimamizi wa kituo hicho ya watoto Br Getachew ameviomba vyuo vikuu vingine kuviangalia vituo hivyo vya kulelea watoto kwa jicho la huruma kutokana na hali mbaya iliyopo ya uendeshaji.


Alisema kuwa kwa asilimia kubwa ya vituo vyenye mahitaji maalumu  vimekuwa vikikabiliana na changamoto ya ukosefu wa misaada mbalimbali ikiwemo kwa upande wa elimu afya na hata kwenye mavazi pia.

«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments :