Kikosi cha timu ya taifa ya Wales ambacho nahodha wake ni Gareth Bale tayari kimeanika kambi yake.
Kambi hiyo itakuwa ni kwa ajili ya michuano ya Euro 2016 itakayofanyika nchini Ufaransa katikati ya mwaka huu.
Chini
ya Kocha Chris Coleman, kikosi hicho kitaweka kambi katika enero la
pwani ya Resort of Dinard maarufu kama 'Cannes of the North' ili
kuwafanya wachezaji kutulia kabisa na kujiandaa vya kutosha.
Tayari
Bale anayekipiga Real Madrid aliishasema kwamba wanakwenda kupambana na
kufanya vema na si washiriki tu kama ambavyo wengi wamekuwa
wakiwafikiria.
No comments
Post a Comment