Kiasi ya watu 40 wameuwawa baada ya kundi la wanamgambo wa Kiislamu la al-Shabaab kuivamia kambi ya jeshi la kulinda amani ya Umoja wa Afrika kusini magharibi ya Somalia mapema leo.
Wengi wa waliouwawa katika shambulio hilo katika kambi hiyo iliyoko katika kijiji cha El-Adde katika jimbo la Gedo ni wanajeshi wa Kenya walioko katika jeshi la AU.
Mohammed Hussein Al_qadi , naibu gavana wa jimbo la Gedo ameliambia shirika la habari la Ujerumani DPA kwamba ni shambulio kubwa kufanywa na al-Shabaab wakitumia washambuliji wanne wa kujitoa muhanga katika gari.
Kamishina wa mji wa El-Adde , Ali Abdi , ameliambia shirika la dpa kwamba wanajeshi kutoka Kenya na Somalia pamoja na wapiganaji wa kundi la al-Shabaab wameuwawa katika shambulio hilo.
No comments
Post a Comment